Idadi ya waliofariki kutokana na kimbunga yafikia 111 Msumbiji

Chanzo cha picha, afp
Takriban watu 111 nchini Madagascar sasa wanadaiwa kufariki tangu Kimbunga Batsirai kilipopiga kisiwa kimoja cha Bahari Hindi karibu wiki moja iliyopita.
Nyumba nyingi zilibomoka kutokana na upepo mkali, na kuwaacha takriban watu 30,000 wakiishi katika makazi ya dharura, kulingana na shirika moja la kukabiliana na za kitaifa.
Mataifa ya Kusini mwa Afrika hivi majuzi yamekuwa yakikabiliana kimbuga Ana.
Vimbunga vimekuwa jambo la kawaida kawaida katika sehemu hii ya lakini tatizo la mabadiliko ya tabia nchini yamechochea ya hali ya hewa na kuvifanya vimbunga hivyo kuwa hatari zaidi.
Hali hiyo imechangia kuwepo kwa ukame, ambao umeathiri sana kusini mwa Madagascar, na hivyo kusababisha wito wa misaada ya kibinadamukwa haraka.
Nchini Madagascar, vifo 87 kati ya 111 vilivyotokana na Kimbunga Batsirai vilikuwa katika wilaya ya kusini-mashariki ya Ikongo.
Watu wote 55 waliouawa kutokana na kimbunga Ana walikuwa wanatoka sehemu nyingine ya Madagascar iliopo kaskazini reuters inaripoti.











