Fahamu siri inayoendelea kumtajirisha bilionea nambari moja duniania duniani
Jeff Bezos tajiri mkubwa duniani anayesimamia kampuni ya kimataifa ya Amazon inayofanya vizuri.
Kampuni yake inakadiriwa kuwa na thamani ya takribani dola bilioni $171 sawa na (£137bn), na pia ameweza kutengeneza mabilioni ya pesa wakati wa janga la Covid-19 .
Lakini je, anazingatia nini katika kuhakikisha anaendelea kufanikiwa?
Fahamu siri inayomfanyatajiri mkubwa duniani kuendelea kutajirika
1. kila tatizo linaweza kutatuliwa kwa kufikiria na uwepo wa ukweli.
2. Kila wakati mteja ni mfalme.
3. Fikiria anachotaka mteja na namna ya kutimiza hitaji lake.
4. Kila siku chukulia kana kwamba ni siku ya kwanza ya biashara yako. Kuwa na hamu ya kutaka kuona unavumbua kitu cha kipekee hadi mafanikio yake.
5. Kuwa na moyo wa kutaka kujaribu kitu hata kama kutakuwa na hatari ya kupoteza.
6. Na hata usipofaulu, hautakuwa sawa na ambaye hajajaribu. Hivyobasi, pendelea kuwa mtu wa kudhubutu.
7. Hutawahi kujuta kwa kujaribu kitu fulani.
“Unapofikiria vitu ambavyo hujafanya ukiwa umetimiza miaka 80, mara nyingi ni vile ambavyo hukujaribu kabisa. Ni nadra sana kujuta kwasababu ya jambo ambalo ulijaribu kufanya lakini halikufanikiwa.”
8. Zungumza unachodhani ni sahihi.
9. Usiogope ushindani.
10. Angalia malengo ya muda mrefu.
Inasemekana kuwa tajiri huyu wa dunia Bezos, “yuko tayari kuchukua miaka 10 kufanya kitu kitakachomwezesha kupata peza miaka ijayo” na kusalia na lengo lake mradi linaonesha dalili ya kupiga hatua.
Soma zaidi kuhusu tajiri mkubwa duniani