Jeshi la Ukraine lasema limedungua zaidi ya ndege 300 za Iran zisizo na rubani

Chanzo cha picha, Office of the President of Ukraine
Tangu Septemba 13, wakati ndege zisizo na rubani za Shahed-136 za kamikaze za Iran zilipodunguliwa kwa mara ya kwanza juu ya Ukraine, vikosi vya Ukraine vimezidungua zaidi ya ndege 300 kama hizo, Yury Ignat, msemaji wa kamandi ya Jeshi la Wanahewa la Ukraine, alisema katika kikao fupi siku ya Ijumaa.
Amebainisha kuwa katika siku za hivi karibuni, Urusi imekuwa na uwezekano mdogo wa kutumia ndege zisizo na rubani za Iran.
Haijulikani ni ndege ngapi zisizo na rubani za Shahed-136 ambazo Urusi ilipokea,” Ignat alisema Urusi iliagiza 2,400 kati yao, lakini haijulikani ikiwa wanazo nyingi na haijulikani ikiwa wana uwezo wa kuzizalisha kwa kiasi ambacho Urusi inataka.
Kwa sababu, pengine, kwa kiasi fulani wamepunguza ukubwa wa mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Irani.
Mamlaka za Urusi zimekana madai kwamba zinanunua ndege zisizo na rubani za Kamikaze za Iran ili kushambulia Ukraine.
Hata hivyo, hivi karibuni mtaalamu wa masuala ya kijeshi aliichapisha moja kwa moja kwenye TV ya Urusi, akifikiri kwamba watazamaji hawawezi kumsikia.
Chini ya hali ya uhasama, BBC haiwezi kuthibitisha ukweli wa taarifa za wawakilishi wa vikosi vya kijeshi vya pande zinazopigana.












