Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Julius Malema: Kiongozi wa upinzani Afrika Kusini aonya kuhusu maasi yanayokaribia kutokea
Bw Malema ameonya kutokea kwa maasi sawa na mapinduzi yaliyoshuhudiwa katika mataifa ya Kiarabu nchini humo.
Moja kwa moja
Ukraine yalaani Urusi kwa kuweka ujumbe wa 'kukejeli' mauaji ya wafungwa
Ukraine imeitaja Urusi kama "nchi ya kigaidi" baada ya ubalozi wa Moscow nchini Uingereza kuweka ujumbe kwenye Twitter kwamba wanajeshi wa Kikosi cha Azov cha Ukraine walistahili "kifo cha kufedhehesha" kwa kunyongwa.
Twitter ya ubalozi huo ilikuja baada ya zaidi ya wafungwa 50 wa vita wa Ukraine (POWs) waliokuwa wakishikiliwa na Urusi kuuawa - wanajeshi wa Azov wanaripotiwa kuwa miongoni mwao.
Walikufa katika shambulio dhidi ya gereza la Olenivka huko Ukraine inayoshikiliwa na Urusi.
Ukraine na Urusi zinalaumiana kuhusu shambulizi lililoua wafungwa.
Twitter haikuondoa ujumbe huo hiyo kutoka kwa Ubalozi wa Urusi nchini Uingereza, lakini ilisema ilikiuka sheria za Twitter za kupinga chuki.
Kando na serikali ya Ukraine, watumiaji wengine Twitter walionyesha kukasirishwa na tweet hiyo.
Meli ya Syria iliyokuwa na nafaka za Ukrane yazuiliwa Lebanon kwa saa 72
Vyombo kadhaa vya habari nchini Lebanon vinaripoti kwamba ofisi ya mwendesha mashtaka wa Lebanon amezuilia meli ya Syria ambayo, kulingana na habari kutoka Kyiv, ilikuwa ikisafirisha ngano iliyoibiwa kutoka Ukraine.
Tovuti ya habari ya LBC ilichapisha ujumbe ambayo ofisi ya mwendesha mashitaka ilitumia kuzuilia meli hiyo katika bandari ya Tripoli na kuwasilisha uchunguzi kwa huduma maalum.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Lebanon, Ubalozi wa Ukraine nchini Lebanon ulipata kibali cha kisheria cha kuzuilia meli hiyo, ambayo imekuwa katika bandari ya Beirut tangu Julai 28, kwa saa 72.
Kwa upande wake, ubalozi wa Urusi nchini Lebanon uliambia vyombo vya habari vya ndani kuwa haukuwa na habari kuhusu meli hiyo, ukizitaja tuhuma za Ukraine kuwa "uongo usio na msingi."
Siku moja kabla, ubalozi wa Ukraine nchini Lebanon uliripoti kwamba mahakama Ukraine ilitoa hati ya kukamatwa kwa meli ya Laodikea yenye bendera ya Syria na mizigo iliyokuwemo, iliyozuiliwa katika bandari ya Beirut.
Maelezo zaidi:
Julius Malema: Kiongozi wa upinzani nchini Afrika Kusini aonya kuhusu maasi yanayokaribia
Mwanasiasa wa upinzani mwenye utata nchini Afrika Kusini, Julius Malema, ameonya kuhusu maasi yanayokaribia kuwa sawa na mapinduzi ya nchi za Kiarabu maarufu "Arab Spring" ambayo yatalenga wazungu na "wasomi weusi".
"Mapinduzi yatakapokuja... walengwa wa kwanza watakuwa wazungu," Bw Malema aliambia kipindi cha Hardtalk cha BBC.
Alidai "kuingilia kati" ili kuimarisha ubora wa maisha ili kuepuka machafuko.
Mbunge huyo anayejulikana kwa misimamo mikali, ameshtakiwa mara mbili kwa matamshi ya chuki.
Pia amekabiliwa na mashtaka ya ulaghai na ufisadi, ambayo yalitupiliwa mbali baadaye. Bw Malema alisema yalichochewa kisiasa.
Mapinduzi ya Kiarabu yalikuwa mfululizo wa maandamano ya kuunga mkono demokrasia ambayo yalianza mwishoni mwa 2010 nchini Tunisia, ambapo rais alipinduliwa, na kuenea katika nchi nyingine kadhaa katika eneo hilo.
Katika mahojiano ya BBC, Bw Malema aliwashutumu matajiri weusi kwa kujitoa kimasomaso.
"Vurugu ambazo zitatokea Afrika Kusini ni kwa sababu watu wasomi wanatoweka na maskini wanazidi kuwa maskini," alimwambia mwandishi wa BBC Stephen Sakur.
"Kwa hiyo kutakuwa na kitu ambacho kinaonekana kama mapinduzi ya Kiarabu. Hilo, tumehakikishiwa."
Soma:
Wanariadha wa Afrika Mashariki watawala mbio za Marathon katika michezo ya Jumuiya ya Madola
Waafrika Mashariki walitawala mbio za marathon za wanaume katika Michezo ya Jumuiya ya Madola, Birmingham.
Mwanariadha wa Victor Kiplangat aliishindia Uganda nishani ya dhahabu yake ya kwanza katika mbio za Marathon.
Kiplagat alitumia muda wa kasi zaidi wa 2:10:55 na kujinyakulia dhahabu mjini Birmingham muda mchache uliopita.
Alphonse Simbu wa Tanzania alimaliza wa pili huku Vincent Kiplangat akiishindia Uganda medali ya dhahabu ya marathon ya kwanza kabisa kwa ushindi wa saa 2:10:55 naye Michael Githae akaipatia Kenya medali ya kwanza kwa kutwaa medali ya shaba kukamilisha kufua kwa jukwaa la Afrika Mashariki mjini Birmingham.
Hii ndio nafasi nzuri zaidi kwa Uganda katika hatua hii baada ya Solomon Mutai kunyakua Silver katika michezo ya 2018 huko Gold Coast.
Stephen Kiprotich alishinda mataji ya Olimpiki ya London 2012 na Ubingwa wa Dunia wa 2013 lakini hakuna raia wa Uganda aliyewahi kushinda marathoni ya medali ya dhahabu katika Michezo ya Jumuiya ya Madola kabla ya Jumamosi.
Ni medali ya kwanza kwa Uganda katika michezo inayoendelea, na medali namba 56 kwa ujumla (dhahabu ya 17) katika michezo iliyoshindaniwa na makoloni ya zamani ya Uingereza.
Lulu ya Afrika itahisi kuwa ni medali ya kwanza kati ya nyingi ambazo timu ya wanachama wapatao 72 wanaweza kupata huko Birmingham.
"Hatufungi mtandao", Waziri wa Kenya anasema
Serikali ya Kenya imeondoa hofu ya uwezekano wa kufungwa kwa mtandao kabla ya uchaguzi wa mwezi ujao.
Waziri wa habari nchini homo Joe Mucheru amepuuzilia mbali pendekezo la Tume ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa(NCIC) la kusimamisha shughuli za Facebook nchini kutokana na matamshi ya chuki.
Katika taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa twitter, waziri huyo alitilia shaka mfumo wa kisheria uliotumiwa na tume hiyo.
Siku ya Ijumaa NCIC ilisema kuwa imeiandikia Meta ikitaka majibu kuhusu madai ya udhibiti dhaifu wa maudhui kwenye Facebook kabla ya uchaguzi wa mwezi ujao.
Iliamuru Facebook kuboresha udhibiti kwenye Fecebii ndani ya siku saba au ikabiliwe na tishio la kufungiwa.
Mashirika ya utetezi ya Global Witness na Foxglove yalisema katika ripoti yao iliyochapishwa Alhamisi kwamba Meta iliidhinisha matangazo ambayo yanakuza matamshi ya chuki na uchochezi kabla ya uchaguzi.
Facebook inasema wameimarisha udhibiti kwenye majukwaa yake ambayo yatarahisisha kutambua na kuondoa maudhui ambayo yanaweza kusababisha vurugu zinazohusiana na uchaguzi.
Maelezo zaidi:
- Uchaguzi Kenya 2022:Yote unayopaswa kujua
- Uchaguzi Kenya 2022 : Kwa nini wakulima wanapenda matamanio makubwa ya William Ruto
- Uchaguzi wa Kenya 2022:Mfumko wa bei za bidhaa umeathiri vipi maisha?
- Uchaguzi Kenya 2022: Uchaguzi wa Kenya una maana gani kwa Tanzania na Afrika Mashariki?
Watu 2 wauawa DRC huku Maandamano dhidi ya Umoja wa Mataifa yakizidi kuongezeka
Watu wawili wameuawa huko Butembo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakati mamia walipokuwa wakifanya tafrija ya mazishi ya raia waliouawa wiki iliyopita wakati wa maandamano ya kupinga Umoja wa Mataifa.
Ripoti zinasema polisi walitumia gesi ya kutoa machozi kutawanya umati mkubwa wa watu waliokuwa barabarani na majeneza ya watu tisa waliouawa.
Makabiliano ya hivi punde kati ya waandamanaji na vikosi vya usalama vya DRC yalitokea wakati mamia ya watu walikusanyika kwa ajili ya mazishi ya raia tisa waliouawa katika maandamano ya ghasia katika mji wa Butembo.
Majeneza ya waliofariki, baadhi yakiwa yamebandikwa bendera ya nchi hiyo, yalikuwa yamepeperushwa barabarani huku watu wakiimba nyimbo na kauli mbiu za kupinga Umoja wa Mataifa.
Waliapa kuendelea na maandamano ambayo yamekuwa yakiendelea tangu mapema wiki jana.
Lakini polisi waliingilia kati, na kutawanya umati wa watu na kuchukua majeneza.
Mazishi ya marehemu yalitarajiwa kufanywa Jumamosi lakini haya sasa yameahirishwa kufuatia vurugu za hivi punde.
Miji ya Mashariki mwa DR Congo imekuwa ikifanya maandamano makubwa yaliyotokana na kile wanachosema ni kushindwa kwa walinda amani wa Umoja wa Mataifa kuwalinda dhidi ya makumi ya makundi yenye silaha yanayofanya kazi katika eneo hilo.
Uchaguzi wa Kenya 2022: Sonko ajiunga na mrengo wa siasa wa Wiliam Ruto
Gavana wa zamani wa gavana wa Nairobi Mike Sonko amejiunga na Muungano wa Kwanza unaoongozwa na Naibu Rais wa Kenya William Ruto miezi mitatu tu baada ya kujiunga na Wiper Democratic Movement kama mwanachama wa maisha.
Bw Sonko, ambaye amekuwa akikabiliana na kesi kadhaamahakamani akitaka kupewa kibali cha kuwania kiti cha ugavana Mombasa, alikutana na Naibu Rais William Ruto Jumamosi asubuhi katika makazi yake huko Karen.
Mara baada ya mkutano huo Bw. Ruto aliandika katika Twitter yake rasmi: ''Tunamkaribisha Mike Sonko kwa Kenya Kwanza timu ya ushindi.''
Bw Sonko alikuwa ametangaza kuwa atamuunga mkono mgombeaji wa chama cha United Democratic Alliance (UDA) Hassan Omar kwa kinyang'anyiro cha ugavana wa Mombosa.
Alisema iwapo maombi yake yatakataliwa tena na mgombea mwenza Ali Mbogo asipate kibali cha kugombea, ataelekeza uungwaji mkono wake kwa Bw Omar.
Shakira: Mwendesha mashtaka ataka afungwe miaka minane kwa kukukwepa kulipa kodi
Shakira anaweza kufungwa jela miaka minane na faini ya zaidi ya euro milioni 23 iwapo atapatikana na hatia katika kesi ya ulaghai wa kodi.
Mwimbaji huyo wa Colombia anashutumiwa kwa kushindwa kulipa ushuru wa €14.5m (£12m) kati ya 2012 na 2014.
Mapema wiki hii Shakira alikataa ofa ya kumaliza na kufunga kesi hiyo. Tarehe ya kesi bado haijawekwa
Taarifa kutoka kwa wawakilishi wa Shakira ilisema "ana uhakika kamili wa kutokuwa na hatia" na anaona kesi hiyo kama "ukiukaji wa haki zake".
Nyota huyo alishtakiwa kwa kukwepa kulipa ushuru mwaka wa 2018. Waendesha mashtaka walisema alikuwa akiishi Uhispania kati ya 2012 na 2014 huku akiorodhesha makazi yake rasmi mahali pengine.
Watu wanaokaa zaidi ya miezi sita nchini wanachukuliwa kuwa wakazi kulingana na kanuni ya utozaji ushuru. Lakini Shakira anasema hakuwa akiishi Uhispania wakati huo.
Hati kutoka kwa waendesha mashtaka iliyoonekana na Reuters inadai Shakira alinunua nyumba huko Barcelona mnamo 2012, ambayo ilikuja kuwa nyumba ya familia yake na mshirika wake wa wakati huo, mchezaji soka wa klabu ya Barcelona Gerard Piqué.
Soma:
Saa ya Hitler yauzwa kwa dola milioni 1.1 katika mnada wenye utata
Saa inayosemekana kuwa ya kiongozi wa Nazi Adolf Hitler imeuzwa kwa $1.1m (£900,000) katika mnada nchini Marekani.
Saa ya Huber, iliyouzwa kwa mzabuni asiyejulikana, inaonyesha swastika na ina herufi za AH zilizochorwa juu yake.
Viongozi wa Kiyahudi walilaani hatua hiyo kabla ya kuuzwa kwa saa hiyo katika Mnada wa Kihistoria wa Alexander huko Maryland.
Hata hivyo jumba la mnada - ambalo limeuza kumbukumbu za Wanazi siku za nyuma - liliambia vyombo vya habari vya Ujerumani lengo lake lilikuwa kuhifadhi historia.
Adolf Hitler aliongoza Ujerumani ya Nazi kati ya 1933 na 1945, akipanga mauaji ya kimfumo ya watu kama milioni 11 - milioni sita kati yao waliuawa kwa sababu walikuwa Wayahudi.
Orodha ya bidhaa za saa hiyo inasema kuwa huenda ilitolewa kama zawadi ya siku ya kuzaliwa kwa kiongozi huyo wa kifashisti mnamo 1933, mwaka ambao alikuwa Chansela wa Ujerumani.
Tathmini ya nyumba ya mnada inasema kuwa saa hiyo ilichukuliwa kama ukumbusho wakati wanajeshi 30 wa Ufaransa walipovamia Berghof, eneo la mafungo la mlima la Hitler mnamo Mei, 1945.
Wakati huo inafikiriwa kuwa saa iliuzwa tena na kupitishwa kwa vizazi kadhaa hadi sasa.
Makala mengine katika mnada huo yalijumuisha vazi la mke wa Hitler, Eva Braun, picha za otomatiki za maafisa wa Nazi na kitambaa cha njano cha Star of David kilichoandikwa neno "Yuda", ambalo ni la Kijerumani kwa ajili ya Wayahudi. Wakati wa mauaji ya kimbari, Wanazi waliwalazimisha Wayahudi kuvaa vitambulisho vya manjano kama vitambaa au beji, kwa nia ya kuwatenga na kuwanyanyasa
Barua ya wazi iliyotiwa saini na viongozi 34 wa Kiyahudi ilielezea mauzo hayo kama "ya kuchukiza" na kutoa wito kwa bidhaa za Nazi kuondolewa kwenye mnada.
Vita vya Ukraine: Umoja wa Mataifa na Msalaba Mwekundu wanapaswa kuchunguza vifo vya wafungwa, inasema Ukraine
Ukraine imetoa wito kwa Umoja wa Mataifa na Shirika la Msalaba Mwekundu kuruhusiwa kuchunguza vifo vya zaidi ya wafungwa 50 wa Kivita wa Ukraine (POWs) katika shambulio dhidi ya maeneo yanayokaliwa kwa mabavu.
Shirika la Msalaba Mwekundu lilisema linatafuta namn aya kufika katika gereza hilo ili kusaidia kuwahamisha na kuwatibu waliojeruhiwa.
Ukraine na Urusi zimeshutumiana kuhusu shambulio dhidi ya kushambulia kambi hiyo.
Picha za video za Urusi ambazo hazijathibitishwa za matokeo zinaonyesha msongamano wa vitanda vilivyoharibika na miili iliyoungua vibaya.
Kilitokea katika kambi ya magereza huko Olenivka, ambayo inadhibitiwa na Jamhuri ya Watu wa Donetsk inayoungwa mkono na Urusi, bado hakijajulikana.
Ukraine inasema eneo hilo lililengwa na Urusi katika juhudi za kuharibu ushahidi wa mateso na mauaji.
Rais Volodymyr Zelensky alielezea tukio hilo kama "uhalifu wa kivita uliopangwa na Urusi."
Karibu katika matangazo ya moja kwa moja.