Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Mzozo wa Sudan: Rais wa zamani Al-Bashir na washirika wake wametolewa jela, huku mzozo ukipamba moto

jeshi lilithibitisha uhamisho wa Bashir mwenye umri wa miaka 79 kutoka gereza la Kober la Khartoum hadi hospitali ya kijeshi, pamoja na maafisa wake wa zamani watano

Moja kwa moja

  1. Mzozo Sudan: Ikulu ya White House yathibitisha kifo cha Mmarekani wa pili nchini Sudan

    Ikulu ya White House imesema kwamba raia wa pili wa Marekani amekufa nchini Sudan siku ya Jumanne huku kukiwa na ghasia kati ya pande zinazozozana.

    John Kirby, msemaji wa usalama wa taifa wa Ikulu ya White House, aliwaambia waandishi wa habari kwamba ghasia zimepungua sana huko na kwamba Marekani ilikuwa ikiwezesha kuondoka kwa idadi ndogo ya Wamarekani wanaotaka kuondoka Sudan.

    Wakati huo huo ndege ya nne ya Uingereza imeondoka katika mji mkuu wa Sudan, Khartoum, Downing Street imesema, na kufanya jumla ya waliohamishwa kufikia 301.

    Serikali ya Uingereza inasema jumla ya ndege nane zitaondoka Sudan ifikapo mwisho wa siku. "Msemaji rasmi wa waziri mkuu alisema: "Kuna ndege nyingine inayopakia hivi sasa.

    Majibu kutoka Khartoum yanaendelea vizuri. Ndege nne tayari zimeondoka, nyingine inapakia sasa. "Tunaita kila mtu mbele na hatuna suala na uwezo, na watu wanashughulikiwa vizuri."

    Msemaji huyo aliongeza kuwa "wengi" wa watu kwenye ndege ni raia wa Uingereza lakini wengine watakuwa raia wa washirika, alisema.

    Unaweza pia kusoma:

    • Mgogoro Sudan: Familia zinasubiri habari za wapendwa wao
    • Vita Sudan: Kwanini nchi za Afrika zinajikongoja kuondoa raia wake?
    • Mohamed Hamdan Dagalo: Mfahamu jenerali anayeongoza vikosi vya RSF dhidi ya jeshi la Suda
  2. 'Ni wanafunzi wa Nigeria pekee waliosalia hapa'

      • Author, Cecilia Macaulay
      • Nafasi, BBC News

    Raia wa Nigeria wanaonekana kuwa wanafunzi pekee wa kigeni waliobakia wamekwama nchini Sudan, mmoja ameambia BBC katika simu yake ya huzuni.

    "Ni wanafunzi wa Nigeria pekee waliosalia hapa Sudan, kila mtu ameondoka, sisi tu," mwanafunzi wa chuo kikuu, ambaye hataki kutajwa jina, alisema.

    Mataifa mengine ya Afrika kama Afrika Kusini, Kenya, Mali, Ivory Coast na Uganda ni miongoni mwa mataifa ambayo yametangaza kuwahamisha baadhi ya raia wao.

    "Inasikitisha sana," aliendelea, akiongeza kwa sauti kwamba alitarajia Nigeria ingekuja kwa ajili yake na uokoaji wa wanafunzi wenzake hivi karibuni.

    Alisema Nigeria iliendelea "kuchelewesha" kutumwa kwa mabasi ili kuwahamisha.

    Alitarajia waje Jumanne, lakini hawakuwahi kufika. Kisha aliambiwa na ubalozi kwamba mabasi yangewachukua saa 06:00 kwa saa za huko leo, lakini walikuwa hawajawachukua hadi saa 10:00.

    Aidha, Ubalozi huo ulisema ni mabasi matano pekee ndiyo yatawasili, lakini hiyo haitoshi kuwasafirisha wanafunzi wote, alisema.

    Watu katika hosteli yake ya chuo kikuu pia walikuwa na upungufu wa chakula, alisema, na walikuwa wakijaribu tu kuishi: "Tuna njaa hapa."

    Unaweza pia kusoma:

    • Mgogoro Sudan: Familia zinasubiri habari za wapendwa wao
    • Vita Sudan: Kwanini nchi za Afrika zinajikongoja kuondoa raia wake?
    • Mohamed Hamdan Dagalo: Mfahamu jenerali anayeongoza vikosi vya RSF dhidi ya jeshi la Suda
  3. Mzozo wa Ukraine: Zelensky azungumza na Rais Xi wa China kwa mara ya kwanza tangu vita

    Volodymr Zelensky wa Ukraine anasema alikuwa na "muda mrefu na wa maana" wa kuzungumza kwa simu na Rais Xi Jinping wa China, mawasiliano yao ya kwanza tangu vita vya Urusi kuanza.

    Alisema kwenye Twitter anaamini simu hiyo, pamoja na uteuzi wa balozi mjini Beijing, "utatoa msukumo mkubwa kwa maendeleo ya uhusiano wetu wa nchi mbili".

    China ilithibitisha mawasiliano hayo, na kuongeza kuwa "daima ilisimama upande wa amani". Hadi sasa, Beijing imetaka kuonyesha msimamo wa kutoegemea upande wowote juu ya uvamizi wa Urusi.

    Lakini haijawahi kulaani uvamizi huo na mwezi uliopita Rais Xi alifanya ziara ya kiserikali ya siku mbili nchini Urusi.

    Alimtaja Rais Vladimir Putin kama "rafiki yake kipenzi", alipendekeza mpango usio wazi wa amani wenye mambo 12 na kusisitiza kuwa China inasimama upande wa kulia wa historia. Walakini, hakujitolea kuipatia Urusi silaha.

    Rais Zelensky alimwalika kiongozi huyo wa China kutembelea Kyiv kwa mazungumzo, akibainisha kwamba walikuwa na mawasiliano kabla ya vita lakini hakuna chochote kilichoendelea tangu vita ilipoanza Februari 2022.

    CCTV ya China ilimnukuu Rais Xi akisema kwamba China "haitatazama moto kutoka upande mwingine, wala kuongeza mafuta kwenye moto, achilia mbali kuchukua fursa ya matatizo kujinufaisha".

  4. Mzozo wa Sudan: Mshukiwa wa uhalifu wa kivita 'atoroka' gerezani huku machafuko yakiendelea

    Mwanasiasa wa zamani wa Sudan anayesakwa kwa tuhuma za uhalifu dhidi ya ubinadamu amesema kuwa yeye na maafisa wengine wa zamani wako nje ya gereza - kufuatia ripoti kuenea kuhusu kutoroka kwao gerezani.

    Ahmed Haroun alikuwa miongoni mwa wale wanaoshikiliwa katika gereza la Kober katika mji mkuu Khartoum wanaokabiliwa na mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).Usitishaji mapigano kati ya vikundi vya kijeshi nchini humo kwa kiasi kikubwa unaonekana kama umesimama.Lakini kuna mashaka juu ya kujitolea kwa pande zote mbili kuhakikisha kunapatikana amani ya kudumu.

    Mgogoro huo - ulioanza tarehe 15 Aprili - ulitokana na mzozo mkali wa madaraka kati ya viongozi wa jeshi la Sudan na kundi pinzani la wanamgambo, Rapid Support Forces (RSF).Ripoti ziliibuka mapema wiki hii katika gereza la Kober - ambapo Ahmed Haroun alikuwa akitumikia kifungo pamoja na Omar al-Bashir, rais wa zamani wa Sudan.

    Siku ya Jumanne, Haroun alithibitisha katika taarifa iliyopeperushwa kwenye televisheni ya Tayba ya Sudan kwamba yeye na wafuasi wengine wa Bashir waliokuwa chini yake walitoroka jela - lakini akasema atakuwa tayari kufika mbele ya mahakama wakati wowote atakapotakiwa.

    Katika ujumbe wa sauti uliosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Haroun alidai kundi hilo lilisaidiwa kutoroka na walinzi wa gereza na vikosi vya jeshi.

    Tulifanya uamuzi huu kujilinda dhidi ya ukosefu wa usalama, maji, chakula na matibabu, pamoja na vifo vya wafungwa wengi huko Kober," Haroun aliambia al-Sudani, gazeti la kila siku lenye uhusiano na Bashir.

    Haroun alikuwa mmoja wa watendaji waliokuwa mstari wa mbele wakati wa utawala wa serikali ya Sudan akitajwa kuwa na mkono kwenye vita viwili vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa muda mrefu na ambavyo bado havijatatuliwa - huko Darfur (toka mwaka 2003) na Kordofan Kusini (tangu mwaka 2011).

  5. Mzozo Sudan: Jeshi la Sudan laanzisha msako kwa wafungwa waliotoroka gerezani

    Jeshi la Sudan na polisi wanasema wameanzisha operesheni ya kuwarudisha wafungwa waliotoroka akiwemo mshukiwa wa uhalifu wa kivita Ahmed Haroun wakati wa mapigano kati ya makundi hasimu ya kijeshi.

    Wizara ya mambo ya ndani ilisema katika taarifa yake kwamba Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF), ambacho kinapambana na jeshi, kilivunja magereza matano na kuachilia idadi isiyojulikana ya wafungwa.

    Wizara hiyo ilisema uvamizi wa Gereza la Kober katika mji mkuu wa Khartoum ulisababisha kuuawa kwa askari wawili wa magereza, na kwamba RSF iliwaachilia wafungwa wote.

    Kutoroka gerezani kulifanyika kati ya 21-24 Aprili, kulingana na wizara.

    Msemaji wa jeshi la Sudan aliiambia Sky News Arabia hii ni "tishio kubwa la usalama". Msemaji huyo alisema jeshi hilo linashirikiana na polisi kuwarejesha wafungwa magerezani.

    Alikanusha jeshi kuhusika katika utorokaji huo wa wafungwa akisema jeshi "halina usimamizi wowote juu ya magereza".

  6. Mzozo wa Sudan: Rais wa zamani Al-Bashir na washirika wake wametolewa jela, huku mzozo ukipamba moto

      • Author, BBC Monitoring
      • Nafasi, The world through its media

    Jeshi la Sudan na jeshi la wanamgambo walipigana viungani mwa mji mkuu siku ya Jumatano, na kudhoofisha usitishaji wa amani katika mzozo wa siku 11 ambao makundi ya kiraia yanahofia kuwa yanaweza kufufua ushawishi wa kiongozi aliyeondolewa madarakani Omar al-Bashir na wafuasi wake.

    Kuchochea wasiwasi huo, jeshi lilithibitisha uhamisho wa Bashir mwenye umri wa miaka 79 kutoka gereza la Kober la Khartoum hadi hospitali ya kijeshi, pamoja na maafisa wake wa zamani watano, kabla ya mapigano kuanza Aprili 15.

    Na afisa kutoka chama tawala cha zamani cha National Congress Party (NCP) ambaye alikimbia kutoka gerezani aliliambia gazeti la Al-Sudani kwamba

    "watajisalimisha kwa mamlaka ya mahakama hali itakaporuhusu". "Tulifanya uamuzi wa kujilinda kutokana na ukosefu wa usalama, maji, chakula na matibabu, pamoja na vifo vya wafungwa wengi huko Kober [gerezani]," Ahmed Haroun alisema.

    Haroun anasakwa kwa tuhuma za uhalifu wa kivita, jambo ambalo awali amelikanusha.

    Zinahusiana na madai ya uchochezi wa ghasia dhidi ya raia huko Darfur. Alikamatwa mwaka 2019 kufuatia mapinduzi dhidi ya Bashir.

    Magereza yameripotiwa kulengwa huku mapigano kati ya makundi hasimu ya kijeshi yakiendelea kwa wiki ya pili.

    Katika mji mkuu wa Darfur Kusini wa Nyala, wafungwa wasiopungua 750 waliripotiwa kutoroka kufuatia maandamano na ghasia za wafungwa, huku mamia ya wengine wakitoroka kutoka magereza mengine ya Khartoum na Omdurman.

  7. Mzozo wa Ukraine: Ndege tatu za Urusi zazuiwa juu ya anga la Baltic

    Ndege tatu za kijeshi zilizokuwa zikipaa bila kutoa ishara zimezuiwa kuendelea na safari katika anga ya kimataifa juu ya Bahari ya Baltic, wamesema maafisa wa Ujerumani.

    Majeshi ya Ujerumani na Uingereza yamezitambua ndege hizo kama- ndege mbili za mapigano za Su-27 na moja ya Il-20.

    Kikosi cha Marekani cha German Air Force kilituma ujumbe wa picha za wahusika katika tukio hilo katika Twitter:

    Mahambulio ya Ukraine: Mengi zaidi

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
  8. Guaifenesin: WHO yatoa tahadhari kuhusu dawa ya kikohozi ya maji inayotengenezwa

    Shirika la Afya duniani (WHO) limesema kwamba shehena ya dawa ya kikohozi yenye sumu ya India - imepatikana katika visiwa vya Marshall na Micronesia.

    WHO ilisema kuwa sampuli zilizofanyiwa vipimovya Guaifenesin TG syrup, iliyotengenezwa na kiwanda cha madawa cha Punjab QP Pharmachem Ltd, zinaonyesha"kiwango kisichokubalika cha diethylene glycol na ethylene glycol".

    Viungo vyote hivyo viwili ni sumu kwa binadamu na vinaweza kusababisha kifo iwapo mwanadamu atainywa.

    Taarifa ya WHO haikuelezea wazi iwapo kuna yeyote aliyeuguakutokana na matumizi ya dawa hiyo.

    Tahadhari ya hivi karibuni inakuja miezi kadhaa baada ya WHO kuhusisha dawa nyingine za maji za kikohozi zilizotengenezwa nchini India ambazo zilisababisha vifo vya watoto katika nchi za Gambia na Uzbekistan.

    Sudhir Pathak, ambaye ni Mkurugenzi mkuu wa QP Pharmachem, ameiambia BBC kwamba kampuni ilikuwa imepeleka shehena ya chupa 18,346 katika mataifa ya Cambodia baada ya kupewa ruhusu ya kufanya hivyo. Alisema kuwa hakujua iwapo bidhaa hiyo ilikuwa imefika katika Visiwa vya Marshall na Micronesia.

  9. Afrika Kusini sasa yasasema haina mipango ya kujiondoa kwenye mkataba wa ICC kwa ajili ya Putin

    Ofisi ya rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaposa ametoa taarifa kwamba nchi yake haina mipango ya kujiondoa kwenye Mkataba wa Roma kuhusu kuanzishwa na mchakato wa mahakama ya kimataifa ya jinai (ICC) kinyume na kauli aliyozitoa mwenyewe rais Jumanne.

    Mwezi Agosti kikao cha ZRICS kinatarajiwa kufanyika nchini Afrika Kusini, na kwa hali ilivyo sasa rais wa Urusi anapaswa kukaribishwa.

    Afrika Kusini inaitambua kisheria mahakama ya The Hague, ambayo ilitoa waranti ya kumkamata Vradimir Putin, na atatakiwa rasmi kutekeleza waranti (hatahivyo, hakuna vikwazo vinavyotolewa kwa wasiotekeleza waranti).

    Ofisi ya rais inadai kwamba chama tawala cha African National Congress (ANC) kilikosea katika mazungumzo . "Ofisi ya rais inataka kuweka wazi kwamba, Afrika Kusini bado imesalia kuwa mwanachama wa Sheria ya Roma... Hii inafuatia kutokamilika kwa kauli katika mazungumzo kwa vyombo vya habari yaliyofanywa na chama cha ANC," ilieleza taarifa iliyotolewa usiku.

  10. Tangaraju Suppiah: Singapore yatekeleza hukumu ya kifo dhidi ya mwanaume kwa kuuza bangi

    Singapore imetekeleza hukumu ya kifo dhidi ya mwanaume mmoja kwa kufaya ulanguzi na usambazaji wa bangi licha ya ombi la hurumakutoka kwa familia, wanaharakati na Umoja wa Mataifa.

    Mwanaume huyo kwa jina Tangaraju Suppiah, mwenye umri wa miaka 46, amenyongwa katika Gereza laChangi alfajiri Jumatano, imesema familia yake.

    Wanaharakati walisema kuwa alikuwa amepatikana na hatia kutokana na ushahidi dhaifu na hakupata usaidizi wa kutosha wa kisheria wakati aliposhitakiwa na waendesha mashitaka.

    Maafisa walisema kuwa alipata usaidizi unaofaa na wakawakosoa wanaharakati kwa kuzihoji mahakama.

    Singapore ina moja ya sheria kali zaidi duniani dhidi ya madawa ya kulevya, ambazo ilidai ni muhimu kwa ajili ya kuzuia uhalifu unaosababishwa na madawa ya kulevya.

    Mwaka jana nchi hiyo ilitekeleza hukumu 11 za vifo kuhusiana na madawa ya kulevya.

    Jumatano, familia ya Tangaraju Suppiah ilikuwa imekusanyika katika gereza hilo lililopo mashariki mwa mji mkuu

  11. Kupanda kwa joto kwa kasi baharini kwawatia tumbo joto wanasayansi

    Kupanda kwa joto kwa kasi isiyo ya kawaida kwenye mabahari ya dunia kunawafanya wanasayansi kuhofia kwamba hili linaweza kuharakisha kuongezeka kwa joto ulimwenguni.

    Mwezi Aprili, maji yaliyoko karibu na sakafu ya bahari yalifikia viwango vya juu zaidi vya joto kuwahi kurekodiwa: haijawahi kamwe kushuhudiwa katika historia ya dunia kwamba bahari inachemka kiasi kikubwa na kwa haraka vile.

    Wanasayansi bado hawajafahamu ni kwanini hili linatokea, lakini kupanda kwa viwango vya joto kwenye mabahari, kunachangiwa na mabadiliko ya tabia nchi kwa ujumla, na wanaonya kuwa hii inaweza kuviweka viwango vya joto dunia katika kiwango kipya kufikia mwishoni mwa mwaka ujao.

    Kulingana na wataalamu, katika kipindi cha miezi ijayo, pia kutakuwa na athari mbaya katika kipindi cha El Niño, mkiwemo kubadilika kwa viwango vya joto la utando wa juu wa maji ya bahari katika maeneo ya Ikweta ya Bahari ya Pacific - mabadiliko ambayo pia yatasababisha athari kwa hali ya hewa.

  12. Mzozo wa Sudan: Mshukiwa wa uhalifu wa vita alifunguliwa katika ghasia

    Mwanasiasa wa zamani wa Sudan anayesakwa kwa uhalifu dhidi ya binadamu amesema kuwa yeye na maafisa wengine kwa sasa hawako gerezani tena.

    Ahmad Harun alikuwa ni miongoni mwa wale waliokuwa wanashikiliwa katika gereza la Kober lililopo katika mji mkuu Khartoum ambao wanakabiliwa na mashitaka katika mahakama ya kimataifa ya jinai (ICC).

    Makundi mawili ya kijeshi yanayohasimiana nchini Sudan yanaonekana kuheshimu makubaliano ya usitishaji mapigano.

    Lakini kuna wasi wasi juu ya iwapo pande hizo mbili zitajitolea kuhakikisha kunakuwepo na amani ya kudumu katika taifa hilo.

    Katika tukio jingine, ndege ya pili ya uokozi inayowaondoa rai awa Uingereza nchini Sudan imetua katika nchi ya Cyprus .

    Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa ambaye bado yupo nchini Sudan,Volker Perthes, amesema kuwa mud awa usitishaji wa mapigano was aa 72 unaonekana kuheshimiwa katika baadhi ya meneo ya Sudan.

    Lakini milipuko na risasi ziliripotiwa katika mji mkuu Khartoum na katika mji jirani wa Omdurman.

    Unaweza pia kusoma:

    • Mgogoro Sudan: Familia zinasubiri habari za wapendwa wao
    • Vita Sudan: Kwanini nchi za Afrika zinajikongoja kuondoa raia wake?
    • Mohamed Hamdan Dagalo: Mfahamu jenerali anayeongoza vikosi vya RSF dhidi ya jeshi la Suda
  13. iSpace: Chombo cha kijapani cha kutua mwezini huenda kilianguka

    Kampuni ya Kijapani inayotarajia kufanya safari nadra ya kibinafsi ya kutua mwezini inasema kuna uwezekano kwamba chombo chake cha mwezi kilianguka angani.

    Mawasiliano na Hakuto-R yalipotea muda mfupi kabla ya kutua saa 16:40 GMT Jumanne.

    Chombo hicho kilirushwa na roketi ya SpaceX mwezi Disemba, na ilichukua muda wa miezi mitano kufika inakoenda.

    "Hatujathibitisha mawasiliano na mpangaji ndege," Mkurugenzi Mtendaji wa iSpace Takeshi Hakamada alisema kama dakika 25 baada ya kutua kama ilivyopangwa.

    "Tunapaswa kukiri kwamba hatukuweza kukamilisha azma yetu ya kutua mwezini," aliongeza.

    Wahandisi wanachunguza kilichotokea.

    Gazeti la iSpace lenye makao yake Tokyo lilikuwa na matumaini kwamba mpangaji huyo angetoa rova ​​ya uchunguzi, pamoja na roboti yenye ukubwa wa mpira wa tenisi iliyotengenezwa na kampuni hiyo ya kutengeneza vifaa vya kuchezea.

    Bw Hakamada baadaye alisema kuwa licha ya kutotarajia kukamilisha misheni hiyo, kampuni hiyo "imekamilisha kikamilifu umuhimu wa misheni hii, baada ya kupata data nyingi na uzoefu kwa kuweza kufikia awamu ya kutua".

    Roketi ya M1 ilionekana ikikaribia kutua baada ya kuja karibu kama futi 295 (89 m) kutoka kwenye anga ya mwezi, picha ya uhuishaji wa moja kwa moja ilionyesha.

    Chombo hicho kilikuwa na urefu wa zaidi ya mita mbili na uzito wa kilo 340, ndogo kiasi na ilishikana kulingana na viwango vya chombo cha anga za juu.

    Ilikuwa kwenye mesheni ya saa moja ya kutua kutoka kwenye obiti yake, karibu kilomita 100 juu ya anga, ambapo ilikuwa ikitembea kwa karibu kilo mita 6,000 kwa saa.

  14. Taliban wamuua kiongozi wa IS 'mpangaji mkuu' wa shambulio la uwanja wa ndege wa Kabul

    Kiongozi wa kikundi cha Islamic State ambaye anadhaniwa kuwa ndiye aliyepanda shambulio baya la bomu la mwaka 2021 katika uwanja wa ndege wa Kabul ameuawa na utawala wa AfghanstanTaliban, maafisa wa Marekani wanasema .

    Ulipuaji mabomu wa mwezi Agosti , 2021 uliwauwaraia 170 na wanajeshi 13 wa Marekani wakati watu walipokuwa wakijaribu kutorokanchiwakati Taliban waliponyakua udhibiti wa nchi.

    Kiongozi huyo wa IS aliuawa wiki kadhaa zilizopita, lakini ilichukua muda kuthibitisha kifo chake, maafisa wa Marekani wamekiambia kituo cha habari washirika na BBC, CBS.

    Jina lake bado halijatangazwa.

    Maafisa wa Marekani walisema kuwa walikuwa wametambua kupitia ujasusi wao na ufuatiliajiwa kanda kwamba kiongozi huyo amefariki , ingawa hawakutoa maelezo zaidi kuhusu ni vipi walifahamu kuwa alikuwa ndiye muhusika wa mashambulio ya mabomu.

    "Wataalamu katika serikali wana Imani kubwa kwamba mtu huyu…alikuwa kweli ndiye muhusika mkuu," afisa wa ngazi ya juu wa Marekani aliiambia CBS.

    Kulingana na Makala katika gazeti la New York Times, marekani ilifahamu kuhusu kifo cha kiongozi huyo wa IS mapema mwezi April. Haijawa wazi iwapo alilengwa na Taliban au iwapo aliuawa wakati wa mapigano yanayoendelea baina ya IS na Taliban, limeripoti gazeti hilo.

    Unaweza pia kusoma:

    • Shambulio la uwanja wa ndege wa Kabul: Je! Tunajua nini?
  15. Hujambo na karibu tena katika matangazo yetu ya moja ya leo tarehe 26.04.2023