Mrithi wa Bensouda katika mahakama ya (ICC) kujulikana leo

Wajumbe wa nchi wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wanakutana mjini New York baadaye leo kumchagua mwendesha mashitaka mpya wa mahakama hiyo.

Moja kwa moja

Lizzy Masinga and Dinah Gahamanyi

  1. Kamanda wa jeshi nchini Rwanda afariki dunia

    Aliyekuwa Mkuu wa jeshi la Rwanda, Luteni Jenerali Jacques Musemakweli, amefariki "kifo cha kawaida" Alhamisi katika hospitali ya jeshi, kulingana na Kikosi cha Ulinzi cha Rwanda.

    "Ndio, Jenerali Musemakweli amefariki, alikuwa mgonjwa," afisa mwandamizi wa jeshi la Rwanda aliiambia BBC.

    Jenerali Musemakweli aliteuliwa kuwa mkuu wa ukaguzi wa Kikosi cha Ulinzi cha Rwanda mnamo Novemba 2019.

    Hapo awali alishikilia nyadhifa za mkuu wa jeshi, mkuu wa walinzi wa rais na kamanda wa vikosi vya akiba.

    Alikuwa mwanachama wa Rwandan Patriotic Front (RPF), kikosi cha waasi kilichoongozwa na Paul Kagame kilichoingia madarakani mnamo 1994.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

  2. Rubani wa jeshi la Uganda afariki katika ajali ya helikopta

    Jeshi la Uganda limethibitisha kifo cha rubani wa helikopta iliyoanguka muda mfupi tu baada ya kuondoka kwenye uwanja wa ndege wa Entebbe siku ya Alhamisi.

    Msemaji wa jeshi la Uganda UPDF) Brigadia Flavia Byekwaso amesema tukio hilo lilitokea wakati wa kupindi cha mafunzo ya uendeshaji wa ndege.

    "TLeo mchana majira ya saa nane na robo ndege aina ya jet iliyokuwa ikiendeshwa na marubani wawili wanafunzi wa mafunzo ya kijeshi ya cadet ilianguka mara moja baada ya kuondoka karibu na ufukwe wa Lido (Lido beach). Wawili hao walikimbizwa hospitalini kuchunguzwa afya zao ," alisema.

    Marehemu alitambuliwa kama Kapteni Caroline Busingye.

    Ruka X ujumbe, 1
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 1

    Gazeti la kibinafsi nchini humo, Daily Monitor lilitweet picha za kifusi cha helikopta hiyo:

    Ruka X ujumbe, 2
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe, 2

  3. Serikali yapiga marufuku maandamano mapya Nigeria

    Maandamano

    Chanzo cha picha, EPA

    Waziri wa Habari Lai Mohammed ameonya dhidi maandamano yaliyopangwa kufanyika huko Lekki jijini Lagos ambapo vikosi vya usalama viliwafyatulia risasi waaandamanaji mwezi Oktoba mwaka jana.

    Maandamano mapya, yaliyopewa jina la 'Occupy Lekki toll gate', yamepangwa kufanywa Jumamosi Waandaaji wanasema watagomea dhidi ya kufunguliwa tena kwa lango la ushuru.

    Bwana Mohammed amesema serikali haitaruhusu maandamano mengine kufanyika. Alisema wahalifu wanaweza kuvamia maandamano na kusababisha watu kupoteza maisha na uharibifu wa mali.

    Amesema matangazo ya kuwataka watu kujitokeza kwenye maandamano yamekuwa yakisambazwa

    Waziri aliongeza kuwa serikali ilikubaliana na matakwa ya awali na kuachiwa kwa waandamanaji waliokuwa wamekamatwa wakati wa wimbi la kwanza la maandamano na kuunda tume huru kutazama suala la ukatili wa polisi.

  4. Mrithi wa Bensouda katika mahakama ya (ICC) kujulikana leo

    Bi Bensouda amekuwa Mwendesha mashitaka Mkuu wa ICC tangu mwaka 2011
    Maelezo ya picha, Bi Bensouda amekuwa Mwendesha mashitaka Mkuu wa ICC tangu mwaka 2011

    Wajumbe wa nchi wanachama wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wanakutana mjini New York baadaye leo kumchagua mwendesha mashita mpya wa mahakama hiyo.

    Wagombea tisaikiwa ni pamoja na majaji wawili mmoja kutoka Nigeria na mmoja kutoka Uganda, wako katika orodha ya kumrithi Mgambia Bi Fatou Bensouda, ambaye muhula wake kama Mwendesha mashitakaMkuu wa mahakama hiyo unamalizika mwezi Juni mwaka huu.

    Bi Bensouda amekuwa Mwendesha mashitaka Mkuu wa ICC tangu mwaka 2011- baada ya kuchukua nafasi ya wakili Muargentina Luis Moreno Ocampo.

    Katika muhula wake madarakani, aliweza kuwatia hatiani washitakiwa Zaidi kuliko mtangulizi wake- na hivi karibuni ikiwa akiwa ni muasi wa zamani wa Uganda kamandaDominic Ongwen ambaye mwezi huu alipatikana na hatia za uhalifu wa kivita.

    Hatahivyo alikabiliwa na ukosoaji mkubwa hususan ni kuhusu kesi zake kuwalenga Waafrika. Mwezi Juni mwaka jana, Bensouda alizuiwa kusafiri nchini Marekani wakati rais wa Marekani wa wakati huo Donald Trump aliposaini sheria ya rais inayoweka vikwazo vya fedha dhidi yake.

    Watu wengine wanaowania nafasi ya Bensouda ni pamoja na:

    1:Karim Khan- Wakili Kutoka Uingereza

    2. Robert Petit, Mwendesha mashitaka kutoka Canada

    3.Susan Okalany- Jaji kutoka Uganda

    4. Morris Anyah- Jaji kutoka Nigeria

    5. Fergal Gaynor - mwendesha mashitaka kutoka IRELAND

    6. Fernandez Castresana- mwendesha mashitaka kutoka Uhispania

    7. Francesco Lo Voi- mwendesha mashitaka kutoka Italia.

    8. Brigitte Raynaud – mwendesha mashitaka kutoka Ufaransa

    9. Richard Roy – wakili kutoka Canada

  5. Mahakama ya kijeshi yahukumu raia kifungo cha miaka 100 Uganda

    Mahakama

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mahakama ya Wilaya huko Mbarara imewahukumu raia wawili kifungo cha miaka 100 gerezani kwa kosa la kumuua afisa wa polisi na kukimbia na silaha yake katika wilaya ya Kabale.

    Wawili hao; Mukwenda Mugisha,19, mkazi wa kijiji cha Gatete na Paul Dusingizimana, 27 mkazi wa Manispaa ya Kabale walipatiwa hukumu hiyo siku ya Alhamisi. Gazeti la Daily Monitor la Uganda limeripoti.

    Mashtaka yakingozwa na Luteni James Omondi yaliyowasilishwa tarehe 24 mwezi Januari, yamesema Mugisha na Dusingizimana walimshambulia na kumuua Gracious Byaryabakabu aliyekuwa zamu ya kulinda Ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya Wilaya ya Kabale.

    Walimpora silaha yake iliyokuwa na risasi takribani 30.

    ''Watuhumiwa hao pia walimpora Godfrey Tukamubona simu yake ya mkononi yenye thamani ya shilingi 60,000 baada ya kumsababishia madhara makubwa, alisema

    Mahakama pia ilielezwa kwamba mnamo Januari 29, wakiwa katika gereza la Rutenga katika Manispaa ya Kabale, wawili hao walimtisha Patrick Arinaitwe kwa bunduki, walimteka nyara na kumuibia Sh20,000 zilizokuwa kwenye akaunti ya simu ya mkononi

    Watuhumiwa walikutwa na hatia ya makosa yote matatu ya unyang'anyi, mauaji na utekaji nyara.

    Hata hivyo wawili hao wameomba huruma ya mahakama ya kuwapunguzia adhabu kwani walikuwa ''wamelewa '' walipokuwa wakitekeleza vitendo hivyo.

  6. Karibu kwa matangazo yetu mubashara leo Ijumaa tarehe 12.02.2021