Mashahidi waripoti milio ya risasi hospitalini Al – Shifa huku Israel ikisema vikosi maalum vinaisaka hospitali hiyo
Wanajeshi wa Israel wanaendelea kufanya msako katika ghorofa moja hadi nyengine katika hospitali ya Al - Shifa , wakati mamia ya wagonjwa na wafanyikazi wa matibabu wakisalia hospitalini humo
Moja kwa moja
ANC yaunga mkono wito wa kutaka ubalozi wa Israel mjini Pretoria ufungwe
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, Waafrika kusini wakifanya maandamano ya kutaka ubalozi wa Israel kufungwa nchini humo
Chama tawala nchini Afrika Kusini ANC kimesema
kitaunga mkono hoja ya upinzani bungeni "ya kufunga ubalozi wa Israel
nchini Afrika Kusini na kusimamisha uhusiano wote wa kidiplomasia na nchi hiyo
hadi ikubali kusitishwa kwa mapigano".
ANC pia imesema inatarajia Israel "kujitolea kuheshimu
mazungumzo yaliyowezeshwa na Umoja wa Mataifa".
Chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF) pia
kinatoa wito wa kusitishwa kwa uhusiano wote wa kidiplomasia na Israel kwa
mshikamano na watu wa Palestina.
Huruma ya Afrika Kusini kwa mapambano ya Wapalestina kwa
ajili ya taifa huru ilianza katika siku za kiongozi wa kupinga ubaguzi wa rangi
Nelson Mandela.
Bunge la Kenya launga mkono askari wa Kenya kupelekwa Haiti licha ya kesi mahakamani
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, Polisi wa Kenya
Bunge la Kenya limeidhinisha mpango tata wa serikali
kupeleka takriban maafisa 1,000 wa polisi nchini Haiti kusaidia kukomesha
ghasia za magenge.
Hii ni licha ya amri ya mahakama inayozuia askari hao
kutumwa nchini haiti, ikisubiri matokeo ya pingamizi la kisheria mahakamani.
Wabunge wa upinzani walilaani kura hiyo, lakini chama tawala
kilitumia wingi wake kuunga mkono serikali kufuatia mjadala mkali.
Haiti ilikuwa imeomba msaada wa kimataifa ili kukabiliana na
ongezeko la uvunjaji sheria.
Ofa ya Kenya ilipata kibali cha Baraza la Usalama la Umoja
wa Mataifa mwezi uliopita, lakini mpango huo umepingwa na chama kikuu cha
upinzani.
Takriban magenge 300 yanafanya kazi nchini Haiti na asilimia
80 ya mji mkuu, Port-au-Prince, uko chini ya udhibiti wa magenge hayo.
Makundi haya yamechukua udhibiti mkubwa wa mji huo tangu
mauaji ya rais wa nchi hiyo mnamo 2021 yalipoiweka Haiti katika mzozo wa
kisiasa.
Katika upigaji kura wa Alhamisi katika bunge la Kenya,
wabunge wanaounga mkono hoja hiyo walisema kuwa nchi hiyo ni sehemu ya jumuiya
ya kimataifa na haiwezi kupuuza maombi ya kuomba msaada kutoka kwa mataifa
mengine.
Pia walisema kuwa taifa hilo la Afrika Mashariki lina
historia ya misheni za kulinda amani kama vile Somalia, Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo na Sierra Leone.
Bunge liliidhinisha mpango huo katika muda mfupi wa kupiga
kura kabla ya Mahakama Kuu kuanza
kusikiliza kesi hiyo.
Chama kidogo cha upinzani, Thirdway Alliance, kimeongoza
changamoto hiyo ya kisheria, kikisema mpango huo haukuwa wa katiba kwa sababu
ni wanajeshi pekee wanaoweza kutumwa nje ya nchi.
Serikali imekataa
hoja hiyo, na inatetea kesi hiyo.
Marekani na China zakubali kuanza tena mawasiliano ya kijeshi baada ya mkutano
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Rais Joe Biden na mwenzake wa China Xi jinping
Marekani na china zimekubaliana kuendelea na mawasiliano ya
kijeshi katika juhudi za kupunguza
wasiwasi uliopo, rais Joe Biden amesema.
"Tumerudi katika mawasiliano ya moja kwa moja, na yalio
wazi," alisema kufuatia mkutano nadra na Rais wa China Xi Jinping huko
California Jumatano.
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa wawili hao kuzungumza ana kwa
ana kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Lakini bado kulikuwa na dalili za mvutano kati ya wawili hao
- Bw Biden alirudia maoni yake kwamba Bw Xi ni dikteta.
Wizara ya mambo ya nje ya China baadaye ilikosoa matamshi
hayo, lakini hayaonekani kuwa yameondoa kile ambacho pande zote mbili
zinaonyesha kama mkutano wenye mafanikio makubwa.
Bw Biden pia alisema viongozi wote wawili wamekubaliana
kuanzisha njia ya moja kwa moja ya mawasiliano kati yao.
Katika mkutano na waandishi wa habari kufuatia mkutano huo,
ambao ulifanyika katika eneo la kihistoria la nchi karibu na San Francisco, Bw
Biden alisema ukosefu wa mawasiliano ni "jinsi ajali zinavyotokea" na
akaongeza kuwa marais wote wawili sasa wanaweza "kuchukua simu na
kusikilizwa moja kwa moja. "
Jaribio la dawa latoa matumaini kwa wagonjwa wenye TB sugu
Majaribio mawili muhimu ya kimatibabu yameonyesha kuwa dawa
za antibiotic zinaweza kuzuia kifua kikuu sugu (MDR-TB) miongoni mwa watoto na watu wazima.
Watafiti kutoka Kituo cha TB cha Desmond Tutu katika Chuo
Kikuu cha Stellenbosch nchini Afrika Kusini walitangaza mjini Paris kwamba
dawa, aina ya levofloxacin, inayotolewa mara moja kwa siku kwa watoto zaidi ya
miezi sita, ilikuwa salama sana.
Zaidi ya watu nusu milioni hupata MDR-TB kila mwaka. Ni vigumu kutibu kwa dawa za sasa na
gharama ni kubwa.
Watafiti wa
mojawapo ya tafiti hizo mbili wanasema wamepata njia ya kuwalinda watoto kwa
usalama wakati mtu mzima nyumbani anaugua maradhi hayo.
Katika jaribio la
TB-CHAMP lililofanywa nchini Afrika Kusini, watoto 453 ambao walikuwa wameambukizwa
na mtu mzima TB walipewa levofloxacin. Ni watano tu ndio waliopata ugonjwa
huo.
Utafiti wa pili,
wa majaribio ya V-QUIN, uligundua kuwa levofloxacin ilipunguza hatari ya watu
wazima na vijana kupata MDR-TB kwa 45%.
Habari za hivi punde, Israel inasema wanajeshi wake wanasaka ghorofa hadi ghorofa katika hospitali ya Al-Shifa
Kama ambavyo tumekuwa
tukiripoti, mtu aliyeshuhudia tukio hilo ameripoti ufyatuaji wa risasi katika hospitali ya Al-Shifa ya Gaza.
Tumekuwa na taarifa mpya kutoka kwa afisa kutoka Jeshi la
Ulinzi la Israeli.
Wanasema wanajeshi kutoka kikosi maalum "wanaendelea
kufanya operesheni" katika hospitali hiyo. Operesheni hiyo inaelezwa kuwa
"tata na inayoendelea"
Afisa huyo pia anasema kwamba "askari wanaendelea kufanya
msako katika ghorofa moja hadi nyengine, wakati mamia ya wagonjwa na
wafanyikazi wa matibabu wakisalia kwenye eneo hilo".
Afisa huyo huyo anakariri madai ya IDF kwamba kuna
"miundombinu ya kigaidi iliyofichwa katika eneo hilo" - jambo ambalo
Hamas inakanusha.
Na tena wanasema
wamepata silaha na "nyenzo za kijasusi" - pamoja na "vituo vya
amri na udhibiti na vifaa vya mawasiliano" mali ya Hamas.
Habari za hivi punde, Shahidi mmoja katika hospitali ya Al-Shifa asema kuwa wanajeshi walifyatua risasi
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, Hospitali ya Al Shifa
Mawasiliano ya ripota wetu huko Gaza anasema kumekuwa na
ufyatuaji risasi katika hospitali ya Al-Shifa.
Khader, mwandishi wa habari ndani ya Al-Shifa, alipigiwa
simu na mwandishi wa BBC Rushdi Abualouf - ambapo alisema: "Askari wako
kila mahali, wakipiga risasi kila upande."
Alisema wanajeshi "wamevamia idara zote" za
hospitali hiyo, na kuharibu sehemu ya kusini ya ukuta wa jengo hilo na makumi
ya magari.
Tunasubiri taarifa zaidi kuhusu hatua hiyo ilioripotiwa. BBC
haikuweza kuithibitisha kwa uhuru.
Wanajeshi wa Israel waliingia hospitalini zaidi ya saa 36
zilizopita. Jana usiku, walisema
walikuwa "wanaendelea na operesheni sahihi na iliyowalenga Hamas"
Mbwa anusurika wiki 10 katika milima ya Colorado kando ya mmiliki wake aliyekufa
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Milima
Mbwa ambaye alipatikana akiwa hai kando ya maiti ya mmiliki
wake wiki 10 baada ya kutoweka katika milima ya Colorado alinusurika kwa
kuwinda wanyama wadogo, waokoaji walisema.
Rich Moore, 71, pamoja na Jack Russell terrier, Finney,
walikuwa wamepanga kupanda Blackhead Peak tarehe 19 Agosti, lakini hawakurudi
nyumbani.
Mwili wa Bw Moore
ulipatikana tarehe 30 Oktoba, na Finney kando yake.
Waokoaji walisema
ni "hadithi nzuri ya kunusurika".
Delinda
VanneBrightyn, wa kikundi cha kujitolea cha Taos Search and Rescue, alisema
waokoaji walifanya msako usio na mafanikio wa siku nyingi katika upande wa
magharibi wa mlima huo
Wiki kadhaa
baadaye mwindaji mmoja alipata mwili wa Bw Moore katika Milima ya San Juan -
takriban maili 1.5 (2.5km) mashariki mwa kilele - huku Finney akiwa bado hai
lakini akiwa na uzani wa takriban pauni sita, karibu nusu ya uzito wake wa
awali.
Kikosi cha
uokoaji kilisafirishwa siku iliyofuata. Finney alipelekwa kwa daktari wa mifugo
na sasa yuko na familia ya Bw Moore.
Mshauri wa zamani anasema Marekani inabadilisha jinsi inavyoichukulia Israel
Msaidizi mkuu wa zamani wa kisiasa wa Marekani anasema ameona "urekebishaji" katika
wiki chache zilizopita kwa jinsi utawala wa Biden unavyomchukulia mshirika wake
Israeli.
Ben Rhodes, ambaye alikuwa naibu mshauri wa usalama wa taifa
chini ya Rais Obama, alipendekeza utawala wa sasa hapo awali ulitumai kuwa
unaweza kuwa na athari katika operesheni ya kijeshi ya Israel kwa "kumkumbatia"
Waziri Mkuu wa nchi hiyo Benjamin Netanyahu na serikali yake.
Lakini hili halijathibitishwa, aliiambia BBC Radio 4 asubuhi
ya leo. Rhodes alibainisha kuwa Marekani iliomba kusitisha vita ili kuruhusu misaada
ya kibinadamu lakini Israel "imepuuza kwa kiasi kikubwa ushauri huo".
Rhodes alipendekeza hii ilionyesha tofauti iliopo kati ya
nchi hizo mbili, ingawa alisema Marekani "bado inaunga mkono kwa
ujumla".
Unaweza pia kusoma:
Hezbollah yaonya vita vya kikanda ikiwa mashambulizi Gaza yataendelea
Mtoto mmoja huuawa kila baada ya dakika kumi Gaza
Nchi ya Amerika Kusini ambayo ina jamii kubwa zaidi ya Wapalestina nje ya Ulimwengu wa Kiarabu na Israeli
'Ninapiga simu kutoka shirika la ujasusi la Israel.Tunarusha bomu, una saa mbili kuondoka’
Vita vya Israel na Gaza: Je, uhalifu wa kivita unatekelezwa?, sheria inasemaje?
Israel yaonya watu kuondoka maeneo ya kusini mwa Gaza
Vikosi vya Israel vilidondosha vijikaratasi katika eneo la Khan Younis kusini mwa Gaza
usiku kucha, vikiwaonya watu katika miji minne kuhama makazi yao na kuelekea
kwenye hifadhi, Reuters na Times of Israel yanaripoti.
Vikaratasi hivyo vilionya watu kutafuta usalama katika maeneo ya Bani Shuhaila,
Khuzaa, Abassan na Qarara - miji ambayo ilikuwa na watu zaidi ya 100,000, kabla
ya kusini kuzidiwa na idadi ya watu waliokimbia makazi.
"Kwa usalama wako, unahitaji kuhama mara moja kwenye
makazi yako na kuelekea kwenye makazi yanayojulikana. Mtu yeyote aliye karibu
na magaidi au vituo vyao anaweka maisha yake hatarini, na kila nyumba
inayotumiwa na magaidi italengwa," vijikaratasi hivyo vilisema, kulingana
na Reuters. .
Wiki zilizopita, vijikaratasi kama hivyo vilirushwa
kaskazini mwa Gaza kabla ya mashambulizi ya ardhini.
Pia siku ya Alhamisi asubuhi, wizara ya mambo ya ndani ya
Gaza inayoendeshwa na Hamas ilisema helikopta za Israel "zimeshambulia
nyumba za raia mashariki mwa Khan Younis".
Mnamo Oktoba, idadi ya watu wa Khan Younis ilitoka kwa
wakaazi 400,000 hadi zaidi ya milioni huku mamia ya maelfu wakiondoka kaskazini
mwa Gaza.
Chanzo cha picha, Reuters
Hiki ndicho ilichopata Israel chini ya hospitali ya Al-Shifa
Chanzo cha picha, IDF
Kama tulivyoripoti, wanajeshi wa Israel wanaendelea na msako
wao katika hospitali ya Al-Shifa katika Jiji la Gaza - kituo kikubwa zaidi cha
matibabu katika Ukanda wa Gaza.
Mwishoni mwa mwezi uliopita, Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF)
lilishutumu Hamas kwa kuwa na kambi yake kuu chini ya Al-Shifa. Ilitoa picha ambayo lilitumia 3D kuibua mtandao unaodaiwa kuwa na
mahandaki chini ya ardhi .
Msemaji alisema kulikuwa na uhusiano kutoka hospitali na mahandaki,
na walikuwa na "ushahidi halisi" kwamba "mamia" ya
wapiganaji wa Hamas walikuwa wamejificha katika hospitali baada ya mashambulizi
dhidi ya Israeli tarehe 7 Oktoba.
Marekani baadaye ilisema taarifa zake za kijasusi
zilithibitisha taarifa za Israel kuhusu matumizi ya hospitali hiyo na Hamas -
ingawa Hamas imekuwa ikikanusha.
Israel ilisema wanajeshi wake waliingia katika hospitali
hiyo takriban saa 36 zilizopita. Wamemruhusu mwandishi wa BBC Lucy Williamson
ndani, wakionyesha vitu ambavyo wanasema wamevipata - ikiwa ni pamoja na
bunduki 15, vesti za kuzuia risasi na vitu vingine ikiwa ni pamoja na kompyuta
ndogo.
IDF bado haijaonyesha ushahidi wa kituo cha Hamas au handaki
chini ya hospitali kama ilivyosema awali.
Unaweza pia kusoma:
Hezbollah yaonya vita vya kikanda ikiwa mashambulizi Gaza yataendelea
Mtoto mmoja huuawa kila baada ya dakika kumi Gaza
Nchi ya Amerika Kusini ambayo ina jamii kubwa zaidi ya Wapalestina nje ya Ulimwengu wa Kiarabu na Israeli
'Ninapiga simu kutoka shirika la ujasusi la Israel.Tunarusha bomu, una saa mbili kuondoka’
Vita vya Israel na Gaza: Je, uhalifu wa kivita unatekelezwa?, sheria inasemaje?
Afrika Kusini yaishtaki Israel katika mahakama ya ICC
Chanzo cha picha, Reuters
Afrika Kusini imeishitaki serikali ya Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kufuatia jukumu lake katika mzozo wa Gaza, Rais Cyril Ramaphosa alisema Jumatano.
"Afrika Kusini, kama nchi nyingine nyingi duniani, tumeona inafaa kuishshtaki serikali ya Israel kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Tumetuma rufaa kwa sababu tunaamini kuwa uhalifu wa kivita unafanywa huko," Rais Ramaphosa alisema
Hakufichua nchi nyingine zilizoshtaki Israel ICC.
Aliongeza kuwa hawakuunga mkono shambulio la awali la Hamas dhidi ya Israel lakini wanapinga hatua zinazoendelea za Israel, ambazo "wanaamini kwamba uchunguzi unastahili kufanywa na ICC".
ICC ni mahakama ya kimataifa ambayo inachunguza na kuwahukumu watu binafsi wanaotuhumiwa kufanya uhalifu mkubwa unaotia wasiwasi jumuiya ya kimataifa, kama vile uhalifu wa kivita au mauaji ya halaiki.
Afrika Kusini imekuwa moja ya wafuasi wengi wa Wapalestina katika mzozo unaoendelea na Israel.
Viongozi kadhaa wa nchi hiyo wamewaunga mkono hadharani Wapalestina na pia kumekuwa na maandamano ya kuunga mkono Palestina.
Tazama: Ufyatuaji wa mizinga ya heshima kwa ajili ya sherehe ya miaka 75 ya kuzaliwa ya Mfalme charles III
Maelezo ya video, Tazama: ufyatuaji wa mizinga ya bunduki ya heshma kwa ajili ya sherehe ya miaka 75 ya kuzaliwa ya Mfalme charles III
Kasri la Buckingham liliadhimisha
miaka 75 ya kuzaliwa kwa Mfalme Charles
III kwa kufyatua mizinga ya bunduki 41. Tukio
hilo lilitekelezwa na Kikosi cha Wanajeshi wa Kifalme cha Kivita cha London Green Park.
Itakuwa
mojawapo ya salamu za bunduki siku ya Jumanne kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa
Mfalme, ikiwa ni pamoja na milio 62
katika Mnara wa London (Tower of London)
Mfalme
Charles atatumia siku hiyo kufanya shughuli za umma, na baadaye ataandaa hafla
ya mamia ya wauguzi na wakunga, kama sehemu ya sherehe za kuadhimisha miaka 75
tangu kuanzishwa kwa Huduma ya Kitaifa ya Afya.
Malawi yasitisha safari zote za kiserikali nje ya nchi
Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Malawi Lazarus Chakwera amesitisha safari zote za kimataifa zinazomhusisha yeye na maafisa wote wa serikali.
Pia amewaagiza mawaziri wote walioko nje ya nchi kwa sasa kurejea nyumbani.
Akihutubia taifa kupitia televisheni Jumatano usiku, pia alitangaza vikwazo vya usafiri wa ndani na kupunguza kwa nusu ya mgao wa mafuta kwa mawaziri na maafisa wakuu wa serikali.
Hatua hizo zitadumishwa hadi mwisho wa mwaka wa fedha mnamo Machi 2024.
Baadhi ya hatua kama hizo za kubana matumizi pia zilitangazwa wakati wa janga la Covid lakini zilikuwa na athari ndogo kwani hazikutekelezwa kikamilifu.
Rais alimtaka waziri wa fedha kuweka masharti ya nyongeza ya mishahara kwa watumishi wote wa umma katika mapitio yajayo ya bajeti.
Biden 'ana matumaini kidogo' kuhusu kuachiliwa kwa mateka wa Gaza
Chanzo cha picha, Reuters
Rais wa Marekani Joe Biden anasema
"ana matumaini kidogo" kuwa kutakuwa na mpango wa kuwakomboa zaidi ya
watu 200 wanaoshikiliwa mateka Gaza.
Aliuambia mkutano na waandishi wa habari California hapo awali kwamba hakutaka
kuzungumza kabla ya wakati wake lakini kwamba Marekani imeona "ushirikiano
mkubwa" kutoka kwa Qatar, ambayo imekuwa ikiongoza mazungumzo
yanayoendelea kati ya Israel na Hamas.
Akizungumzia operesheni ya hivi karibuni ya Israel katika hospitali kubwa zaidi ya Gaza
- Al-Shifa - rais huyo wa Marekani anasema Hamas ilifanya "uhalifu wa
kivita" kwa kuwa na kituo chini yake.
Israel imeonyesha kile inachodai kuwa ni silaha na vifaa vingine vya Hamas
ambavyo vilipatikana kutoka hospitalini.
Hamas inakanusha kuwa inatumia vituo vya matibabu kama ngome ya harakati
zake za kijeshi dhidi ya Israel.
Biden anasema Marekani imeitaka Israel kuwa makini , kuhakikisha kuwa raia
wanakuwa salama wakati wa kuzisaka ngome za Hamas.
Unaweza pia kusoma:
Hezbollah yaonya vita vya kikanda ikiwa mashambulizi Gaza yataendelea
Mtoto mmoja huuawa kila baada ya dakika kumi Gaza
Nchi ya Amerika Kusini ambayo ina jamii kubwa zaidi ya Wapalestina nje ya Ulimwengu wa Kiarabu na Israeli
'Ninapiga simu kutoka shirika la ujasusi la Israel.Tunarusha bomu, una saa mbili kuondoka’
Vita vya Israel na Gaza: Je, uhalifu wa kivita unatekelezwa?, sheria inasemaje?
Polisi Washington wajeruhiwa katika maandamano ya uungaji mkono wa Wapalestina
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Polisi wa mjini Washnton Marekani wakijaribu kuwaondoa waandamanaji kutoka makao makuu ya DNC wakati wa maandamano
Polisi wanasema
kuwa takriban maafisa sita wamejeruhiwa baada ya waandamanaji wengi kukabiliana
na mamlaka nje ya ofisi za Kamati ya Kitaifa ya Kidemokrasia (DNC) mjini
Washington.
Maafisa waliokuwa
wamevalia zana za kudhibiti ghasia
walitumia pilipili ili kuwatawanya waandamanaji hao waliokuwa wakitaka
kusitishwa kwa shughuli za kijeshi za Israel Gaza.
Takriban mtu
mmoja amekamatwa hadi sasa, polisi walisema.
Mbunge wa
California Brad Sherman alikuwa miongoni mwa wale ambao walilazimika kuhamishwa
kutoka kwa DNC.
"Waandamanaji
walikua na vurugu, wakiwapulizia pilipili maafisa wa polisi na kujaribu kuingia
ndani ya jengo hilo," aliandika kwenye mtandao wa kijamii.
Unaweza pia kusoma:
Hezbollah yaonya vita vya kikanda ikiwa mashambulizi Gaza yataendelea
Mtoto mmoja huuawa kila baada ya dakika kumi Gaza
Nchi ya Amerika Kusini ambayo ina jamii kubwa zaidi ya Wapalestina nje ya Ulimwengu wa Kiarabu na Israeli
'Ninapiga simu kutoka shirika la ujasusi la Israel.Tunarusha bomu, una saa mbili kuondoka’
Vita vya Israel na Gaza: Je, uhalifu wa kivita unatekelezwa?, sheria inasemaje?
Farasi alivyoilazimisha ndege kurudi kwenye uwanja wa ndege baada ya kutoroka kwenye kibanda
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Farasi, ambaye hayupo kwenye picha hii, alitoroka wakati ndege hiyo ikisafiri umbali wa futi 30,000 (picha ya faili)
Ndege ya mizigo aina ya Boeing 747
imelazimika kugeuka, baada ya farasi kutoroka kutoka kwenye kibanda chake ndani
ya ndege na kusababisha vurugu wakati ndege hiyo ikisafiri kumbali wa futi 30,000
(9,144m) angani.
Ndege hiyo ilikuwa ikitoka New York kuelekea Ubelgiji lakiniilibidi ilazimike kurudi baada ya farasi aliyekuwemo ndani ya banda lake kwenye ndege kutoroka takriban
dakika 90 baada ya ndege hiyo kupaa.
Sauti ya udhibiti wa usafiri wa anga ilimrekodi rubani akisema:
"Tuna mnyama hai, farasi, kwenye ndege. Farasi ametoroka.""Hatuwezi kumrejesha farasi salama."
Rubani wa ndege ya Air Atlanta Icelandic 4592 aliwaambia waongozaji wa
safari ya ndege hali ilikuwa swari, lakini
farasi aliyeruka ndiye aliyekuwa na
wasiwasi.
Kisha alimuomba daktari wa mifugo kukutana na ndege hiyo mara tu
ilipotua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa John F Kennedy.
Bado haijafahamika ni kwa jinsi farasi Houdini alivyoweza kutoka ndani
ya kibanda chake na kutoroka.
Ndege hiyo ilipaa baadaye siku
hiyo hiyo na kufanikiwa kufika katika Uwanja wa Ndege wa Liege Ijumaa asubuhi,
kulingana na FlightRadar24.
Jeshi la Ulinzi la Israel limeripoti tena mashambulizi ya anga dhidi ya Hezbollah.
Chanzo cha picha, EPA
Maelezo ya picha, Israel imepeleka makombora kwenye mpaka wake na Lebanon
Katika ujumbe wa X ( zamani ikiitwa Twitter),
jeshi la Israel limesema lilishambulia maeneo kadhaa katika ardhi ya Lebanon
Jumatano.
Limesema miongoni mwa maeneo hayo ni pamoja na ghala la silaha, miundombinu ya
kijeshi, vituo vya uchunguzi na maeneo ambayo wanamgambo wa Hezbollah walirusha
makombora katika ardhi ya Israel.
Chanzo cha picha, X
Unaweza pia kusoma:
Hezbollah yaonya vita vya kikanda ikiwa mashambulizi Gaza yataendelea
Mtoto mmoja huuawa kila baada ya dakika kumi Gaza
Nchi ya Amerika Kusini ambayo ina jamii kubwa zaidi ya Wapalestina nje ya Ulimwengu wa Kiarabu na Israeli
'Ninapiga simu kutoka shirika la ujasusi la Israel.Tunarusha bomu, una saa mbili kuondoka’
Vita vya Israel na Gaza: Je, uhalifu wa kivita unatekelezwa?, sheria inasemaje?
Ikiwa ndio kwanza unautembelea mtandao wetu, huu ndio muhtasari wa habari kuu za dunia
Israel imeahidi itatoa
ushahidi wa kuthibitisha madai yake kuwa wanamgambo wa Hamas wana kituo chao
kikuu cha kuratibu operesheni zao katika hospitali ya Al Shifa,hospitali kubwa
zaidi Gaza.
Mpaka sasa jeshi hilo
halijatoa ushahidi madhubuti unaothibitisha kuwa chini ya majengo ya Al Shifa
kuna mahandaki ya Hamas lakini imeonesha video ambazo haziwezi kuthibitishwa
kuwa walipata silaha ndani ya hospitali hiyo. Hamas mara kwa mara imeakanusha
madai hayo.
Baaraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
limepitisha azimio linalotaka kusitishwa na kurefushwa kwa makubaliano ya
kusitisha mapigano kwa misingi ya kiutu katika Ukanda wa Gaza.
Rais wa Marekani Joe Biden
ameyataja mazungumzo yake na kiongozi wa China Xi Jinping mjini San Francisco
kama yenye tija zaidi kuwahi kufanyika kati yao.
Raia wa Madagascar leo
wanapiga kura katika uchaguzi wa rais unaokuja baada ya wiki kadhaa za
maandamano.
Hujambo na karibu kwa matangazo yetu ya mubashara leo ikiwa ni tarehe 16.11.2023