Hamis Tale, asema harakati za kumpinga Diamond kushinda tuzo za BET hazitafanikiwa

Meneja wa Msanii wa muziki wa Kizazi kipya nchini Tanzania; Diamond Platnumz, Hamis Tale Tale, amesema harakati za kumpinga msanii huyo kushinda tuzo za mwaka huu za BET hazitafanikiwa.

Moja kwa moja

Dinah Gahamanyi

  1. Nyota wa PSG Mauro Icardi awasili Tanzania

    Mauro Icardi

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Mauro Icardi

    Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Argentina na Klabu ya PSG inayoshiriki ligi kuu ya Ufaransa, Mauro Icard amewasili nchini Tanzania.

    Nyota huyo aliwasili na mkewe Wanda Icardi nchini humo kwa likizo ya siku kadhaa.

    Wawili hao wanadaiwa kuwa katika hifadhi moja ya wanyamapori ambapo wanajivinjari.

    Wakati Icardi akiendelea na mapumziko yake nchini Tanzania, timu yake ya Taifa ilienda sare ya 1-1 wiki hii na mahasimu wao Chile, mchexzo wa kufuzu fainali za kombe la dunia mwakani.

    Kwa sasa Icardi amepoteza nafasi katika timu ya taifa, ambapo kocha Leonel Scaloni amekuwa akiwatumia zaidi Lionel Messi, Lautaro Martinez na Sergio Aguero.

    Ruka Instagram ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa Instagram ujumbe

  2. Aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai Tanzania amefikishwa mahakamani

    ITV

    Chanzo cha picha, ITV

    Aliyekuwa mkuu wa Wilaya Hai, Lengai Ole Sabaya amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha kujibu tuhuma inazomkabili.

    Sabaya amefikishwa mahakaman akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi akiwa na walinzi wake sita na baada ya kushuka kwenye magari pamoja na wenzake walitakiwa kuchuchumaa kusubiri taratibu nyingine.

    Baada ya muda mfupi walichukuliwa na kupelekwa katika chumba maalum wakisubiri kupelekwa mahakamani.

    Kwa takribani wiki moja Sabaya alikuwa akihojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) kwa tuhuma mbalimbali.

    ITV

    Chanzo cha picha, ITV

    Maelezo ya picha, Mwezi uliopita Rais wa Tanzania, Samia Suluhu alimuachisha kazi Bw Lengai Ole Sabaya ili kuruhusu uchunguzi

    Mwezi uliopita Rais wa Tanzania, Samia Suluhu alimuachisha kazi Bw Lengai Ole Sabaya ili kuruhusu uchunguzi kuhusiana na madai dhidi yake.

    Taarifa iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Gerson Msigwa tarehe 13 Mei, haikuelezea sababu za kusimamishwa kazi kwa Mkuu huyo wa Wilaya ambaye wakati mmoja alikuwa mwenyekiti wa UVCCM Arusha.

    Sabaya aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Kilimanjaro na aliyekuwa rais wa Tanzania hahayati John Magufuli mwaka 2018 .

  3. Umoja wa Mataifa wataka wanaharakati wa mapenzi ya jinsia moja waliokamatwa waachiliwe

    Walikamatwa wiki mbili zilizopita walipokuwa katika mkutano

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Walikamatwa wiki mbili zilizopita walipokuwa katika mkutano

    Wataalam wa Shirika la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa wametoa wito wa kuachiliwa kwa wanaharakati wapenzi wa jinsia moja 21 wakike, wa kiume, waliobadili jinsia na wenye jinsia mbili (LGBT+) waliokamtwa mwezi uliopita.

    Watetezi hao wa haki za makundi hayo al maarufu kama LGBT+ walikamatwa yapata wiki mbili zilizopita wakati walipokuwa wakihudhuria mkutano kusini-mashariki mwa Ghana na walishitakiwa kwa kuwa katika mkusanyiko usio wa kisheria.

    Ijumaa, wataalam wa Umoja wa Mataifa katika taarifa yao walielezea hofu yao ‘’kubwa’’ na kulaani kukamatwa kwao na kufungwa ambako wamesema kulikuwa na misingi ya ubaguzi ikiwa ni pamoja na kubaguliwa kutokana na jinsia yao.

    “Ushahidi wote uliopo kwetu unaonesha ukweli kwamba walifungwa wakati walipokuwa wakitekeleza haki zao za uhuru wa kujieleza, na kukusanyika kwa amani.

    “Serikali ya Ghana inapaswa kuwachilia huru mara moja bila masharti,” walisema.

    Wanaharakati hao wanakwenda mahakamani Ijumaa.

  4. Watoto wa kike wadogo wakamatwa na polisi wakiendesha gari

    Polisi

    Chanzo cha picha, @WVCPD

    Wasichana wawili mmoja wa miaka 4 na mwingine wa miaka 9 wamekatwa wakiendesha gari kwenda kuogelea.

    Polisi wa Utah wanasema kuwa "wamepigwa na butwa" baada ya kuona mtoto mwenye umri wa miaka tisa akiendesha gari, huku akimuendesha mdogo wake wa miaka minne.

    Watoto hao wawili wasichana waliwaambia polisi kuwa walikuwa wakiendaCalifornia kwasababu wanataka "kuoga baharini".

    Walipita katika barabara kuu mbili, wakagonga gari lingine, baadaye wakagongana na lori, kama polisi walivyoifananisha Twitter.

    Watoto hawa ndugu walikuwa wamevaa mikanda kwa hiyo hakuna hata mmoja wao aliyeumia.

    Picha za video zilizochukuliwa na polisi waliokwenda kwenye tukio zilioneshwa kwenye mtandao wa Twitter wa polisi wa Utah:

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Polisi wa Jiji la West Valley City lkatika jimbo la Utahwanasema wasichana hao wadogo awaliamka saa tisa usiku Jumatano,wakaingia ndani ya gari aina ya Chevrolet Malibu, wakaingia barabarani kutoka nyumbani kwao, wakati wazazi wao walipokuwa wamelala fofofo.

    Dereva wa lori ndiye aliyewaita polisi baada ya kugongwa na gari la watoto hao.

  5. Akamatwa kwa kujaribu kuwauza watoto wake mapacha

    Mwanamke mmoja nchini Afrika Kusini amekamatwa pamoja na watu wengine wawili kwa madai ya kujaribu kuwauza watoto wake wawili wachanga pacha, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti.

    Mama huyo anadaiwa kuwa mraibu wa madawa ya kulevya na alijaribu kuwauza watotowake kwa ajili ya 'kukata kiu uraibu wa dawa", msemaji wa polisi Yolisa Mgolodela, alinukuliwa akisema.

    Mapacha wa siku tano wasichana walipelekwa kwasababu walikuwa na "upungufu wa maji mwilini na utapiamlo", ilisema polisi.

    Washukiwa wanatarajiwa kufika mahakamani kujibu mashtaka ya ulanguzi wa binadamu Jumatatu.

  6. Hamis Tale Tale, asema harakati za kumpinga Diamond kushinda tuzo za BET hazitafanikiwa

      • Author, Yusuph Mazimu
      • Nafasi, BBC Swahili
    Diamond

    Meneja wa Msanii wa muziki wa Kizazi kipya nchini Tanzania; Abdul Nassib maarufu kama Diamond Platnumz, Hamis Tale Tale, amesema harakati za kumpinga msanii huyo kushinda tuzo za mwaka huu za BET hazitafanikiwa.

    Wanaompinga msanii huyo kupitia mitandao ya kijamii wanadaiwa kufanya hivyo ili kuonyesha hisia zao kutokana na msanii huyo kushiriki kampeni za Uchaguzi mkuu wa nchi hiyo na kukiunga mkono chama tawala cha CCM, kilichoshinda ushaguzi mkuu wa 2020.

    Hamis Tale Tale maarufu kama Babu Tale na ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, katika mkoa wa Morogoro, ameiambia BBC kwamba, wanoendesha kampeni hiyo si mashabiki halisi wa msanii huyo. ‘Hao wanaosema hawatamuunga mkono Diamond si mashabiki wa Diamond na hawajawahi kuwa mashabiki wa Diamond, shabiki hushabikia kile anachokipenda, yaani kufa na kupona’, alisema Tale.

    Akizungumzia suala hilo, Msanii kutoka Kenya, Ole Karai alionyesha masikitiko kwa wanaaopinga Diamond kwenye tuzo hizo akisema sanaa na siasa ni vitu ambavyo vinaendana. ‘Ni jambo la kusikitisha sana kuona msanii kutoka Afrika, anawakilisha Afrika, ili hali kuna watu ambao wanapiga vita mafanikio ya Afrika’, alisema Karai.

    Diamond aliyeshinda tuzo zaidi ya 40 katika mkipindi cha miaka 10 iliyopita ametajwa kuwania tuzo maarufu za mwaka huu za BET katika kipengele cha ‘Best International Act’ akichuana na wasanii wengine maarufu duniani ambao ni Wizkid, Burna Boy, Emicida, Aya Nakamura, Youssoupha, Headie na Young T& Bugsey kutoka Uingereza. Ni mara ya tatu sasa kutajwa katika tuzo hizo, alitajwa pia mwaka 2014 na 2016 ambapo hakushinda na iwapo atashinda sasa atakuwa msanii wa pili kutoka Tanzania kushinda tuzo hiyo baada ya msanii aliye katika lebo yake ya Wasafi, Rayvanny kushinda mwaka 2017 katika kipengele cha ‘Viwer’s Choice Best New International Act’.

  7. Rais wa Kenya akosolewa kwa kuwakataa majaji

    Siku za nyuma Rais Kenyatta alishutumiwa kwa kutoheshimu maagizo ya mahakama

    Chanzo cha picha, AFP

    Maelezo ya picha, Siku za nyuma Rais Kenyatta alishutumiwa kwa kutoheshimu maagizo ya mahakama

    Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amekosolewa kwa kukataa kuidhinisha uteuzi wa majaji sita.

    Majaji hao sita ni miongoni mwa majaji 41 ambao walikuwa wamependekezwa kwa ajili ya uteuzi na Tume ya Huduma za mahakama nchini humo (JSC) miaka miwili iliyopita . Mmoja wa majaji hao alifariki.

    Rais Kenyatta amekataa mapendekezo ya JSC licha ya maagizo mawili ya mahakama yaliyomtaka kufanya hivyo.

    Alhamisi hii, rais ameidhinisha uteuzi wa majaji 34 na kuwaacha sita- wakiwemo majaji wawili ambao walikuwa miongoni mwa majaji watano ambao hivi karibuni walitangaza kuwa mchakato wa kufanyia marekebisho ya katiba (BBI) ulikiuka katiba.

    Wataalamu wa sheria nchini Kenya wanasema rais hawezi kubadili orodha ya majaji walioteuliwa au mapendekezo ya JSC na hana chaguo ila kuwaidhinisha majaji wote walioteuliwa na tume hiyo

    Hivi karibuni Bw Kenyatta aliishutumu mahakama kwa "kuvijaribu vikomo vya katiba" baada ya mahakama ya juu nchini hukmo kuzuia mpango wa serikali wa kufanya marekebisho ya katiba.

    Chama cha mawakili nchini Kenya(LSK) kimesema kuwa kuondoa au kushindwa kuwateua majaji 6 ni ukiukaji wa kipengele cha sura ya 116 ya katiba, na ni ukiukaji hoja ya kikatiba nambari 369 ya 2019, iliyotolewa na Adrian Kamotho Njenga dhidi ya Mwanasheria Mkuu, ambapo mahakama iliafiki kwamba Tume ya huduma za mahakama inapotoa mapendekezo, rais hana chaguo jingine bali ni kuidhinisha uteuzi.

    ‘’Rais hawezi kubadilisha orodha, kuitathmini au kuyakataa baadhi ya maneno. Anapaswa kuwateua watu kulingana na majina kama walivyopendekezwa na kupelekwa kwake na Tume ya huduma za mahakama’’, imeeleza taarifa ya LSK.

  8. DRC yakabiliwa na wimbi la tatu la Corona

    DRC

    Chanzo cha picha, UN

    Maelezo ya picha, Mji mkuu Kinshasa ni kitovu cha maambukizi hayo DRC

    Jamhuri ya Kidemokrasi Congo inakabiliwa na wimbi la tatu la maambukizi ya virusi vya corona, huku mji mkuu Kinshasa ambao ni mji wenye idadi kubwa zaidi ya watu Afrika, ukiwa ni kitovu cha maambukizi hayo, amesema Waziri wa afya Jean-Jacques Mbungani Alhamisi.

    Sawa na mataifa mengine ya Afrika, Congo imeripoti maambukizi na vifo vichache, lakini maafisa wa afya wanahofu juu ya ongezeko kubwa la maambukizi ambapo watu 243 walipatikana na Corona Jumatano, kikiwa ni kiwango cha juu zaidi tangu ulipotokea mlipuko mwezi Machi.

    "Nilitangaza rasmi mara moja wimbi la tatu la janga la Covid-19 nchini mwetu, Kinshasa kikiwa ni kitovu cha maambukizi," Mbungani aliwaambia waandishi wa habari

    Kiwango cha chini cha idadi ya waliochanjwa na kukosa kudumisha usafi ni miongoni wa sababu za kuongezeka kwa kiwango cha maambukizi, alisema.

    Kampeni ya chanjo DRC imekwama baada ya kucheleweshwa kuanza kwasababu ya hofu ya usalama wa wa chanjo ya AstraZeneca

    Chanzo cha picha, OLIVIA ACLAND / UNICEF

    Maelezo ya picha, Kampeni ya chanjo DRC imekwama baada ya kucheleweshwa kuanza kwasababu ya hofu ya usalama wa wa chanjo ya AstraZeneca

    Jumatano, Shirika la afya duniani (WHO), lilisema lilinahofu juu ya kusambaa kwa aina ya kirusi cha corona cha Delta ambacho kilibainika kwa mara ya kwanza nchini India , ambayo inadhaniwa kuwa ndio inayosambaa zaidi.

    Mwishoni mwa juma lililoishia tarehe 30 Mei, kulikuwa na ongezeko la viwango vya maambukizi mjini Kinshasa, WHO imesema

    Kampeni ya chanjo DRC imekwama baada ya kucheleweshwa kuanza kwasababu ya hofu ya usalama wa chanjo ya AstraZeneca. Matokeo yake, takriban, 75% ya dozi milioni 1.7 ilizopokea mwezi Machi zilipelekwa katika mataifa mengine ili kuhakikisha zinatumiwa kabla ya muda wake kuisha.

    Kwa jumla, Congo imeripoti zaidi ya maambukizi 31,900 na vifo 786 vilivyohusishwa na virusi vya corona tangu janga lilipoanza.

    Miongoni mwa wahanga wa corona ni pamoja na wabunge 32, idadi hiyo ikiwa ni sawa na 5% ya jumla ya watu waliouliwa na virusi, maafisa walisema wiki iliyopita.

  9. Aliyetoroka jela mara ya 12 akamatwa tena Senegal

    gereza

    Chanzo cha picha, AFP

    Mfungwa wa Senegal anayefahamika kama Mtoro sugu wa jela , Baye Modou Fall ambaye alitoroka Jumamosi kutoka gerezani katika mji mkuu Dakar amekamatwa tena.

    Ilikuwa ni mara ya 12 akitoroka kutoka kwenye magereza nchini, vimeripoti vyombo vya habari nchini humo.

    Alikamatwa katika eneo la Moussala mashariki mwa nchi karibu na mpaka taifa jirani la Mali, msemaji wa jeshi la Senegal aliliambia Shirika la habari la AFP.

    Mfungwa huyo mwenye umri wa miaka 32, ambaye anafahamika kama"mtoro sugu " Jumatatu aliiambia televisheni nchini humo kwamba alikuwa ametoroka kwasababu mchakato wa sheria ulikuwa unachukua muda mrefu sana na alitoroka kupitia ukuta wa gereza akitumia kamba

    Alielezea jinsi alivyotoroka kutoka gerezani kwa kuvunja kifaa kinachoingiza hewa ndani ya seli ya mahabusu na kupanda juu ya ukuta akitumia kamba.

    Maafisa wanachunguza iwapo kuna mtu aliyemsaidia kutoroka.

  10. Hujambo na karibu kwa matangazo haya mubashara leo tarehe 04.06.2021