Mcheshi Eric Omondi azua sintofahamu bungeni Kenya
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa Instagram ujumbe
Mchekeshaji wa Kenya Eric Omondi hii leo amezua sintofahamu nje ya majengo ya bunge nchini Kenya baada ya kujifungia katika kisanduki kinachoonesha ndani.
Kwa mujibu wa gazeti la The standard, lengo lake lilikuwa kushinikiza bunge kujadili muswada unaopatia kipaumbele asilimia 75 ya muziki wa Kenya kuchezwa katika maeneo yote nchini.
‘’Huu ni mgomo wa kutokula na nitasalia hapa hadi wabunge watakapojadili muswada huu’’, Omondi alinukuliwa na gazeti la The Standard akisema.
‘’Natangaza rasmi mgomo wa kula, iwapo nitalazimika kusalia hapa kwa miezi miwili, basi ni sawa. Iwapo nitakufa hapa kwasababu ya kutokula pia ni sawa’’, Omondi alisema.
Tayari Mbunge wa Dagoretti nchini Kenya John Kiarie amewasilisha muswada bungeni unaosema kwamba suala linalowasilishwa na mcheshi huyo litajadiliwa.
Miezi miwili iliopita mcheshi huyo alikamatwa alipokuwa akijaribu kuvamia bunge kwa suala hilo hilo.
‘’Nilipokuwa hapa siku za nyuma , nilisalia peke yangu , hakuna msanii hata mmoja wa muziki alinisaidia kupigania maslahi yao’’, Omondi alilalama.
Lengo lake amesema kwamba ni kuhakikisha kuwa muswada huo unapitishwa kufikia machi mwezi huu ili kuwasaidia wasanii nchini kenya.













