Charlene Ruto: Mjadala watanda kenya kuhusu ufadhili wa mikutano ya mwana huyo wa Rais
Yeye ni mtoto wa pili wa Rais William Ruto, na anajiita Binti wa Kwanza wa Kenya, lakini watumiaji wa mitandao ya kijamii wanauliza kwa nini Charlene Ruto anaonekana kukutana na mawaziri wengi wa serikali na kusafari nje.
Miezi kadhaa tangu babake achaguliwe kuwa rais, vyombo vya habari vya humu nchini vinaripoti kuwa Bi Ruto amekutana na maafisa kadhaa wa kaunti kote nchini Kenya pamoja na mawaziri nje ya nchi.
Wasiwasi kama huo ulizuka wakati Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump alipochaguliwa kwa mara ya kwanza na binti yake Ivanka alihudhuria mikutano na baba yake kama mshauri asiye rasmi. Bw Trump baadaye alimteua Ivanka katika jukumu rasmi la serikali.
Mnamo Alhamisi, Charlene Ruto alisema kwenye Twitter kuwa amekutana na waziri wa vijana wa Morocco, Mohammed Mehdi, kwa "mazungumzo na kubadilishana mawazo ambayo yatasaidia sana katika kuunda miradi ya maendeleo ya vijana kwa mataifa yote mawili".
Baadhi ya Wakenya sasa wanauliza, ni nani anayefadhili mikutano yote hii, na je ni mikutano rasmi ?