Achraf Hakimi, mchezaji aliyezaliwa Madrid, kaiondoa Uhispania kwenye Kombe la Dunia katika ushindi wa kihistoria wa Morocco
Achraf Hakimi, mchezaji aliyezaliwa Madrid, ameweza kuiondoa Uhispania kwenye Kombe la Dunia, nchi aliyozaliwa na kuipa ushindi wa kihistoria Morocco.
Yeye na wachezaji wenzake wakiinama mbele ya mashabiki ambao wamekuwa wazuri usiku kucha. Walishangilia kila teke. Kelele za wakati wote ni kubwa kama za mkwaju huo wa ushindi. Afrika itakuwa na timu katika nane bora.
Haya ni matokeo ya kwanza ya mshtuko wa raundi ya mtoano. Morocco wameiondoa Uhispania.
Walifanya iwe vigumu sana kwa Wahispania kuwachambua wakati wa dakika 120 na kisha wakashikilia ujasiri wao katika mikwaju ya penalti.
Morocco, timu pekee ya Kiafrika iliyosalia kwenye kinyang'anyiro hicho, imetinga hatua ya robo fainali.
Wakati huohuo, Morocco iliishangaza Ubelgiji na kuishinda Canada baada ya sare ya ufunguzi na Croatia, na kuongoza kundi lao na mabingwa wa 2010 Uhispania.
Baadaye leo, Ureno itamenyana na Uswizi katika mchezo wa fainali ya hatua ya 16 bora ya Qatar 2022, huku mshindi wa mechi hiyo akicheza na mshindi wa mchezo huu katika raundi inayofuata ambae ni Morocco.