Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Shimo la ajabu la Chile lawashangaza wengi
Iliyochapishwa
Maafisa nchini Chile wanachunguza shimo la ajabu linaloendea kuongezeka kina lililojitokeza wikendi katika eneo la mgodi kaskazini mwa nchi hiyo.
Picha za droni zinaonyesha shimo kubwa kwenye ardhi ya mgodi wa machimbo ya madini unaoendeshwa na kampuni ya Canada - Lundin Mining.
Taasisi ya kitaifa ya huduma za Giolojia na machimbo, Sernageomin, imewatuma wataalamu kwenye eneo hilo, ambalo lipo takriban maili 413 (665km) kaskazini mwa mji mkuu, Santiago.