Raia 13 wa Tunusia hawajulikani walipo baada ya boti lao kuzama bahari ya Mediterenia

Chanzo cha picha, Getty Images
Takriban raia 13 wa Tunisia, hawajulikani walipo baada ya boti iliyokuwa imebeba wahamiaji kuzama katika pwani ya Tunisia ikiwa inaelekea Italia, huku watu wawili wakiokolewa.
Akizungumza na shirika la habari la Reuters, Mostafa Abdelkebir, mkuu wa shirika la Tunisian Observatory for Human Rights, alisema boti hiyo iliondoka mapema siku ya Alhamisi.
Mmoja wa manusura hao wawili aliwaambia waokoaji kuwa walikuwa wamekwama baharini kwa saa kadhaa kabla ya chombo chao kupinduka.
Tunisia ni mojawapo ya maeneo makuu yanayotumiwa na wahamiaji wanaovuka Bahari ya Mediterania, lakini safari hizo zimepungua kwa kiasi kikubwa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kutokana na operesheni kali dhidi ya uhamiaji na kuimarishwa kwa usalama wa baharini.
Njia ya katikati ya Bahari ya Mediterania ni mojawapo ya njia hatari zaidi za uhamiaji duniani, inayotumiwa na wahamiaji kutoka Afrika na Mashariki ya Kati wanaotaka kufika Ulaya, mara nyingi wakitumia boti zisizo salama kwa safari za baharini.
Soma pia:


