Waziri Mkuu wa Qatar anatarajiwa kuzuru Iran hii leo
Moja kwa moja
Na Beldeen Waliaula
Raia 173 wa Tanzania warejea kutoka Afrika Kusini
Chanzo cha picha, Getty Images
Takriban raia 173 wa Tanzania wamerejea nyumbani kutoka Afrika Kusini.
Serikali ya Tanzania kupitia ubalozi wake ulikuwa umetoa mwito wa wale wanaotaka kurejea kwa hiari kufika katika ubalozi wa taifa hilo ulioko mjini Pretoria Afrika Kusini.
Kundi la kwanza liliwasili usiku wa kuamkia leo, huku kundi lingine likitarajiwa kuwasili hii leo.
Zoezi hilo litawahusisha Watanzania wasio na pasipoti, ambao muda wa kutumika wa pasipoti zao umekwisha au kupotea, pamoja na watoto waliozaliwa Afrika Kusini.
Watanzania wasio na pasipoti watapewa hati za dharura za kusafiria ili kuwawezesha kurejea nchini humo.
Uamuzi wa kuwarejesha Watanzania nchini unakuja wakati kumekuwa na maandamano ya kupinga wahamiaji nchini Afrika Kusini.
Mataifa kadhaa ya Afrika tayari yamewaondoa raia wao nchini humo.
Tunachokijua kufikia sasa kuhusu maporomoko ya ardhi nchini Nepal
Chanzo cha picha, reut
Maporomoko makubwa ya ardhi na
mafuriko ya ghafla yameshuhudiwa
katika mpaka wa Nepal na Tibet,na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali, miundombinu na kuwauwa watu.
Juhudi
za kuwatafuta manusura bado zinaendelea
Chanzo cha picha, Reuters
Nini kimesababisha maporomoko hayo ya ardhi?
Waziri wa Mambo ya Kigeni
wa Nepal amesema kuwa tetemeko la ardhi
liliripotiwa katika mpaka wa Tibet na Nepal muda mfupi kabla ya maporomoko hayo
ya ardhi kutokea,
akipendekeza kuwa huenda tetemeko hilo ndilo lililosababisha janga hilo.
Hata
hivyo, uchambuzi wa hivi karibuni wa Shirika la Jiolojia la Marekani (USGS)
unaonyesha kuwa hakukuwa na tetemeko la ardhi,
jambo ambalo limeibua maswali kuhusu chanzo halisi cha maporomoko hayo ya
ardhi.
Kuna uwezekano kuwa maji
kutokana na mvua au kuyeyuka kwa barafu huenda yalifanya ardhi au barafu kutokuwa
imara, na hivyo kusababisha mfululizo wa matukio hayo.
Mabadiliko
ya tabianchi yamekuwa yakichochea kuyeyuka
kwa barafu katika eneo la Hindu Kush Himalaya, lakini wanasayansi wanasema bado
ni mapema kubaini mchango wake katika tukio hili.
Kwa
sasa, wanasayansi wanajaribu kurejelea
matukio hayo ili kubaini kilichotokea
Chanzo cha picha, Reuters
Ni watu wangapi wamefariki na kupotea?
Idadi
ya watu waliofariki au kupotea bado inaendelea kuongezeka.
Polisi
nchini Nepal wanasema angalau watu 162 wamefariki. Kati ya waliokufa,
miili ya watu 64 ilipatikana katika maeneo ya chini ya mkondo wa maji katika
wilaya ya Chitwan, huku miili mingine 26 ikipatikana Nawalparasi Mashariki.
Idadi
ya watu waliopotea kufuatia janga hili katika kaunti ya Gyirong, Tibet, imeongezeka hadi 558.
Watalii waliopotea wanatoka nchi gani?
Watalii
kutoka sehemu mbalimbali duniani huitembelea Nepal kwa ajili ya kukwea milima yake na maeneo yake
matakatifu. Takwimu rasmi zinaonyesha kuwa angalau wageni 291
ni miongoni mwa watu waliopotea, wakiwemo:
India –142 wa India, Ukraine
–53, Malaysia
–50, Uingereza
–33, Canada –24, Marekani
–54
, Australia
–34
,
Idadi
ndogo ya wasafiri kutoka Korea Kusini, Afrika Kusini, Ureno na Uholanzi pia
ni miongoni mwa watu waliopotea.
Moto wa nyika wauwa watu 12 Algeria
Chanzo cha picha, Reuters
Wizara ya Mambo ya Ndani nchini Algeria, imetangaza kuwa watu 12 wamefariki kutokana na moto wa nyika unaoendelea
kuteketeza maeneo ya kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo.
Waziri
wa Mambo ya Ndani, Serikali za Mitaa na Uchukuzi, Said Saioud, amethibitisha vifo hivyo na kuongezea kuwa watu wengine 54 walipata
majeraha ya moto, huku sita kati yao wakiwa katika hali mbaya na wamelazwa
katika vyumba vya watu mahututi.
Mamlaka za Algeria zimeripoti visa 154 vya
moto kote nchini humo, huku wakiweza kudhibiti sehemu kubwa ya moto huo.
Moto wa nyika umetokea wakati mataifa ya Afrika Kaskazini
yanaendelea kukumbana na joto kali, haswa Tunisia na Algeria.
Marekani na UN zatoa msaada kwa waathiriwa wa mafuriko Nepal
Chanzo cha picha, EPA
Marekani
imeahidi kutoa msaada wa dola 500,000 ambazo zitatumika kugharamikia makazi ya muda, maji, huduma za usafi na
misaada mingine kwa jamii zilizoathiriwa na mafuriko.
“Marekani
inatuma salamu zake za rambirambi
kwa familia na jamaa wa
waliofariki katika mafuriko makubwa ya ghafla yaliyoikumba wilaya ya Rasuwa nchini
Nepal,” Idara ya Mambo ya Kigeni
ya Marekani ilisema katika taarifa.
Takriban raia 54 wa Marekani, wengi wao wakiwa watalii,
wameripotiwa kuwa miongoni mwa mamia ya watu waliopotea kufuatia mafuriko na
maporomoko ya ardhi.
Hayo yakijiri, Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesema “amehuzunishwa na mafuriko hayo makubwa”
ambayo yamesababisha vifo vya watu wengi, huku wengine wakiwa hawajulikani walipo nchini Nepal
na China.
“Nasimama
pamoja na wote walioathiriwa,” amesema kiongozi huyo.
Ameongezea kuwa timu za
Umoja wa Mataifa na washirika wake zinaandaa kusafirisha vifaa pamoja na kuwapeleka wahudumu wa dharura nchini
Nepal ili kuisadia kukabiliana na janga hilo.
Maelezo ya video, Picha za angani zaonyesha mafuriko makubwa katika mpaka wa Nepal na Tibet
Waokoaji wanakabiliwa na changamoto kufika katika maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko makubwa ya ghafla na maporomoko ya udongo nchini Nepal, ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 160.
Mamia ya watalii hawajulikani walipo, wakiwemo zaidi ya 100 kutoka India, 54 kutoka Marekani, 34 kutoka Australia na 33 kutoka Uingereza.
Maafisa pia wanasema zaidi ya watu 100 kutoka Nepal wenyewe hawajulikani walipo.
Eneo hilo ni maarufu kwa watalii wanaofanya matembezi milimani pamoja na mahujaji.
Wakati shughuli za uokoaji zikiendelea, wataalamu wanaonya kuwa vifusi vilivyoziba mto karibu na eneo la maafa vinaweza kusababisha mafuriko mengine.
Mamlaka zinaendelea na juhudi za kuwasaka na kuwaokoa watu waliokwama katika maeneo yaliyoathiriwa.
Iran yaishtumu Marekani kwa kujaribu kuzuia mazungumzo yao na Oman
Chanzo cha picha, Getty Images
Jeshi la Iran IRGC,
limeishtumu Marekani kwa kile wamekitaja ‘kujaribu kuzuia’ makubaliano kati ya
Iran na Oman, kuhusu usimamizi wa Mlango Bahari wa Hormuz.
Jeshi hilo limesema
wamefikia makubaliano na Oman, ya kugawana mapato watakayokusanya katika
usimamizi wao wa Pamoja wa Mlango wa Hormuz,ila Marekani inajaribu kuzuia
kukamilika kwa makubaliano hayo.
Tehran
na Muscat zimejadili kuanzishwa kwa njia nyingingine ya bahari na mfumo
utakaoendesha safari za meli katika Mlango wa Hormuz.
Aidha, Tehran imeonya kuwa njia hiyo ya bahari haitafunguliwa tena hadi Marekani
isitishe vita.
Mazungumzo kati ya Iran na Oman, yanajiri
baada ya Washington kutangaza vikwazo vipya vinavyolenga kuilemaza Iran kiuchumi.
Mafuriko Nepal na Tibet yaua zaidi ya 160, mamia ya watalii hawajulikani walipo
Chanzo cha picha, Reuters
Zaidi ya watu 160 wamefariki nchini Nepal, huku mamia ya watalii wakiwa hawajulikani walipo baada ya mafuriko makubwa ya ghafla na maporomoko ya udongo katika eneo la mpaka kati ya Nepal na Tibet.
Nchini China, idadi ya watu ambao hawajulikani walipo baada ya maporomoko ya udongo katika kaunti ya Gyirong, Tibet, imefikia 558, kwa mujibu wa shirika la utangazaji la serikali CCTV.
Kati yao, 260 ni raia wa kigeni. Idadi ya waliofariki imeendelea kuwa watatu.
Mpaka wa Gyirong ni njia kuu inayotumiwa na watalii na magari kusafiri kati ya China na Nepal.
Nepal awali ilisema watu 579 hawajulikani walipo, wakiwemo raia 466 wa kigeni. Haijafahamika mara moja iwapo baadhi ya watu hao wamehesabiwa mara mbili katika takwimu za nchi hizo mbili.
Jeshi la Nepal limetuma wanajeshi 2,000 kushiriki katika shughuli za utafutaji na uokoaji kwa njia ya ardhini na angani katika maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko.
Msemaji wa jeshi, Brigedia Jenerali Rajaram Basnet, ameiambia BBC kuwa wanajeshi hao wamejikita katika maeneo yaliyoathirika zaidi, yakiwemo wilaya za Rasuwa na Nuwakot.
Jeshi hadi sasa limefanikiwa kuwaokoa watu 97 waliokuwa wamekwama kwenye mafuriko. Watatu kati yao walikuwa wafanyakazi waliokwama katika handaki la mradi wa kuzalisha umeme wa maji wa Trishuli A.
Polisi na kikosi cha polisi wenye silaha cha Nepal pia vimepeleka maafisa katika maeneo yaliyoathiriwa kusaidia shughuli za utafutaji.
Awali mamlaka zilidhani kuwa huenda tetemeko la ardhi lilitangulia mafuriko hayo. Hata hivyo, Utafiti wa Jiolojia wa Marekani, USGS, sasa umesema nishati iliyosababisha mtikisiko huo ilitokana na maporomoko ya udongo, badala ya tetemeko la ardhi.
Waziri Mkuu wa Qatar kuzuru Tehran
Chanzo cha picha, Getty Images
Waziri
Mkuu wa Qatar anatarajiwa kuzuru
Tehran hii leo, katika
juhudi za kuanzisha tena
mazungumzo ya kidiplomasia, baada ya makubaliano ya kusitisha vita kati ya Iran na
Marekani kuvunjika.
Washington tayari imetangaza kuiwekea Iran
vikwazo vya kiuchumi pamoja na washirika wake wa karibu.
Qatar,
ambayo ni jirani wa Iran katika eneo la Ghuba
na pia mshirika wa Marekani, imekuwa mpatanishi wa siri kati ya pande hizo mbili zinazozozana, na ilichangia pakubwa katika kufanikisha makubaliano
ya kusitisha mapigano yaliyoafikiwa mwezi Juni.
Ziara
ya
Waziri Mkuu wa Qatar, Mohammed bin Abdulrahman bin Jassim bin Jaber Al Thani, inafanyika wakati vita kati ya Iran na Marekani vinaingia mwezi wake wa sita huku kukiwa hakuna
dalili ya mafanikio yoyote ya kidiplomasia.
Marekani na Iran bado zinatofautiana
kuhusu Mlango Bahari wa Hormuz ambayo ni njia muhimu ya usafirishaji mafuta
duniani.