Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

China 'kujenga' kambi za kijeshi Tanzania na Kenya

Tanzania na Kenya zimetajwa kuwa miongoni mwa nchi kadhaa za Afrika ambazo China inapanga kujenga kambi za kijeshi, kwa mujibu wa ripoti ya idara ya ulinzi ya Marekani.

Moja kwa moja

Ambia Hirsi

  1. Tunakamilisha matangazo yetu ya moja kwa moja kwa leo.

    Lakini tunakuacha na taarifa ya duka la urembo nchini Afrika Kusini kuvamiwa kwa kutoa tangazo la ‘kibaguzi'

    Hii ni baada ya waandamanaji kulalazimisha maduka kadhaa ya urembo yanayomilikiwa na kampuni ya Click kufungwa kufuatia tangazo la biashara lililotolewa na kampani hiyo ambalo wanadai kuwa na ujumbe wa kibaguzi.

    Tangazo hilo lilikuwa na picha inayolinganisha nywele ya mwafrika na mzungu ikiashiria kuwa nywele ya mwafrika imekauka na kuharibika ilihali ya mzungu ni laini, nyororo na ya kuvutia.

    Chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) kimetaja tangazo hilo kuwa la"kibaguzi" na la "kudhalilisha".

  2. Tanzania yapinga madai ya kuhusika na mzozo wa Msumbiji

    Msemaji wa jeshi Luteni kanali Juma Sipe amesema kwamba habari hizo ni uvumi uliozagaa katika vyombo vya habari na kwamba hazina ukweli wowote.

  3. Mkurugenzi wa mashtaka Tanzania aidhinisha kushtakiwa kwa Saed Kubenea

    Jeshi la polisi Tanzania, limemkamata mbunge wa zamani wa upinzani Saed Kubenea katika mpaka wa Tanzania na Kenya, eneo la Namanga akielekea Arusha mjini.

    Baada ya upekuzi, bwana Kubenea alikutwa na kiasi cha Dola za 8000 za Marekani tiketi ya basi ya kutoka jijini Nairobi kwenda Namanga, Risiti ya malipo ya hoteli iliyopo jijini Nairobi yenye jina lake kama mgeni aliyelala hotelini hapo kuanzia tarehe 3 mpaka tarehe 5 mwezi Septemba na pasi yake ya kusafiria.

    Taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Mkurugenzi wa mashtaka Biswalo Eutropius Kachele imesema kuwa mara baada ya kukamatwa Kubenea alieleza kuwa alifika mkoani Arusha tarehe 2 akitokea Dar esSalaam na kulala katika hoteli iliyo Arusha mjini pia tarehe 3 mwezi Sptemba alikwenda kulala kwa kaka yake na tarehe 4 alikwenda Namanga na kupokea fedha taslimu zilizotajwa awali kutoka kwa raia wa Kenya.

    Hivyo baada ya kujiridhisha na uwepo wa ushahidi wa kutosha dhidi yake, sambamba na misingi ya kikatiba inayotoa muongozo kwa Mkurugenzi wa mashtaka, Mkurugenzi wa Mashtaka aimeidhinisha mashtaka yafuatayo.

    Kuingia nchini Tanzania kinyume na sheria ya uhamiaji sura ya 54,marejeo ya mwaka 2016 na

    Kuingiza nchini fedha za kigeni bila kutoa tamko kinyume na kanuni za Utoaji Tamko la fedha za mpakani za mwaka 2016.

  4. Afrika Kusini yashuka kwenye orodha ya Covid-19 duniani

    Afrika Kusini imeshuka hadi nambari nambari saba katika orodha ya nchi zilizo na idadi ya juu ya watu walioambukizwa virusi vya corona duniani huku viwango vya maambukizi mapya vikiendelea kushuka, data rasmi zinaonesha.

    Marekani, India, Brazil, Urusi, Peru na Columbia ndio nchi sita zinazoongoza duniani kwa kuwa na viwango vya juu vya maambukizi.

    Afrika Kusini ilitangaza kuwa na visa vipya 1,633siku ya Jumapili na kufikisha 638,517 jumla ya watu walioambukizwa virusi hivyo. Idadi ya watu waliofariki kutokana na janga la corona ni 14,889.

    Kiwango hicho kilishuka baada ya kupitwa na Peru, ambayo inapakana na Colombia, mapema wiki iliyopita. Perukufikia sasa ina watu 676,848 waliothibitishwa kuwa na virus vya corona.

    Waziri wa Afya wa Afrika Kusini Zweli Mkhize amesema japo viwango vya vya maambukizi vinashuka, nchi hiyo bado inahofia huenda ikapanda.

  5. Keki ya kuadhimisha mwaka mmoja ya Air Uganda yazua gumzo

    Shirika la ndege la Uganda limeadhimisha mwaka wake wa kwanza kwa kukata keki ambayo umbo lake limezua gumzo katika mitandao ya kijamii.

    Kampuni iliyooka keki hiyo ilibezwa mitandaoni wikendi iliyopita. Kampuni hiyo imekiri kuwa haikutoa vyema muundo wa ndege ya shirika la ndege la Uganda na kuanzisha shindano la kuoka keki tena hiyo.

    Katika taarifa yake kampuni ya Britam ambayo inafadhili shindano hilo ilisema:

    ‘’Tulijaribu kutengeza keki ya muundo wa ndege lakini kama mlivyona kwenye mitandao ya kijamii hatukufanikiwa’’

    Wito sasa umetolewa kwa waokaji keki wakubwa kwa wadogo kushiriki katika shindano hilo ambalo mshindi atafadhiliwa na kutengeza keki na kupewa nafasi ya kuiwasilishwa binafsi kwa shirika la ndege la Uganda.

  6. Barbara Gonzalez mkurugenzi mpya wa Simba

      • Author, Eagan Salla
      • Nafasi, BBC Swahili, Dar es Salaam

    Hatua ya Klabu ya Simba nchini Tanzania kumtangaza Barbara Gonzalez kuwa mkurugenzi mkuu wake mpya na kumfanya kuwa mwanamke wa kwanza kushika nafasi hiyo kwenye soka la Tanzania imeibua hisia mseto.

    Baadhi ya mashabiki na wanachama wa klabu hiyo wanatilia shaka utendaji wake wengine wakihoji namna alivyopatikana.

    Uteuzi wake umekuja baada ya aliekuwa mkurugenzi mkuu wa klabu hiyo Senzo Mbatha kujiuzulu na kuagana na mahasimu wao Dar young African (Yanga)

    Kupitia mtandao wake wa twitter, mmoja wa wanachama wa klabu hiyo yenye makao yake makuu mtaa wa Msimbazi Kariakoo jijini Dar es salaam, Dr Khamisi Kigwangala amehoji ueledi wa mtendaji huyo mkuu mpya na mchakato uliopitiwa kumpata.

    Kupitia taarifa yao rasmi wekundu wa msimbazi wakijibu tuhuma hizo wameelezea uwezo na weledi alionao mtendaji huyo mpya, wakieleza amekuwa akifanya kazi nyuma ya pazia na kutoa mchango mkubwa uliochangia kuundwa kwa mfumo wa sheria utakaongoza mabadiliko na uendeshaji mpya wa klabu.

    Bi Gonzalez, amesomea shahada ya sanaa katika uchumi na sayansi ya siasa nchini Marekani Mwaka 2016. Barbara alianza kufanya kazi Melt Mohammed Enterprises Limited kama msamiamizi mkuu wa mfuko wa Mo dewji lakini pia amekuwa msaidizi mkuu wa Rais wa makampuni ya MELT.

  7. Waziri wa Uganda kushitakiwa kufuatia kisa cha ufyatulianaji risasi

    Waziri wa leba wa Uganda, Mwesigwa Rukutana, anatarajiwa kufikishwa mahakamani Jumatatu baada ya kukamatwa kufuatia kisa cha ufyatulianaji risasi.

    Waziri huyo anadaiwa kumpiga risasi mfuasi wa mpinzani wake baada ya kushindwa katika uchaguzi wa chama tawala cha National Resistance Movement (NRM).

    Mfuasi mmoja alijeruhiwa vibaya na wengine wawili kupata majeraha madogo, kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari nchini humo.

    Bwana Rukutana amekanusha madai ya kuwafyatulia risasi wafuasi wa mpinzani wake.

    Vyombo vya habari vimemnukuu mmoja wa watu walioshuhudia kisa hicho akisema waziri alichukua bunduki kutoka kwa mmoja wa walinzi na kuanza kuwapiga risasi wafuasi wa mpinzani wake.

    Waziri huyo pamoja na walinzi wake watatu walitiwa nguvuni.

    Watashitakiwa kwa jaribio la mauaj, kwa mujibu wa naibu wa msemaji wa polisi Polly Namaye.

    Video inayomuonesha waziri akitumia bunduki iliwekwa mtandaoni:

  8. China 'kujenga' kambi za kijeshi Tanzania na Kenya

    China inafikiria kujenga kambi za kijeshi katika nchi nne za Afrika, kwa mujibu wa ripoti ya idara ya ulinzi ya Marekani.

    Tanzania, Kenya, Ushelisheli na Angola zimetajwa kuwa miongoni mwa nchi kadhaa ambazo China inapania kujenga kambi za kijeshi.

    Serikali za nchi hizo nne za Afrika zilizotajwa na Marekani hazijatoa tamko lolote kuhusiana na suala hilo.

    Ripoti hiyo iliyochapishwa wiki iliyopita imeangaziwa sana na vyombo vya habari wikendi iliopita, huku baadhi ya nchi ambazo kambi hizo zitajengwa zikikanusha kufanya mazungumzo na China.

    "Kando na kambi yake ya sasa nchini Djibouti, Jamhuri ya watu wa China ina mpango wa kuongeza kambi zake za kijeshi ughaibuni kusaidia vikosi vya majini, angani na ardhini," sehemu ya ripoti hiyo ilisema.

    Pia imeongeza kuwa China huenda ameamua sehemu itakapojenga vituo vyake vya kijeshi nchini Myanmar, Thailand, Singapore, Indonesia, Pakistan, Sri Lanka, Umoja wa Falme za Kiarabu,(UAE), Kenya, Ushelisheli, Tanzania, Angola, na Tajikistan.

  9. Tawala hasimu za Libya zakutana Morocco kwa mazungumzo

    Wajumbe wa tawala mbili hasimu nchini Libya wamekutana kwa mazungumzo nchini Morocco wiki mbili baada ya pande hiz mbili kusitisha mapigano.

    Wajumbe watano kutoka kila upande ikiwa ni pamoja na ule wa serikali inayotambuliwa na Umoja wa Mataifa iliyo na makao yake Tripoli na bunge hasimu lililo na makao yake katika mji wa mashariki wa Tobruk.

    Akifungua rasmi mkutano huo katika mji wa Bouznika Waziri wa mambo ya nje wa Morocco Nasser Bourita, amesema Morocco haina ajenda yoyote bali inataka uwapatia nafasi viongozi wa Libya kadili masuala yanayowagawanya.

    Morocco ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa mwaka2015 ambao ulichangia kubuniwa kwa serikali inayotambuliwa na Umoja wa Mataifa mjini Tripoli.