Rais Zelensky ajadili mazungumzo ya amani na Trump

Chanzo cha picha, Reuters
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema siku ya Jumapili kwamba amezungumza na Rais wa Marekani Donald Trump na kujadili juhudi za kufikia mwisho wa vita vya zaidi ya miaka minne , kabla ya mkutano wa G7 nchini Ufaransa wiki hii.
Zelensky, akiandika kwenye Telegram, alisema alikuwa amemtakia Trump siku njema ya kuzaliwa ya 80 na akamshukuru kwa msaada uliotolewa na Washington katika kipindi chote cha mzozo.
"Nilimtakia Rais Trump mafanikio mema, kwanza kabisa katika juhudi zake za kukomesha vita vya Urusi dhidi ya Ukraine," Zelensky alisema.
Akizungumza baadaye katika hotuba yake kwa njia ya video iliyotolewa usiku, Zelensky alisema yeye na Trump wamekubaliana kukutana wakati wa mikutano huko Evian-les-Bains.
Alisema ni muhimu kuhakikisha Marekani inaunga mkono juhudi za Ukraine za kupata amani, pamoja na washirika wa Ukraine wa Ulaya.
"Hili ndilo jambo muhimu zaidi tunalotaka sote, na ni muhimu kwamba jamii ya Marekani iunge mkono kikamilifu hamu yetu ya Waukraine, hamu ya kupata amani," alisema.
Mazungumzo yanayosimamiwa na Marekani yanayolenga kukomesha vita yamekwama huku Washington ikiendelea kutoa kipaumbele kwa mzozo nchini Iran.
Hata hivyo, Zelensky amesema katika wiki za hivi karibuni mabadiliko ya kasi katika vitani kwa upande wa Ukraine yamefungua fursa ya kufikia makubaliano ya amani.
Soma zaidi:




