Nairobi: Kilimo cha mjini kilichobuniwa kukabiliana na gharama ya juu ya maisha

Maelezo ya video, Nairobi: Kilimo cha mjini kilichobuniwa kukabiliana na gharama ya juu ya maisha
Iliyochapishwa

Kilimo cha mjini katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi ni njia mojawapo inayotumiwa na baadhi ya vijana kukabiliana na kupanda kwa gharama za Maisha.

Kwa kawaida kilimo hufanyika zaidi vijijini. Janga la corona limelazimisha baadhi ya watu kufikiria jinsi ya kujipatia mbogamboga, lakini pia hata kuuza.Mwandishi wa BBC Salim Kikeke amezungumza na mkulima mmoja wa mjini katika eneo la Kitengela.