Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Russia yadai meli yake bado inaelea huku Ukraine ikisema inazama baada kuishambulia

Jeshi la Ukraine linadai kuwa meli hiyo ya Urusi ilianza kuzama baada ya kupigwa na makombora ya Neptune.

Moja kwa moja

  1. Urusi yaishutumu Ukraine kwa shambulio la mpakani

    Wachunguzi wa Urusi wanasema kuwa Ukraine ilifanya mashambulizi ya anga kwenye eneo la makazi nchini Urusi mapema leo.

    Maafisa wanasema helikopta mbili za kijeshi zinazoruka chini zikiwa na silaha nzito zilishambulia mji wa Klimovo, na kuwajeruhi watu saba akiwemo mtoto na kuharibu nyumba sita.

    Ripoti za shambulio hilo - ambazo hazijathibitishwa kwa njia huru - zilikuja baada ya Moscow kutangaza kuwa itashambulia kwa mabomu maeneo ya Kyiv na maeneo mengine ya Ukraine ikiwa vikosi vya Ukraine vitaendelea kushambulia eneo lake.

    Kulingana na gavana wa eneo la Belgorod la Urusi, kijiji cha Spodaryushino kilipigwa makombora na Ukraine, na kusababisha uhamishaji wa watu .

    Akiandika kwenye Telegram, Vyacheslav Gladkov alisema hakuna mtu aliyejeruhiwa na hakuna majengo yaliyoharibiwa.

    Madai hayo yanajiri baada ya maafisa wa Urusi kuishutumu Ukraine kwa kufanya mashambulizi ya anga kwenye eneo jingine la makazi ya watu katika mji wa Klimovo katika eneo la Bryansk.

    Wiki mbili zilizopita, bohari ya mafuta pia ilichomwa moto huko Belgorod - Urusi ilidai Ukraine ilihusika na hii pia.

    BBC haiwezi kuthibitisha ni nani aliyehusika na matukio haya, lakini Ukraine ilikanusha kugonga bohari ya mafuta ya Belgorod mapema mwezi huu.

    Unaweza pia kusoma

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
    • SILAHA:Mzozo wa Ukraine:Makombora ya stinger na silaha nyingine kali zinazotumiwa Ukraine
  2. Wanigeria wadai haki kufuatia kifo cha mwimbaji wa nyimbo za injili Osinachi Nwachukwu

    Zaidi ya watu 9,000 wametia saini ombi la mtandaoni la kudai haki kwa niaba ya mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili Osinachi Nwachukwu na watu wengine wanaodaiwa kuwa waathiriwa wa unyanyasaji wa nyumbani nchini Nigeria.

    Pia wanatoa wito kwa sheria ya kushughulikia unyanyasaji wa nyumbani.

    Kifo cha Nwachukwu kimezua ghadhabu miongoni mwa Wanigeria na kuibua mjadala kuhusu ndoa, unyanyasaji wa nyumbani na talaka.

    Hapo awali, mwimbaji huyo alisemekana kufariki kwa saratani ya koo, lakini marafiki na familia walidai kwamba alikuwa mwathirika wa unyanyasaji wa nyumbani.

    Mume wake, Peter Nwachukwu anazuiliwa na polisi lakini hajashtakiwa kwa kosa lolote. Uchunguzi bado unaendelea.

    Waziri wa Masuala ya Wanawake nchini Nigeria Pauline Tallen ameahidi kumtafutia haki Nwachukwu.

    Hakuna sheria ya kitaifa dhidi ya unyanyasaji wa nyumbani nchini Nigeria.

    Sheria ya Marufuku ya Unyanyasaji dhidi ya Watu iliyopitishwa mwaka wa 2015 inatumika mji mkuu wa Abuja pekee.

    Maelezo zaidi:

    • Mama yake Osinachi azungumza kwa mara ya kwanza
    • Kifo cha Osinachi Nwachukwu:Binti wa muhubiri wa kanisa la Dunamis azungumza kuhusu kifo cha Osinachi
  3. Moskva:Urusi yasema Meli yake ya kivita bado inaelea huku Ukraine ikidai meli hiyo inazama

    Wizara ya ulinzi ya Urusi imetoa taarifa hivi punde kuhusu Moskva. Inasema:

    "Moto kwenye meli ya ya kivita ya Moskva umedhibitiwa. Hakuna miale ya moto inayoonekana. Vifaa vya risasi havilipuki tena.

    "Meli ya Moskva bado inaelea. Ghala kuu la silaha za makombora halijaharibiwa.

    "Wahudumu wa meli hiyo walihamishwa hadi kwenye meli za msafara wa Black Sea zilizo karibu. Hatua zinachukuliwa ili kuivuta meli hiyo bandarini.

    "Sababu za moto huo zinachunguzwa kwa sasa ."

    Jeshi la Ukraine ladai kwamba Moskva ilianza kuzama

    Muda mfupi uliopita tulisikia kutoka kwa jeshi la Urusi, ambao wanasema Moskva bado iko.

    Sasa jeshi la Ukraine linadai kuwa meli hiyo ya Urusi ilianza kuzama baada ya kupigwa na makombora ya Neptune.

    Ikichapisha kwenye ukurasa wake wa Facebook, kamandi ya jeshi la kusini mwa Ukraine inasema meli hiyo ilipata uharibifu mkubwa na moto ulianza baada ya shambulizi .

    Meli za uokoaji za Urusi kisha zilitatizwa na risasi zilizolipuka ndani ya meli pamoja na hali mbaya ya hewa ambayo "ilipindua meli na kuanza kuzama", inaongeza.

  4. Bei ya petroli yaongezwa Kenya licha ya uhaba wa bidhaa hiyo

    Wenye magari nchini Kenya watalazimika kulipia zaidi mafuta baada ya bei ya Petroli, Dizeli na mafuta ya Taa kuongezwa kwa Shilingi 9.90.

    Kulingana na Mamlaka ya Udhibiti wa Kawi na Petroli (EPRA), petroli sasa itauzwa kwa Sh144.62 huku dizeli na mafuta taa zikigharimu Sh125.50 na Sh113.44 mtawalia.

    EPRA imesema bei hizo mpya zitadumishwa kati ya April 15 na Mei 14, 2022.

    Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Daniel Kiptoo alidokeza kuwa serikali itakubaliana na ushuru wa maendeleo ya mafuta ili kuwakinga Wakenya dhidi ya na bei ya juu bidhaa hiyo.

    Haya yanajiri baada ya serikali kuthibitisha kufukuzwa kwa Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Rubis Energy Kenya Jean-Christian Bergeron abaada ya mamlaka ya udhibiti wa kawi kusema kuwa itawachukulia hatua wachuuzi wa mafuta kwa kusababisha kile inachosema ni uhaba bandia wa mafuta nchini.

    Bw Bergeron bado hajatoa tamko lolote.

    Kulingana na Wizara ya Nishati, Kenya ina akiba ya kutosha ya bidhaa za petroli na uhaba huo umetokana na makampuni ya kuuza mafuta kuweka kipaumbele katika mauzo ya nje nchi.

    Hii ni sawa na uhujumu uchumi, ilisema. "Serikali haitavumilia chombo chochote au mtu ambaye anasababisha dhiki kwa kubuni tatizo bandia. Chombo chochote ambacho hakiko tayari kufanya kazi kwa mujibu wa sheria za Kenya kiko huru kuondoka katika soko hili mara moja," alisema Waziri wa Kawi, Monica Juma.

    Serikali imesema $295m (£225m) zinazodaiwa na wauzaji mafuta zimelipwa, huku $121m iliyosalia ikitarajiwa kutlipwa baadaye leo.

    Kenya imekumbwa na uhaba wa mafuta kote nchinikwa muda wa wiki mbili zilizopita hali ambayo imelemaza usafiri na shughuli za kiuchumi.

    Serikali inatarajia hali ya kawaida kurejeshwa ndani ya saa 72.

    Soma zaidi:

    • Wazijua bidhaa tatu zilizopanda bei Tanzania, Kenya na Uganda?
    • Bei ya Mafuta ya kula Afrika Mashariki: Je ni wakati wa kula chukuchuku?
    • Mzozo Ukraine: Je dunia inategemea vipi mafuta na gesi ya Urusi?
  5. Zaidi ya watu 300 wafariki katika mafuriko Afrika Kusini

    Idadi ya waliofariki katika jimbo la KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini imefikia zaidi ya 300, kufuatia mafuriko yaliyosababisha uharibifu mkubwa katika eneo hilo.

    Mamlaka za mitaa zinatoa wito wa hali ya maafa kutangazwa, baada ya baadhi ya maeneo kuona mvua ya miezi kadhaa kunyesha kwa siku moja.

    Maafisa wameiita "moja ya dhoruba mbaya zaidi ya hali ya hewa katika historia ya nchi yetu". Maporomoko ya udongo yamenasa watu chini ya majengo, huku mafuriko zaidi yakitarajiwa.

    Juhudi za uokoaji zimeripotiwa kutatizwa na ukungu huku helikopta ikiendelea kuwarejesha watu kwenye usalama

    Siku ya Jumanne BBC ilishuhudia oparesheni moja kama hiyo ya kumtafuta msichana mwenye umri wa miaka 10 ambaye alikuwa sehemu ya familia ya watu wanne waliosombwa na maji kwenye daraja lililofurika.

    Wafanyakazi wa kujitolea wa jumuiya waliingia kwenye mto wenye matope, kwa zamu ya kuteka matawi kwa kutumia mapanga na kuondoa uchafu na takataka zilizokuwa zimesombwa na mto huo.

  6. Cuba Gooding Jr: Muigizaji akiri kumbusu kwa lazima mhudumu

    Muigizaji Cuba Gooding Jr amekiri kumbusu mwanamke kwa nguvu, katika makubaliano ambayo yanatarajiwa kumaliza kesi ya jinai dhidi yake.

    Mshindi huyo wa tuzo ya Oscar alikiri shtaka la utovu wa nidhamu la kumbusu kwa lazima mhudumu katika kilabu cha usiku mnamo 2018.

    Ni lazima aendelee kutoa ushauri nasaha kwa muda wa miezi sita na kuepuka kukamatwa tena.

    Iwapo atafanya hivyo, anaweza kubatilisha ombi lake la sasa na badala yake kukiri kosa la unyanyasaji.

    Asipofanya hivyo, anaweza kufungwa jela mwaka mmoja.

    Gooding Jr, 54, alishinda Oscar kwa uhusika wake katika filamu ya 1996 Jerry Maguire, na pia anajulikana kwa filamu zikiwemo Boyz N The Hood na Men of Honour.

    Ameshutumiwa kuwapapasa na kuwagusa bila ridhaa yao zaidi ya wanawake 20, na tuhuma tatu zinazoongoza katika mashtaka ya jinai.

  7. Mjenga misuli nyota wa Marekani Cedric McMillan afariki dunia

    Mjenga misuli wa Marekani Cedric McMillan amefariki akiwa na umri wa miaka 44, baada ya miaka kadhaa ya matatizo ya kiafya yaliyosababishwa na Covid-19, na ajali ya barabarani.

    McMillan, mkongwe wa muda mrefu wa Jeshi la Marekani na Walinzi wa Kitaifa, alikuwa mjenga misuli mkongwe na mshindi wa 2017 wa taji la kifahari la Arnold Classic.

    Kifo chake kilithibitishwa mtandaoni na mfadhili wake, Black Skull USA, ingawa sababu haijawekwa wazi.

    Ni kifo cha tatu cha mjenga misuli mashuhuri nchini Marekani katika mwaka uliopita.

    "Tunasikitika kuwafahamisha kuwa rafiki na kaka yetu @cedricmcmillan amefariki leo," Black Skull USA alisema kwenye Instagram. "Cedric atakumbukwa sana kama mwanariadha, mwanachama mwenzetu, rafiki na baba."

    McMillan amekuwa mtaalamu wa kujenga misuli tangu 2009, kabla ya kushinda mfululizo wa mashindano kilele chake ikiwa 2017 aliposhinda Arnold Classic, iliyopewa jina la mjenzi wa misuli, mwigizaji na gavana wa zamani wa California Arnold Schwarzenegger.

  8. Afrika Kusini yamshutumu Balozi wa Ukraine kwa 'ukiukaji wa diplomasia'

    Afrika Kusini imemshutumu balozi wa Ukraine nchini humo kwa kutumia njia "zisizo za kidiplomasia" kuomba mazungumzo na Rais Cyril Ramaphosa kuhusu uvamizi wa Urusi unaoendelea katika nchi hiyo ya Ulaya mashariki.

    Balozi Liubov Abravitova anasema alilazimika kutumia Twitter kuomba kukutana na rais.

    Alishutumu mamlaka ya Afrika Kusini kwa madai ya kupuuza maombi yake mengi ya kukutana na Bw Ramaphosa na mawaziri wengine.

    "Tangu kuanza kwa uvamizi wa Urusi, sijapokea ombi lolote la mkutano kutoka kwa maafisa wa serikali ya Afrika Kusini.

    Watu wangu wanakabiliwa na mashambulizi ya kikatili kutoka kwa Warusi muda huu, "Bi Abravitova aliandika katika Aprili Twitter 10.

    Hata hivyo afisa mkuu wa wizara ya mambo ya nje ya Afrika Kusini Clayson Monyela, amekanusha madai ya mjumbe huyo, akisema tayari alikuwa amefanya mikutano na maafisa kadhaa wa serikali.

    "Balozi, unajua hii sio sawa na sio njia ya kidiplomasia. Tumetuma ombi kwa muda mrefu kwa Mhe. Rais Cyril Ramaphosa kuzungumza na rais wako. Hujatoa jibu,” Bw Monyela alimjibu kwenye Twitter.

    Balozi huyo alitetea hatua yake, akisema: "Sina chaguo tu, sina wakati. Watu wangu wanakufa, wanateswa, wanabakwa.”

    Afrika Kusini imekabiliwa na ukosoaji wa msimamo wake wa kutoegemea upande wowote kuhusu uvamizi wa Urusi nchini Ukraine.

    Wiki iliyopita, nchi hiyo ilijiepusha na kura ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa iliyotaka kuisimamisha Urusi katika Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa.

  9. Urusi ilivamia Mariupol lakini haikufaulu - Jeshi la Ukraine

    Leo ikiwa ni siku ya 50 ya uvamizi wa Urusi, jeshi la Ukraine linasema kuwa vikosi vya Urusi vinaendelea kurusha makombora na mabomu kwenye miundombinu ya kijeshi na kiraia katika mikoa ya Kharkiv, Donetsk na Zaporizhzhia.

    • Vikosi vya Urusi vinaendelea kuimarisha vitengo vya silaha, kuboresha mifumo iliyopo ya amri, kijasusi na usaidizi wa kimatibabu karibu na mpaka wa mashariki mwa Ukraine.
    • Wanajeshi wa Urusi kupiatia mshirika wake Belarus wanaendelea kutekeleza majukumu ya kufunga maeneo ya Brest na Gomel yanayopakana na Ukraine na Belarus.
    • Huko Slobozhansky kaskazini-mashariki mwa Ukraine, vikosi vya Urusi vinafanya uchunguzi wa maeneo yanayoweza kushambulia.
    • Pia wanaendelea kudhibiti kwa kiwango fulani mji wa Kharkiv huku ushambuliaji wa makombora ukiendelea katika eneo hilo.
    • Huko Donetsk mashariki mwa Ukraine, vikosi vya Urusi vilipigana katika wilaya za Slavyansk, Popasna, na Kurakhovo, na kuvamia jiji la bandari la Mariupol bila mafanikio.
    • Vikosi vya Ukraine viliharibu vifaru, vitengo vinne vya kivita na magari sita, pamoja na mfumo wa mizinga ya Urusi.

    BBC haijafanikiwa kuthibitisha madai.

    Unaweza pia kusoma

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
    • SILAHA:Mzozo wa Ukraine:Makombora ya stinger na silaha nyingine kali zinazotumiwa Ukraine
  10. Mtendaji Mkuu raia wa Ufaransa kufurushwa Kenya kufuatia mzozo wa mafuta

    Mamlaka nchini Kenya imeripotiwa kufuta kibali cha kufanya kazi cha mtendaji mkuu wa Ufaransa wa mojawapo ya kampuni ya kubwa ya kuuza mafuta nchini Kenya kutokana na tatizo la uhaba wa bidhaa hiyo.

    Serikali inasemekana kuamuru kufukuzwa nchini kwa Christian Bergeron, mtendaji mkuu wa Rubis Energy Kenya - kampuni tanzu ya Rubis Group yenye makao yake nchini Ufaransa.

    Siku ya Jumanne mamlaka ya udhibiti wa kawi nchini humo iliwashutumu baadhi ya wauzaji mafuta kwa kuzuiausambazaji wa mafuta katika soko la ndani na kutoa kipaumbele kwa mauzo ya mafuta kwa nchi jirani.

    Mamlaka hiyo aidha ilisema kampuni hizo zitaadhibiwa kwa kupunguziwa kiwango cha mafuta watakayoruhusiwa kuagiza kwa muda wa miezi mitatu ijayo.

    Makampuni ya mafuta ya Kenya yanauza takriban 65% ya bidhaa zao kutoka nje kwa soko la ndani na nyingine kwa nchi jirani zisizo na bandari kama vile Uganda, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Kumekuwa na uhaba mkubwa wa bidhaa hiyo katika wiki za hivi karibuni kote nchini, huku milolongo mirefu ya magari katika vituo vya kuuza mafuta.

    Mamlaka ya Kenya inasema kuna mafuta ya kutosha katika hifadhi yake.

    Kuna uvumi kwamba baadhi ya wauzaji wamekuwa wakihifadhi mafuta kwa kutarajia ongezeko la bei leo Alhamisi wakati bei za mwezi ujao zitatzngazwa.

    Wataalamu wanasema mzozo wa sasa nchini Kenya umesababishwa na kucheleshwa kwa utoaji ruzuku ya mafuta inayodaiwa na wauzaji mafuta.

    Kenya inatoa ruzuku kwa bei ya mafuta ili kuwakinga raia wake dhidi ya bei ya juu mafuta.

    Lakini wauzaji mafuta wamekuwa wakilalamikia kucheleweshwa kwa malipo ya kufidia bei wanayotoza watumiaji inayotakiwa kulipwa na serikali kama ruzuku.

    Serikali ilitoa baadhi ya malipo yaliyocheleweshwa wiki iliyopita.

    Soma zaidi:

    • Wazijua bidhaa tatu zilizopanda bei Tanzania, Kenya na Uganda?
    • Bei ya Mafuta ya kula Afrika Mashariki: Je ni wakati wa kula chukuchuku?
    • Mzozo Ukraine: Je dunia inategemea vipi mafuta na gesi ya Urusi?
  11. Mahakama yazuia mali za Roman Abramovich zenye thamani ya dola bilioni 7

    Roman Abramovich amelazimishwa kuuza klabu ya Chelsea FC na kuihahamisha mashua yake ya kifahari nje ya maji ya nchi za Muungano wa ulaya.

    Mali za birionea wa Mrusi Roman Abramovich zenyethamani ya dola bilioni 7 (£5.4bn) zinazohusiana naye zimefujwa na mahakama yaJersey.

    Jumanne, polisi ya Jersey ilisaka eneo linaloshukiwa kuwa na shuguli za kibiashara zenye uhusiano na Bw Abramovich katika kisiwa hicho, Maafisa wa idara ya sheria ya walisema.

    Bilionea Abramovich yuko katika orodha ya vikwazo vya Uingereza vinavyohusiana na vita vya Urusi katika Ukraine.

    Kisiwa cha Channel Island Jersey kinafuata sera ya Uingereza na kuwawekea vikwazo watu walioko kwenye orodha hiyo ya Uingereza.

    "Mahakama hiyo pia iliweka amri rasmi tarehe 12 Aprili, inayofahamika kamasaisie judiciaire, juu ya mali zinazofahamika kuwa na thamani ya zaidi ya dola bilioni 7 za Kimarekani ambazo zinashukiwa kuwa na uhusiano na Bw Abramovich na ambazo zinapatikana Jersey au zimeingizwa katika taasisi zaJersey," Maafisa idara ya sheria wa Jersey walisema.

    Bw Abramovich alikuwa ni miongoni mwa matajiri Warusi walioongezwa mwezi uliopita kwenye orodha ya uingereza na muungano wa Ulaya ya vikwazo , ambao tayari wamekwishachukuliwa hatua ya kuchukuliwa kwa mashua zao za kifahari na mali zao nyingine za kifahari.

    Bilionea huyo alijaribu kuuza klabu ya soka ya Chelsea katika mwezi March, lakini mchakato huo uliondolewa mikononi mwake na serikali baada ya kuwekewa vikwazo.

    Mapema mwezi huu, taifa la Caribbean la Antigua and Barbudalilisema liko tayari kuisaidia Uingereza kushikilia mashua zinazomilikiwa na Abramovich.

    Boti hizo za kifahari zilizohusishwa na mfanyabiashara Abramovich, kwa pamoja zina thamani inayokadiriwa kuwa ya dola bilioni 1.2 na kwa sasa zimetia nanga kusini mwa Uturuki, nje ya eneo la Muungano wa Ulaya na uingereza.

  12. Hujambo na karibu kwa matangazo yetu mubashara leo tarehe 14.04.2022