Moja kwa moja, Marekani yaishambulia Iran baada ya vikosi vyake kushambulia meli ya mizigo

Kamandi Kuu ya Marekani au Centcom ilishambulia vituo vya kuhifadhia makombora na ndege zisizo na rubani siku ya Ijumaa.

Skip Video and continue reading
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Idadi ya waliofariki katika tetemeko la ardhi Venezuela yafikia 920

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Zaidi ya watu 900 wamethibitishwa kufariki dunia na wengine 3,360 kujeruhiwa katika tetemeko la ardhi la Venezuela, kulingana na serikali, huku waokoaji wakiendelea kuwatafuta manusura wa mkasa huo.

    Waliojeruhiwa wanatibiwa katika vituo vya matibabu vya muda baada ya makumi ya majengo kaskazini mwa nchi hiyo kuharibiwa na matetemeko hayo mawili, ukiwemo mji mkuu Caracas.

    Afisa mkuu wa serikali alisema mamia ya waokoaji wa kimataifa wamewasili nchini, na wengine zaidi wako njiani.

    Matetemeko mawili makubwa ya ardhi yaliitikisa Venezuela ndani ya sekunde moja baada ya nyingine Jumatano. Tetemeko la pili lililokuwa na ukubwa wa 7.5. lilikuwa mojawapo ya mitetemeko makubwa zaidi kuwahi kuikumba nchi hiyo katika karne moja.

    Eneo la La Guaira, kaskazini mwa mji mkuu wa Caracas limeathirika zaidi, maafisa wanasema.

    Watu wengi hawajulikani walipo huku maafisa wakihofia huenda idadi ya vifo ikaongezeka ingawa juhudi za uokoaji bado ziendelea.

    Maelezo zaidi:

  2. Marekani yaishambulia Iran baada ya vikosi vyake kushambulia meli ya mizigo

    ,

    Chanzo cha picha, Reuters

    Jeshi la Marekani limefanya mashambulizi katika maeneo maalum nchini Iran baada ya Rais Donald Trump kuishutumu Iran kwa "ukiukaji wa kijinga" wa makubaliano yake ya kusitisha mapigano kufuatia shambulio dhidi ya meli ya mizigo katika Mlango wa bahari wa Hormuz.

    Kamandi Kuu ya Marekani au Centcom ilisema ilishambulia vituo vya kuhifadhia makombora na ndege zisizo na rubani na sehemu za rada za pwani siku ya Ijumaa.

    Ilisema hatua hiyo ilikuwa kujibu shambulio la ndege isiyo na rubani dhidi ya meli ya mizigo siku ya Alhamisi, tukio ambalo lilisimamisha mpango wa kuwahamisha maelfu ya mabaharia waliokwama katika eneo hilo.

    Tehran ilisema meli hiyo ya mizigo ilishambuliwa kwa sababu ilikuwa ikitumia njia ambayo ahaijaidhinishwa kupita kwenye maji ya Ghuba.

    Centcom - ilielezea mashambulio hayo kama "jibu kubwa" la kulipiza kisasi shambulio la ndege zisizo na rubani za Iran.

    "Uchokozi usio na msingi dhidi ya meli za kibiashara uliofanywa na vikosi vya Iran ulikiuka wazi makubaliano ya usitishaji mapigano," ilisema katika taarifa.

    Centcom inasema jeshi la Marekani "litaendelea kutoa uratibu wa njia salama na usaidizi kwa meli za kibiashara zinazopita kwenye mlango wa bahari wa Hormuz".

    Hata hivyo Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) lililaumu "serikali ya Marekani kwa kukiuka mkataba".

    Katika taarifa yake IRGC ilisemaMarekani ilifanya mashambulizi ya anga katika ufuo wa Iran "kwa visingizio mbalimbali vya meli inayokiuka utaratibu wa usafiri katika Mlango wa bahari wa Hormuz".

    IRGC ilisema jeshi lake la majini lililipiza kisasi kwa kushambulia ngome kadhaa za kijeshi za Marekani katika eneo hilo, bila kutoa maelezo zaidi. BBC imewasiliana na Pentagon kuthibitisha hilo.

    "Wakiendelea kufanya uchokozi majibu yetu yatakuwa makubwa zaidi kuliko haya," IRGC iliongeza.

    Tehran ilifunga mkondo huo baada ya mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran kuanza mwishoni mwa mwezi Februari.

    Soma zaidi:

  3. Karibu kwa matangazo ya moja kwa moja