Rais Xi wa China kukutana na Putin mjini Moscow wiki ijayo
Rais wa China Xi Jinping atasafiri hadi Moscow wiki ijayo kufanya mazungumzo na Rais wa Urusi Vladimir Putin, maafisa wanasema.
Moja kwa moja
Rais Samia amkumbuka mtangulizi wake John Pombe Magufuli
Chanzo cha picha, Ikulu ya Rais Tanzania
Maelezo ya picha, Rais Samia
Huku Watanzania
wakimuenzi rais wa awamu ya tano marehemu John Pombe Magufuli miaka miwili
tangu alipoaga dunia, Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa miongoni mwao.
Katika chapisho
lake la mtandao wa Twitter , rais Samia alimuenzi mtangulizi wake akisema: ‘Leo
ni miaka miwili tangu tuondokewe na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati
Dkt. John Pombe Magufuli.Mwenyezi Mungu aendelee kumpa pumziko jema na aendelee kuwatia nguvu
wanafamilia wote. Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kumuenzi kwa kuendeleza
mazuri aliyoyaanzisha’.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe
Upofu na majeraha viliripotiwa baada ya Marekani kutaka kurejeshwa kwa dawa ya macho
Chanzo cha picha, Getty Images
Maafisa wa afya wa Marekani wanasema kuwa dawa ya macho kuna
uwezekano kuwa imemuua mtu mmoja na kuwajeruhi vibaya wengine kadhaa kutokana
na kushindwa kwake kukabili bakteria ambao wanastahili kufa baada ya kutumia
dawa hiyo.
Vituo vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (CDC) vimegundua
wagonjwa 68 katika majimbo 16 walio na aina adimu ya Pseudomonas aeruginosa.
Aina hiyo ya bakteria haijawahi kupatikana nchini Marekani
kabla ya mlipuko huu wa hivi karibuni.
Mbali na kifo kimoja, wagonjwa wanane wamepoteza uwezo wa
kuona, na wanne wametolewa macho kwa upasuaji.
Wagonjwa wengi waliogunduliwa na maambukizi waliripoti
kutumia matone ya dawa hiyo ya macho, kulingana na CDC.
Chapa kumi tofauti za dawa hiyo zilitambuliwa hapo awali
kama zinaweza kuhusishwa na mlipuko huo, CDC ilisema.
Dawa ya macho ya matone ambayo yanatengenezwa India na
kuletwa Marekani chini ya chapa mbili baadaye zilitolewa kwenye rafu za
manunuzi mnamo Januari na Februari.
Mnamo Januari, CDC ilionya watu kuacha kutumia Machozi
Bandia ya EzriCare na Machozi Bandia ya Delsam Pharma kwasababu inasemekana pia
hilo linachangia katika hali kama hizo.
Rais Xi wa China kukutana na Putin mjini Moscow wiki ijayo
Chanzo cha picha, Reuters
Rais wa China Xi Jinping atasafiri hadi Moscow wiki ijayo
kufanya mazungumzo na Rais wa Urusi Vladimir Putin, maafisa wanasema.
Kremlin ilisema watajadili "ushirikiano wa kina na
ushirikiano wa kimkakati".
Ziara hiyo inajiri huku Beijing, mshirika wa Urusi,
ikitoa mapendekezo ya kumaliza vita nchini Ukraine, ambapo nchi za Magharibi zilionyesha
kutoshabikia mapokezo hayo.
Nchi za Magharibi zimeionya Beijing dhidi ya kuipatia
Moscow silaha.
Hii itakuwa ziara ya kwanza ya rais Xi nchini Urusi tangu
wanajeshi wa Urusi kuivamia Ukraine.
Anatarajiwa kula chakula cha mchana na Bw Putin siku ya
Jumatatu na kufuatiwa na mazungumzo siku ya Jumanne.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje alisema China
itashikilia "msimamo wenye lengo na haki" kuhusu vita vya Ukraine na
"kuchukua jukumu la kuhakikisha tija kukuza mazungumzo ya amani".
Ukweli ni kwamba ziara ya kiongozi wa China inaashiria
uungaji mkono mkubwa wa Beijing kwa Moscow.
Hakuna linaloshangaza kuhusu hilo: Putin na Xi wana maoni
sawa kuhusu ulimwengu, wote wanakumbatia wazo la ulimwengu wenye nchi zinazoonekana
kuwa sawa.
Mwaka jana watu hao wawili walitangaza ushirikiano wao
hauna kikomo. Hiyo si kweli kabisa.
Mwaka jana watu hao wawili walitangaza ushirikiano wao
hauna kikomo.
Hiyo si kweli kabisa.
Hadi kufikia sasa, China haijaipatia Urusi misaada hatari
ili kuisaidia kushinda vita vya Ukraine, ingawa Marekani inadai kuwa China
inafikiria kufanya hivyo.
Uranium ya Libya: Mapipa yaliyokosekana yapatikana - vikosi vya mashariki
Chanzo cha picha, LNA
Vikosi vya kijeshi mashariki mwa Libya vinasema kuwa
wamepata takriban tani mbili na nusu za madini ya urani yaani uranium ambayo
yaliripotiwa kutoweka na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki.
Mapipa kumi yenye madini hayo yalipatikana karibu na
mpaka na Chad, alisema mkuu wa kitengo cha vyombo vya habari vya vikosi hivyo.
IAEA ilisema "inafanya kazi kikamilifu ili
kuthibitisha" ripoti za vyombo vya habari.
Shirika hilo lilipiga yamgambo baada ya ziara ya wakaguzi
wake mapema wiki hii kwenye tovuti ambayo haijatajwa
Eneo hilo halikuwa katika eneo linalodhibitiwa na
serikali.
Uranium ni kipengele kinachotokea kawaida ambacho
kinaweza kuwa na matumizi yanayohusiana na nyuklia mara tu kitakaposafishwa, au
kurutubishwa.
Uranium ambayo ilitoweka haiwezi kufanywa kuwa silaha ya
nyuklia katika hali yake ya sasa, lakini inaweza kutumika kama malighafi ya
mpango wa silaha za nyuklia, wataalam waliiambia BBC.
Mnamo Desemba 2003, chini ya mtawala wa wakati huo wa
kijeshi Kanali Muammar Gaddafi, Libya iliachana hadharani na silaha za nyuklia,
kibayolojia na kemikali.
Patrick Vieira: Crystal Palace yamfuta kazi meneja baada ya kushindwa mechi 12
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Nahodha wa zamani wa Arsenal Patrick Vieira alichukua nafasi ya Roy Hodgson huko Crystal Palace mnamo Julai 2021.
Crystal Palace imemfuta kazi meneja Patrick Vieira baada ya kucheza mechi 12 na kutoka bila kushinda yoyote.
Palace
hawajashinda mechi yoyote mwaka wa 2023 na walichapwa 1-0 na Brighton kwenye
Ligi ya Premia Jumatano, kikiwa ni kipigo chao cha tatu mfululizo.
Wako nafasi
ya 12 kwenye jedwali lakini wako pointi tatu pekee juu ya Bournemouth walio
katika nafasi ya 18, ambao wana mchezo unaowasubiri.
"Ni kwa
masikitiko makubwa kwamba uamuzi huu mgumu umefanywa," mwenyekiti Steve
Parish alisema.
"Hatimaye,
matokeo ya miezi ya hivi karibuni yametuweka katika hali mbaya ya ligi na
tuliona mabadiliko ni muhimu ili kutupa nafasi nzuri zaidi ya kubaki na hadhi
ya Ligi Kuu.
"Mfaransa
Vieira, 46, aliteuliwa kabla ya kuanza kwa msimu wa 2021-22 na kuiongoza Eagles
kumaliza katika nafasi ya 12, na kujipatia sifa kwa mtindo wa kushambulia.
Hata hivyo,
msimu huu wamefunga mabao 21 pekee katika mechi 27 - ni Wolves, Everton na
Southampton walio mkiani mwa jedwali.
Kabla ya
kushindwa na Brighton, Palace walikuwa wamecheza mechi tatu mfululizo bila
shuti lililolenga lango.
Hakuna timu ya Premier League iliyoshinda
pointi chache zaidi mwaka wa 2023 kuliko Palace.
Wanachama
watatu wa makocha wa Vieira - Osian Roberts, Kristian Wilson na Said Aigoun -
pia wameiacha klabu hiyo na mchakato wa kumteua meneja mpya unaendelea.
Alama tano
pekee zinatenganisha vilabu tisa vilivyo chini ya Premier League kuelekea miezi
ya mwisho ya msimu.
Palace
itasafiri kwa viongozi Arsenal, klabu ya zamani ya Vieira, Jumapili (14:00
GMT).
Mechi zao 10
za mwisho msimu huu zitawakutanisha na wapinzani wao wote wanane walioshuka
daraja.
Kwa picha : Shughuli ya mazishi ya mchezaji soka Christian Atsu yaanza Accra Ghana
Maelezo ya picha, Jeneza la Mchezaji soka wa Ghana Christian Atsu, likiwasili kwa ajili ya shughuli ya mazishi mjini Accra Ghana
Mchezaji soka wa Ghana Christian Atsu, ambaye
alifariki baada ya tetemeko la ardhi kuikumba Uturuki anazikwa leo Ijumaa katika nchi yake ya asili Ghana.
Atsu alipatikana akiwa
amefariki baada ya tetemeko la ardhi kuangusha nyumba ya gorofa ambamo alikuwa
anaishikusini mwa Uturuki . Alikuwa akiichezea klabu ya soka ya Hatayspor.
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Atsu alifariki katika tetemeko la adrhi lililoikumba Uturuki
Shuguli ya mazishi yake ambayo yamesaidiwa na taifa la Ghana inafanyika katika mji mkuu Accra.
Maelfu ya waombolezaji wamefika katika eneo la mazishi kutoa heshima zao za mwisho kwa Christian Atsu, katika mazishi yanayofanyika kwa utamaduni wa Ghana.
Hizi ni baadhi ya picha za mazishi ya Christian Atsu, zilizochukuliwa na mwandishi wa BBC wa Ghana Thomas Naadi:
Unaweza pia kusoma:
Christian Atsu wa Ghana alikuwa na 'moyo wa kipekee'
Christian Atsu anaamini Ghana watashinda kombe la AFCON
Burna Boy kutumbuiza katika fainali za UEFA
Msanii wa Nigeria na mshindi wa Tuzo za Grammy Burna Boy atatumbuiza katika sherehe za uzinduzi
wa fainali za kuwania Kombe la Ligi ya
championi ya UEFA mjini Istanbul, Turkey.
Nyota huyo wa Nigeria ataleta nguvu na ladha ya
muziki wa Solo wenye mapigo ya afrobeat kabla ya kuanza kuanza kwa mechi za fainali ya UEFA , imesema taarifa
"Dunia haiko tayari kwa kile tulichoiandalia," Burna Boy alinukuliwa akisema, kabla
ya onyesho lake katika Uwanja wa Atatürk
Olympic.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe
Mahujaji wa Uganda watahadharishwa dhidi ya kunywa ’maji matakatifu’
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Waumini wanaochukua maji wanadai kuwa yana nguvu za uponyaji wa kiroho
Mahujaji wa Kikatoliki wanaotembelea eneo la
mashahidi wa Uganda la Namugongo wametahadharishwa dhidi ya kunywa maji katika
kile kinachoitwakisima kitakatifu .
Maafisa wa kanisa hilo wanasema maji hayo yanaweza
kutumiwa kwa malengo mengine ya kiroho kama vile kufanya ishara ya msalaba ,
lakini hayafai kunywa.
Katibu mkuu
wa Baraza kuu la mkutano wa maaskofuwa Uganda, John kauta, Alhamisi alisema
kuwa ingawa waumini waliochukua maji wanadai kutibiwa kiroho, wataalamu wa afya
wamewashauri viongozi wa kanisa kwamba maji hayo sio masafi na sio salama..
“Maji katika Namugongo yamechujwa, lakini bado sio salama
kwa kunywa. Hii ni kwasababu pia yanapita kutoka katika maeneo mengi. Watu wanaweza
kuyachukua na kuyagusa wanapofanya ishara ya msalaba, lakini sio kuyanywa,” Bw Kauta aliuambia mtandao wa gazeti llinalodhibitiwa
na serikali la New Vision.
Bw Kauta alisema
kwamba siku zijazo kanisa litaweka mabomba mengi katika kisima hicho kwa ajili
ya kuwasaidia watu kuyafikia kwa urahisi zaidi kutokana na kwamba idadi ya
wanaoyataka ni wengi.
Chanzo cha picha, UGANDA MARTYRS CATHOLIC SHRINE/FACEBOOK
Maelezo ya picha, Maelfu kwa maelfu ya watu hufika Namugongo kila mwaka kutoka maeneo mbali mbali duniani kuhudhuria sherehe za Siku ya Mashahidi wa Uganda mwezi Juni
Mahujani wameanza kuwasili katika eneo la makaburi ya mashahidi wa Namugongo kwa ajili ya sherehe za Siku ya Mashahidi inayoadhimishwa mwezi Juni.
Tukio hilo la kila mwaka linahusu mashahidi 22 wa kikatoliki na 23 wa kianglikani waliuawa kwa ajili ya Imani yao kutokana na amri yaKabaka Mwanga wa Buganda baina yam waka 1885 na 1887.
Marekani: Video ya kifo cha mwanaume mwenye asili ya Kenya inaonyesha polisi wakimfanyia ukatili – familia
Chanzo cha picha, BEN CRUMP LAW
Maelezo ya picha, Familia ya ya Irvo Otieno (kulia) ilisema alikuwa na matatizo ya kiakilialipofariki katika mahabusu
Mama wa
mwanaume mweusi mwenye umri wa miaka 28 ambaye alifariki akiwa katika mahabusu ya
polisi anasema video ya dakika 12 inayoonyesha tukio la mauaji yake inayo "
sumbua na kutia kiwewe" na kisa hicho ni "ukatili".
Polisi saba wa cheo cha sheriff wa Virginia wameshitakiwa kwa mauaji ya daraja cha pili kuhusiana na kifo cha mwanaume huyo anayefahamika kama Irvo Otieno.
Waendesha mashitaka Alhamisi pia
walitangaza mashitaka zaidi ya mauaji ya daraja la pili dhidi ya wafanyakazi watatu
wa hospitali.
Wakili Crump alisema, katika
video Otieno alionekana "akizuiliwa kwa ukatili mkubwa, huku akishindiliwa
chini kwa goti kwenye shingo lake , akiwekewa uzito wa watu saba mwilini mwake,
huku uso wake ukiangalia chini, akiwa amefungwa pingu."
Bw Crump amefananisha kisa cha Bw Otieno na
tukio la George Floyd, Mmarekani mwingine mweusi aliyeuliwa kikatili na polisi.
Bw Otieno alifariki tarehe 6 Machi wakati
alipokuwa akihamishwa kutoka gereza kupelekwa katika kituo cha afya cha watu wenye
matatizo ya akili.
Ripoti ya awali inaonyesha kuwa uchunguzi
wa kimatibabu ulionyesha kuwa alifariki kwa - kukosa hewa, walisema waendeshamashitaka.
Polisi saba wa Kaunti ya Henrico wameshutumiwa
na waendeshamashitaka kwa kumuua Bw Otieno kwa kumkosesha hewa ya kupumua, wakati walipokuwa wakimhamisha.
Waendeshamashitaka wanasema ushahidi zaidi
uliwawezesha pia kuwashitaki wafanyakazi wa hospitali katika Hospitali ya -Central
State Hospital, ambako Bw Otieno alikuwa akihamishiwa.
Video ya tukio ilinaswa na kamera za
usalama, na ilitazamwa Alhamisi na wakili maarufu wa haki za binadamu Ben Crump pamoja na familia ya Bw
Otieno.
Mama yake Otieno, Caroline Ouko, na Bw Crump kwa pamoja
walisema kuwa alikuwa anasumbuliwa na matatizo ya kiakili , na amekuwa akipata
matibabu ya kiakili, lakini hakuweza kuendelea kumeza dawa hizo akiwa gerezani.
Familia ya Otieno ambayo
ilitoka Kenya na kuhamia Marekani alipokuwa na umri wa miaka minne. Bw Otieno alikuwa
na ndoto ya kuwa mwanamuziki na mwanamichezo, walisema, na alikuwa akiandika na
kurekodi muziki wakat iwa muda wake wa ziada
Uteuzi wa Manaibu Waziri wazua mjadala Kenya
Maelezo kuhusu taarifa
Author, Caro Robi
Nafasi, BBC Swahili
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, Rais wa Kenya William Ruto
Rais wa Kenya William Ruto mnamo Alhamisi 16.03.2023 amewateua Mawaziri Wasaidizi (CAS) 50 ambao wamepewa kusimamia wizara 22.
Kwenye orodha hiyo iliyotangazwa kupitia taarifa ya Mkuu wa Utumishi wa Umma Felix Koskei, idadi kubwa ya wateuzi hao ni wanasiasa wa Muungano wa Chama tawala Kenya Kwanza walioshindwa kwenye uchaguzi mkuu uliopita.
Miongoni mwao ni aliyekuwa Gavana wa Kaunti ya Nairobi Evans Kidero, Seneta mteule wa zamani Millicent Omanga, aliyekuwa mbunge wa Starehe Margaret Wanjiru na mbunge wa zamani wa Rarieda Mhandisi Nicholas Gumbo miongoni mwa wengine.
Uteuzi huo wa mawaziri wasaidizi 50 wa wizara 22 walioidhinshwa na Tume ya Utumishi wa Umma,umepokelewa kwa hisia mseto na Wakenya.
Wengi katika mitandao ya kijamii wamehoji utashi wa Rais Ruto wa kutimiza ahadi yake wakati wa kampeini mwaka jana ambapo aliahidi kuwa serikali yake itajumuisha kwa kiasi kikubwa wananchi wa tabaka la chini aliowaita 'Mama Mboga na Boda Boda'.
Serikali inakosolewa pia kwa kufeli kupunguza mzigo wa kuajiri maafisa wengi serikalini wanaolipwa fedha nyingi za walipa ushuru,wakati ambapo uchumi wa Kenya unasuasua na Wakenya wengi wakilalamikia ugumu wa maisha.
Aidha darubini inamulikwa kwa kutowapa fursa zaidi vijana katika serikali na teuzi kutokuwa na sura ya kitaifa. Baadhi ya wizara zimetengewa zaidi ya mawaziri wasaidizi wawili katika uteuzi huo wa Alhamisi.
Katika serikali iliyopita ya Rais Uhuru Kenyatta, ambayo Rais wa sasa William Ruto aliikosoa vikali kwa teuzi nyingi alizozitaja mzigo kwa 'Mahustler',kulikuwa na mawaziri 23, hivyo basi uteuzi huu wa sasa ni karibu mara mbili ya ilivyokuwa awali.
Katika ukurasa wake wa Twitter,Naibu wa Rais Rigathi Gachagua ametetea uteuzi huo akisema wizara zina masuala mengi ambayo yanahitaji kushughulikiwa na wanaleta nguvu mpya kupiga jeki utendakazi na uwezo wa serikali.
Walioteuliwa kuchukua wadhifa huo wa mawaziri wasaidizi ambao haujaanishwa katika Katiba ya Kenya, watapigwa msasa na bunge kabla ya kuanza rasmi kutekeleza majukumu yao.
Mtaalamu wa afya ya akili:Felician Kabuga hataki kesi yake iendelee kwasababu anaumwa
Chanzo cha picha, SCREENGRAB IRMCT LIVE EVENT
Maelezo ya picha, Profesa Henry Kennedy makiwa katika Mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai ICC, Alhamisi, akitoa ushahidi kuhusu afya ya akili ya Bw Kabuga
Mmoja wa wataalam wa afya ya akili waliotoa ripoti
kuhusu afya ya mtuhumiwa maarufu wa mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994,Felician
Kabuga, amesema kuwa afya yake haimruhusu
"kuhusdhuria kesi dhidi yake mahakamani" – akihojiwa na waendesha mashitaka na mawakili wake.
Kabuga, ambaye
alifuatilia kesi yake katika gereza la Mahakama kwa njia ya video, hakupewa muda wa kuzungumzia kuhusu maelezo yaliyotolewa na mtaalamu wa afya ya akili kumuhusu.
Chanzo cha picha, SCREENGRAB IRMCT LIVE EVENT
Maelezo ya picha, Félicien Kabuga ambaye anashitakiwa kwa mauaji ya kimbari ya Rwanda ya 1994, akifuatilia kesi yake akiwa gerezani
Kesi ya Bw Kabuga ambaye anashutumiwa kama mmoja wa wahusika wakuu waliodhamini mauaji ya kimbari ya Rwanda, imekuwa ikiendelea katika mahakama ya kimataifa ya jinai ICC, mjini The Heague Uholanzi.
Katika kikao cha mahakama Alhamisi wiki hii, jopo la waendesha mashitaka lilifuatilia kesi hiyo kwa njia ya mtandao kutoka Arusha -Tanzania, huku mawakili wa Bw Kabuga wakiwa The Heague -Uholanzi.
Awali Bw Kabuga alikana mashitaka yote kuhusu mauaji ya kimbari ya Rwanda anayoshitakiwa.
Unaweza pia kusoma:
Mauaji ya Rwanda: Jinsi Felicien Kabuga alivyojificha kwa miaka 26
Félicien Kabuga: Mshukiwa mkuu wa mauaji ya kimbari Rwanda akamatwa
Félicien Kabuga: 'Huo wote ni uongo, sikumuua Mtutsi yeyote'
Kamanda wa Ukraine 'aliyetoa siri' kwa waandishi wa habari ashushwa cheo
Chanzo cha picha, Reuters
Kamanda
wa kikosi cha jeshi la Ukraine Anatoly al
maarufu "Kupol", ambaye aliliambia gazeti la Marekani la Washington Post kuhusu kushindwa vibaya kwa vikosi vya Ukraine, alishushwa cheo, limeripoti gazeti la Ukraine "Ukrainian Pravda" likimnukuu afisa wa vikosi vya uvamizi wa anga nchini humo.
Taarifa ya mwanajeshi huyo
ilichapishwa baada ya kufanya mazungumzo na kundi la waandishi wa habari wa
Marekani ambao walichapisha taarifa hiyo tarehe 13 Machi, kuhusiana na hali katika eneo la Bakhmut kufuatia mashambulizi ya Warusi.
Alidai
kuwa kushindwa kwa jeshi la Ukraine katika mapigano ya Bakhmutkulipelekea kupungua pakubwa kwa idadi ya
wanajeshi wa Ukraine, jambo ambalo awali liliangaliwa kama faida ya Ukraine ikilinganishwa
na Urusi. Matokeo yake , baadhi ya maafisa walianza kuhoji utayari wa Ukraine
wa kukabiliana na vita siku zijazo.
Miongoni mwa mambo mengine
, kamanda hiyo wa Ukraine alisema kuwa takriban wanajeshi 100 kati ya 500
katika kikosi chake waliuawa na wengine 400 wakajeruhiwa katika mashambulio ya Bakhmut.
Mwakilishi rasmi wa kikosi
cha anga cha Ukraine, Valentin Shevchenko, katika mahojiano na gazeti la Ukraine -Ukrayinska Pravda, alisema
taarifa zilizotolewa na mwanajeshi huyo zilizidi
makadirio na sio za kuaminika na akasema kwamba maafisa wanachunguza zaidi
kuhusu taarifa alizozitoa.
Vita vya Ukraine:Poland kutuma ndege nne za kivita Ukraine 'katika siku zijazo'
Chanzo cha picha, EPA
Poland itatuma ndege nne za
maoigano za aina ya Mig jetza
enzi ya Usovieti nchini Ukraine – na kuwanchi ya kwanza ya Nato kutuma ndege zaketangu Urusi uanze uvamizi wa Urusi nchini Ukraine .
Rais wa Poland Andrzej
Duda alisema kwamba ndege hizo zitapelekwa katika siku zijazo, na nyingine
zitapelekwa baadaye.
Ingawa msada huo unapokelewa vyema kwa maana kwamba utaboresha utendaji wa kikosi cha ulinzi wa anga cha Ukraine,
jeti hizi za ziada hazitarajii kuleta mabadiliko yoyote katika vita.
Naibu spika wa bunge la Ukraine Olena Kondratyuk amesema kuwa anatumaini
nchi zaidi zitafuata mfano wa Poland.
Nchi nyingine za Nato zinaangalia uwezekano wa kutuma ndege za
enzi ya Usovieti, ambazo ndizo marubani
wa Ukraine wamefunzwa kuzitumia .
Awali Ukraine iliyaomba mataifa ya Magharibi kuipatia ndege za kisasa za aina ya jeti kama vile F-16.
Uingereza inawapatia mafunzo marubani wa Ukraine kuhusu
uendeshwaji wa ndege zenye viwango vya NATO.Lakini kwasabababu ya mafunzo ya kipindi
kirefu, imeonya kuwa kupeleka jeti za Magharibi nchini Ukraine utakuwa ni
mpango wa baadaye.
Vita vya Ukraine: Mengi zaidi
YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
Afya: Idadi ya wanaume wanaofunga uzazi kuongeza – madaktari
Chanzo cha picha, Getty Images
Idadi ya wanawaume
wanaotumia njia ya kufunga uzazi ya kudumu (vasectomy) inatarajiwa kuongezeka
zaidi, kuliko inavyoripotiwa kwa sasa, wanasema madaktari wa Uingereza waliofanya
utafiti kuhusu suala hilo.Madaktari hao wanasema baada ya kufanyiwa
upasuaji wa kufunga uzazi, wanaume wanaweza kuhisi maumivu kidogo , lakini
wanasema ni nadra kwa wanaume waliofunga uzazi kwa njia hiyo kupata madhara makubwa
ya kiafya.
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Upasuaji wa kufunga uzazi kwa njia ya vasectomy, huchukua dakika 15 pekee
Kundi la madaktari hao lilitoa matokeo ya utafiti wake katika kongamano la matibabu lililomalizika Alhamisi Milan nchini Italia, baada yakuwafanyia utafiti wanaume 94,000 ambao walifungwa uzazi kwa njia ya vasectomy.
Upasuaji wa kufunga uzazi kwa njia ya vasectomy, ambapo mwanaume hudungwa sindano ya ganzi, huchukua dakika 15 pekee.
Kwa ujumla takwimu zinaonyesha kuwa wanaume wengi bado
hawajitolei kufanyiwa upasuaji wa vasektomi kama njia ya kufanya uzazi wa mpango, zaidi
kutokana na imani zinazozingira njia hii.
Ufungaji wa kizazi kwa wanaume ni nini?
Njia ya kufunga uzazi kwa wanaume ni njia ya uzazi wa mpango ambayo hufanywa kwa njia ya upasuaji kukata au kufunga mirija inayosafirisha mbegu za uzazi za mwanaume, ili kuzuia mwanamke asipate mimba.
Upasuaji mara nyingi hufanywa kwa muda wa dakika takriban 15, mgonjwa huwa macho lakini huwa hapati maumivu yeyote.
Njia hii inafanya kazi ya kuzuia mimba kwa silimia 95.
Njia ya kufunga uzazi kwa wanaume haiathiri nguvu za kiume au uwezo katika tendo au kulifurahia tendo.Mwanaume ataweza hayo yote,isipokuwa hataweza kumpa mwanamke ujauzito.
Njia hii haizuii mwanaume dhidi ya maradhi ya zinaa, kama mipira ya kiume ambayo inaelezwa kuwa njia ya kuaminika kwa asilimia 98 ikiwa itatumika vyema.
Unaweza pia kusoma:
''Mwanamume afunguka kuhusu hatua yake ya kufunga njia ya uzazi''
Wanaume wengi Kenya wanakubali kufunga mirija ya mbegu za uzazi-Vasektom
Hujambo na karibu kwa matangazo yetu ya moja kwa moja leo Ijumaa tarehe 17.03.2023