IGP Sirro: Hakuna marufuku ya kukimbia siku za ibada

Mkuu wa jeshi la polisi nchini Tanzania IGP Simon Sirro amefanunua juu ya marufuku kwa wakimbiaji wa mbio za pole pole (Jogging) iliyotolewa na Kamanda wa polisi kanda ya Dar es salaam, Lazarus Mambosasa.

Moja kwa moja

Dinah Gahamanyi

  1. Virusi vya Corona: Saudia yapiga marufuku raia wa kigeni kuizulu

    Saudia

    Chanzo cha picha, AFP

    Vyombo vya habari nchini Saudi Arabia vinaripoti kuwa nchi hiyo imeweka marufuku dhidi ya raia wasio wa nchi hiyo kuingia nchini humo, wakiwemo mabalozi, wahudumu wa afya na familia zao.

    Hatua hiyo itaziathiri nchi 20, huku Saudi Arabia ikihangaika kupambana na janga la corona.

    Taarifa hiyo imesema nchi ambazo raia wake wamewekewa marufuku hiyo ni pamoja :

    Argentina na Milki za kiarabu, Ujerumani, Marekani, Indonesia, Ireland, Italia, Pakistan, Brazil, Ureno, Uingereza, Uturuki, Afrika Kusini, Sweden, Uswiss,Ufaransa, Lebanon, Misri, India na Japan.

    Marufuku hiyo itaanza kutekelezwa kuanzia saa tatu usiku (kwa saa za Saudi Arabia ) Jumatano, tarehe 3 Februari .

    "Aidha , marufuku hiyo inawahusu raia wanaopita katika mataifa hayo 20 ," yameripoti magazeti ya Saudi Arabia.

  2. IGP Sirro: Hakuna marufuku ya kukimbia siku za ibada

    IGP Sirro amesema kuwa taarifa ya mwanzo haikuleweka vizuri.
    Maelezo ya picha, IGP Sirro amesema kuwa taarifa ya mwanzo haikuleweka vizuri.

    Mkuu wa jeshi la polisi nchini Tanzania IGP Simon Sirro amefanunua juu ya marufuku kwa wakimbiaji wa mbio za pole pole (Jogging) iliyotolewa na Kamanda wa polisi kanda ya Dar es salaam, Lazarus Mambosasa.

    Aidha katika ufafanuzi huo Sirro amesema kuwa marufuku hiyo ya wakiambiaji inahusisha njia za karibu na maeneo ya ibada na wakati wa ibada.

    ‘’viongozi wa madhehebu wamekua wanalalamika wakati wa ibada, imekua tabu wakipita wanapigiwa kelele, maeneo mengine ni ruhsa, vi vizuri wasipite maeneo hayo, hasa wakati wa ibada. Tukisema wapite kimya kimya, watu wengine hawatopita kimya kimya, hivyo maeneo ya ibada wakati wa ibada’’anasema IGP Sirro

    Awali akizungumza na televisheni ya Taifa Kamanda wa kanda Maalum Lazarus Mambosasa alisema maandamano na mbio za pole pole (Jogging) katika baadhi ya njia jijini Dar es salaam hazituruhiswa siku za ibada kwa kunyimwa kibali kutokana na kuingilia shughuli za ibada.

    Aliongeza kuwa siku za ibada ni ijumaa, jumamosi na jumapili.

  3. Kampuni za Tanzania zashinda zabuni za mabilioni ya pesa za ujenzi wa mkongo wa taifa

      • Author, Aboubakar Famau
      • Nafasi, BBC News, Dar es Salaam
    Dkt Faustine Ndugulile ni Waziri wa Mawasiliano na teknolojia ya habari
    Maelezo ya picha, Dkt Faustine Ndugulile (Kushoto) Waziri wa Mawasiliano na teknolojia ya habari, amezitaka kampuni zikamilishe kazi wa kwa wakati uliopagwa

    Kampuni nne za kitanzania zimeshinda zabuni yenye thamani ya shilingi bilioni 7 nukta 5 kwa ajili ya ujenzi wa mkongo wa taifa pamoja na maboresho ya anwani ya makazi.

    Ujenzi huo wa mkongo wa taifa utakuwa ni wa kilomita 409 ambapo utafikisha mawasiliano katika nchi Jirani ya Msumbiji pamoja na kuunganisha mawasiliano katika mikoa mingine ya Tanzania ikiwemo Singida na Mbeya.

    Mikataba hiyo pia ni pamoja na maboresho ya anwani za makazi.

    Wakati huo huo, Waziri Ndugulile ametilia mkazo suala la ubora na kuzitaka kampuni hizo kukamilisha kazi kwa wakati uliopangwa.

    Akizungumza kwa niaba ya makampuni mengine yaliyosaini mikataba hiyo

    ameihakikishia serikali kwamba watakamilisha kazi hiyo kwa wakati na ufanisi.

    Hii ni mara ya kwanza kwa kampuni za ndani kushinda zabuni ya Ujenzi wa mkongo wa taifa.

    Tayari Tanzania imejenga wastani wa kilomita 7910 ya mkongo wa taifa kwa lengo la kurahisisha Mawasiliano na kufikia malengo ya uchumi wa kidigitali na biashara Mtandao.

  4. Watu 32 wathibitishwa kufariki kwenye ajali ya gari Uganda

      • Author, Isack Mumena
      • Nafasi, BBC Swahili Kampala

    Watu 32 wamethibitishwa kufariki kwenye ajali ya gari nchini Uganda iliyotokea usiku wa kuamukia leo katika wilaya ya Kasese nchini Uganda.

    Vifo hivyo vimetokea baada ya magari matano kugongana katika kijiji cha Kihongo kilichopo kwenye barabara kuu ya Hima –Rugendabara wilayani Kasese magharibi mwa Uganda.

    Miili ya marehemu 32 imepatikana na majeruhi watano wamepelekwa katika hospitali ya Kilembe.

    Katika taarifa iliyotolewa na shirika la Msalaba mwekundu nchini humo , timu yao ikishirikiana na jeshi la UPDF na Polisi ikiongozwa na Meja Charles Nzei wameweza kuwaokoa majeruhi na kupata miili ya waliofariki.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Sababu ya ajali hiyo imetajwa kuwa ni ufinyu wa barabara inayotengenezwa na kulikuwa giza kubwa na hivyo kusababisha Malori mawili kugongana mjini Kasese na kuanguka.

    Baada ya yaliangukakwa malori mawili ambayo tayari , gari lingine kutoka Budibugyo pia likaanguka kwenye katika eneo hilo hilo.

    Kwa pamoja magari 5 yakaanguka kwanye ajali iliyosababaisha vifo vya watu 32 na watano kujeruhiwa vibaya majira ya saa tatu za usiku kwa mujibu wa msemaji wa Red Cross Irene Nakasita.

    Kati ya magari hayo ,Lori dogo ya aina ya kenta lilikuwa limebeba jeneza na watu waliokuwa wakielekea kwenye mazishi wakitoka wilayani Budibugyo wakielekea Kata ya Maliba.

    Kwa mujibu wa takwimu za jeshi la polisi nchini Uganda karibu ajali za barabarani 20,000 hutokea kila mwaka nchini Uganda na kusababisha takribani vifo vya watu 2,000.

    Hii inaifanya Uganda kuwa miongoni mwa mataifa yenye kiwango cha juu cha ajali za barabarani.

  5. Maandamano na mazoezi ya riadha marufuku siku za ibada Tanzania

      • Author, Munira Hussein
      • Nafasi, BBC Africa
    Mbio

    Chanzo cha picha, Scolar Kisanga

    Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam nchini Tanzania Lazaro Mambosasa amesema kuanzia sasa ni marufuku watu kufanya maandamano na mbio za polepole ( jogging) siku za ibada na amesisitiza kuwa jeshi la polisi halitatoa vibali katika siku hizo.

    Mambosasa amesema kuandamana siku za ibada ni kuwachelewesha waumini kufika sehemu za ibada kwa wakati.

    “Siku za Ibada, haturuhusu zile njia zote kwa kutotoa kibali, kundi lolote haliruhusiwi kupita maeneo hayo , waumini Dar es salaam wanaenda na magari hivyo ukiuruhusu jogging barabarani au maandamano yoyote yale yanepelekea kufunga barabara, ibada zinakwenda na muda”

    Aidha ameongeza kuwa siku za ibada ni Ijumaa, Jumamosi na Jumapili.

    Miaka ya hivi karibuni, kumekua na muamko wa mazoezi kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam.

    Mazoezi ya mbio za Polepole ama maarufu jogging yamekua yakiandaliwa na mashirika mbalimbali kuhamasisha mazoezi lakini pia kama harambee za kuawasadia wahitaji katika maeneo tofauti.

    Mbio hizi mara nyinyi kufanyika mwishoni mwa juma ili kupata washiriki wengi ambao wanakua katika mapumziko ya kazi.

  6. Zuchu ndiye mwanamuziki wa kwanza wa kike Mashariki kupata watazamaji milioni 100 katika Youtube

    Zuchu

    Chanzo cha picha, Officialzuchu

    Mwanamuziki wa Tanzania Zuhura Othman , al maarufu Zuchu amekua mwanamuziki wa kwanza wa kike Afrika Mashariki anayeimba peke yake kupata jumla ya watazamaji milioni 100 kwenye mtandao wa Youtube.

    Mwanamuziki huyo kutoka kampuni ya Wasafi amepata kutokana na wimbo wake alioutoa hivi karibuni kwa jina ''sukari'' ulioikonga mioyo ya mashabiki na wapenzi wa muziki wake.

    Zuchu ameelezea furaha yake ya kupata ufuasi huo kupitia mtandao wa Instagram:

    Ruka Instagram ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa Instagram ujumbe

    Kampuni ya Wasafi pia imempongeza zake kwa Bi Zuchu kwa mafanikio yake:

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Kampuni ya Wasafi, ambayo pia ni nembo inamilikiwa na Mwanamuziki maarufu wa Bongo Flava, Naseeb Abdul al maarufu Diamond Platnamz.

  7. Bunge la DRC kumchagua Spika mpya

    Bunge la DRC

    Chanzo cha picha, MBELECHI MSOCHI

    Maelezo ya picha, Mwezi Disemba Bunge la DRC lilimg'oa madarakani Spika Jeanine Mabunda, ambaye ni mshirika wa Joseph Kabila

    Wabunge wa bunge dogo la DRC wanatarajiwa kumchagua Spika mpya leo, huku Rais Felix Tshisekedi akikusanya nguvu chini ya muungano wake mpya unaoitwa –Muungano mtakatifu.

    Hii inafuatia kuondolewa kwa Spika Jeanine Mabunda, ambaye ni mshirika wa rais wa zamani Joseph Kabila, ambaye aliondolewa kwa kura ya kutokuwa na imani naye mwezi Disemba kufuatia tuhuma za ufisadi.

    Jana zaidi ya maseneta 60 waliwasilisha ombi la kutimuliwa madarakani kwa Spika wa bunge la Seneti Alexis Thambwe Mwamba, kwa tuhuma za ubadhilifu wa mali ya umma.

    Mwamba, mbaye pia ni mshirika wa Bw Kabila, anashutumiwa kuchukua zaidi ya dola milioni 3 za kimareani kwa niaba ya Seneti. Amekana tuhuma hizo.

    Wiki iliyopita Waziri Mkuu Sylivestre Illunga alijiuzulu baada ya kura ya kutokuwa na imani naye kupigwa dhidi yake.

    Tshisekedi amekuwa akiwatimua washirika wa mtangulizi wake tangu alipovunja muungano mwezi Disemba mwaka jana kufuatia kuongezeka kwa tofauti kuhusiana na mageuzi ya usalama, mahakama, tume ya uchaguzi na mashirika mbali mbali ya taifa.

  8. BBC imebaini ushahidi wa ubakaji na mateso katika mahabusu za Waislam wa Uighur

    Mateso

    Chanzo cha picha, Google

    Wanawake ambao walisema wamekua wafungwa katika kambi kwa miezi kadhaa, wamedai kuwa walikua wakiteswa kwa nguvu za umeme.

    Pia wameelezea tukio la mamia ya wafungwa kulazimishwa kumtazama msichana akibakwa na maafisa wa usalama mbele yao.

    Katika taarifa, serikali ya China ilisema kuwa imejitolea kulinda haki za wanawake.

    Makundi ya kutetea haki za binadamu yanasema Waislamu wa Uighur wapatao 500,000 wanashikiliwa katika vituo vya mahabusu.

    China imekuwa ikikana mara kwa mara shutuma za mateso dhidi ya Waislamu, ikisema kuwa inawapatia mafunzo katika kambi ili waondokane na fikra za itikadi kali.

  9. Shinikizo la kumtimua Spika wa seneti laendelea DRC

    Rais Félix Tshisekedi (Kushoto) amekuwa akidhoofisha ushawishi wa mtangulizi wake Joseph Kabila

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Rais Félix Tshisekedi (Kushoto) amekuwa akidhoofisha ushawishi wa mtangulizi wake Joseph Kabila

    Seneta wa Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo amewasilisha ombi la kufukuzwa kwa Spika wa bunge la Seneti Alexis Thambwe Mwamba.

    Bw Thambwe Mwamba ni mshirika wa karibu wa rais wa zamani wa taifa hilo Joseph Kabila.

    Seneta Valentin Gerengo kutoka vuguvugu la ukombozi wa DRC -Liberation of Congo, aliwasilisha ombi hilo katika ofisi ya seneti .

    "Kwa mujibu wa kipegele nambari 27 cha katiba ya nchi hiyo, aya ya tano, kifungu cha 28 na aya ya 2 hadi ya 5 ya taratibu za utendaji wa seneti, tunawasilisha ombi hili ili kutaka kuondolewa kwa Spika wa Seneti ," alisema Seneta Gerengo katika barua ambayo alithibibitisha uhalali wake katika wavuti wa habari.

    Seneti inafanya kikao chake cha dharura Jumatano kujadili ajenda moja tu, iliyoitwa kuchunguza na kuidhinisha kusomwa kwa mara ya pili kwa muswada wa kuidhinisha biashara huria ya bara la Afrika.

  10. Hujambo, na karibu kwa matangazo yetu mubashara leo Jumatano tarehe 03.02.2021