Mwanamuziki D'Banj akamatwa kwa kashfa ya ufisadi Nigeria

Chanzo cha picha, D'BANJ/INSTAGRAM
Tume Huru ya Ufisadi na Makosa Mengine nchini Nigeria (ICPC) imethibitisha kwa BBC idhaa ya Pidgin kumshikilia mwanamuziki wa Nigeria Daniel Oyebanjo maarufu kama D'Banj.
Taarifa ya ICPC ilisema inamshikilia mwimbaji kwa uchunguzi wa ulaghai unaohusishwa na Mpango wa N-Power, mabilioni ya pesa ya kuwezesha vijana Nigeria.
N-Power ni mpango ambao Rais Muhammadu Buhari alianzisha tarehe 8 Juni, 2016, kushughulikia masuala ya ukosefu wa ajira kwa vijana na uwezeshaji, na kusaidia kuongeza maendeleo ya kijamii.
Katika taarifa ilitolewa na kaminshna wa ICPC, Azuka Ogugua, tume ilieleza chanzo cha kuzuiliwa kwa D'banj.
"Takriban watu 10 wamealikwa na ICPC katika miezi michache iliyopita kuhusiana na ulaghai wa N-Power, na wamepewa dhamana ya kiutawala baada ya kuzuiliwa kwao. Mialiko kadhaa kwa Bw Oladipo Daniel Oyebanjo, kufika mbele ya timu ya wachunguzi ilipuuzwa na kutoheshimiwa.
“Bw Oyebanjo (D'banj) alijisalimisha na kuzuiliwa katika Makao Makuu ya ICPC mnamo Jumanne, 6 Desemba 2022, na kwa sasa anasaidia wapelelezi kubaini mazingira ya madai ya ulaghai ya walalamishi.











