Wizara ya afya ya Palestina huko Gaza, inasema idadi ya watu waliouawa huko Gaza tangu 7 Oktoba imeongezeka hadi 5,087 - ongezeko la 436 tangu jana.
Hiyo inajumuisha watoto 2,055, wanawake 1,119, na wazee 217, wanasema zaidi ya watu 15,273 wamejeruhiwa.
Familia ya Uingereza na Israel inasema jamaa yao amefariki
Raia mwingine wa Uingereza-Israel amethibitishwa kuuawa katika mashambulizi ya Hamas dhidi ya Israel.
Yosef Guedalia, 22, alikuwa mwanajeshi katika kitengo cha kupambana na ugaidi na aliuawa wakati akikabiliana na wapiganaji wa Hamas huko Kibbutz Kfar Aza waliposhambulia tarehe 7 Oktoba.
Kaka yake Asher alisema alisaidia kuwahamisha raia waliojeruhiwa kabla ya kurejea kupambana na wapiganaji wa Hamas.
Kuna video ya Yosef akimfanyia huduma ya kwanza raia aliyejeruhiwa ambaye sasa anapata nafuu hospitalini Asheri anasema.
' Aliokoa watu dakika chache kabla hajapigwa risasi.Alifanya kwa ushujaa na dhamira, aliendelea kupigana na hakujifikiria mwenyewe au kusita ... aliingia katika uokoaji wa raia wengi iwezekanavyo kabla ya kuuawa majumbani mwao na kuua magaidi wengi kadiri alivyoweza."
'Aliokoa watu dakika chache kabla ya kupigwa risasi.Alifanya kwa ushujaa na dhamira, aliendelea kupigana na hakujifikiria mwenyewe au kusita ... aliingia katika uokoaji wa raia wengi iwezekanavyo kabla ya kuuawa majumbani mwao na kuua magaidi wengi kadiri alivyoweza."
Asheri aliendelea kusema alikuwa na uhakika kwamba kaka yake alielewa "huenda asirudi kwa mke wake na familia yake lakini huo ndio wito wake. Huyo ndiye shujaa tuliyekuwa naye kwa miaka 22".
Yusufu alikuwa karibu kusherehekea kumbukizi yake ya kwanza ya harusi.
Waingereza kumi na moja sasa wanajulikana kuuawa na Hamas.Mmoja ametekwa nyara.Takriban wanne bado hawajulikani walipo
Waziri kiongozi wa Uskoti: Familia yangu huko Gaza ina chupa sita za maji kwa watu 100
Waziri Kiongozi wa Uskoti Humza Yousaf anasema mama mkwe wake na mumewe wanaishi kwa "mateso" huku wakisalia kukwama huko Gaza.
"Zimepungua hadi chupa sita za maji safi ya kunywa katika nyumba ya watu 100 akiwemo mtoto mchanga wa miezi miwili," Yousaf aliwaambia waandishi wa habari wakati wa ziara ya Brechin.
Aliondoka ili kupokea simu yake na kusema kwamba familia haiwezi kujua kama "itafanikiwa kutoka usiku mmoja hadi mwingine," huku makombora, milio ya roketi na ndege zisizo na rubani zikiendelea usiku kucha.
Wakwe wa Yousaf walikuwa Gaza wakitembelea familia wakati uhasama ulipopamba moto.Alisema anaiomba serikali ya Uingereza kwa niaba yao kutaka kufunguliwa kwa kivuko cha Rafah na kusitishwa kwa mapigano.
Mengi zaidi kuhusu mzozo wa Israel-Gaza: