Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tazama Chui akiingia darasani na kumshambulia mwanafunzi India
Chui mmoja alikamatwa katika mji wa kaskazini wa India Aligarh baada ya kuingia katika shule moja na kumshambulia mwanafunzi.
Mwanafunzi huyo , ambaye alipata majeraha madogo alisema kwamba alitoroka katika darasa hilo baada ya kumuona mnayama huyo akiwa amejificha.
Chui huyo mwenye umri wa miaka mitano baadaye alitulizwa na kukamatwa baada ya juhudi za saa kumi na moja.
Maafisa wanasema kwamba Chui huyo kutoka msitu jirani huenda alipotea njia na kuingia katika shule hiyo .
Mizozo kati ya chui na binadamu huwa jambo la kawaida nchini India huku Chui hao wakilazimika kutafuta chakula katika vijiji na miji.