Jiwe kubwa la moto kutoka angani lililoangamiza mji mzima

Chanzo cha picha, Allen West and Jennifer Rice, CC BY-NDBBC
Siku moja miaka 3,600 hivi iliyopita, wakazi wa jiji la kale la Mashariki ya Kati ambalo sasa linaitwa Tall el-Hammam walifanya shughuli zao za kila siku bila kujua kwamba jiwe la angani la moto lisiloonekana lilikuwa likiwakaribia kwa mwendo wa takriban kilomita 61,000 kwa saa.
Likiwa angani, jiwe lililipuka kwa moto mkubwa umbali wa kilomita 4 kutoka ardhini.
Mlipuko huo ulikuwa na nguvu mara 1,000 zaidi ya bomu la atomiki la Hiroshima.
Wakazi wa jiji walioshtuka waliomtazama walipofushwa mara moja. Joto lilipanda kwa kasi zaidi ya Fahrenheit 3,600 (nyuzi joto 2,000 ). Nguo na kuni ziliwaka moto mara moja. Mapanga, mikuki na vyombo vya udongo vilianza kuyeyuka.
Mara, jiji zima lilishika moto.
Sekunde chache baadaye, wimbi kubwa la tetemeko la ardhi lilitikisa jiji hilo. Ikienda kwa kasi ya kilomita 1,200 kwa saa, ilikuwa na nguvu zaidi kuliko kimbunga kibaya zaidi kuwahi kurekodiwa.
Upepo mbaya ulivuma kwenye mji huo, ukabomoa majengo yote. Ulirarua mita 12 za jumba la orofa nne na kurusha vifusi vilivyoporomoka kwenye bonde.
Hakuna hata mmoja wa watu 8,000 au wanyama na mji uliosalia: miili yao iligawanyika vipande vipande na mifupa yao ililipuka na kuwa vipande.
Takribani dakika moja baadaye, kilomita 22 magharibi mwa Tall el-Hammam, pepo za mlipuko zilifika kwenye jiji la kibiblia la Yeriko. Kuta zake zilianguka na jiji likateketea kabisa.
Yote inaonekana kama kilele cha filamu ya maafa ya Hollywood. Tunajuaje kwamba haya yote yalitokea mahali pale karibu na Bahari ya Chumvi huko Yordani milenia kadhaa zilizopita?
Kupata majibu kulihitaji takriban miaka 15 ya uchimbaji mgumu wa mamia ya watu.
Pia ilihusisha uchambuzi wa kina wa nyenzo zilizochimbwa na wanasayansi zaidi ya dazeni mbili katika majimbo 10 ya Marekani, pamoja na Canada na Jamhuri ya Czech.
Hivi ndivyo tunavyojenga taswira hii ya uharibifu siku za nyuma.
Wakati kundi letu hatimaye lilipochapisha ushahidi hivi majuzi katika Ripoti za Kisayansi, waandishi-wenza 21 walijumuisha wanaakiolojia, wanajioloji, wataalamu wa madini, wataalamu wa paleobotanists, sedimentologists, wataalam wa athari za ulimwengu, na madaktari. Hivi ndivyo tunavyojenga taswira hii ya uharibifu uliofanyika siku za nyuma.
Dhoruba kali ya moto
Miaka iliyopita, wakati wanaakiolojia walipotazama uchimbaji wa jiji lililoharibiwa, waliweza kuona blanketi jeusi, lililohariika lenye unene wa takribani mita 1.5 lililogeuka makaa ya mawe, majivu na udongo na vyombo vya udongo vilivyoyeyushwa.
Ilikuwa dhahiri kwamba dhoruba kali ya moto ilikuwa imeharibu jiji hili muda mrefu uliopita. ilipewa jina la safu iliyoharibiwa.

Chanzo cha picha, Phil Silvia, CC BY-ND
Hakuna aliyekuwa na uhakika ni nini hasa kilitokea, lakini tabaka hilo halikusababishwa na volkano, tetemeko la ardhi, au vita. Hakuna kati ya hayo yenye uwezo wa kuyeyusha chuma, adobe na kauri.
Ili kujua ni nini kilichokuwa kimetokea, kikundi chetu kilitumia "Kikokotoo cha Athari za Mtandaoni" kutazama hali zinazolingana na ushahidi.
Chombo hiki kimeundwa na wataalamu wanaotazama athari, huruhusu watafiti kukadiria maelezo mengi ya tukio la athari za ulimwengu, kulingana na matukio mengine ya athari inayojulikana na milipuko ya nyuklia.
Inaonekana chanzo huko Tall el-Hammam ilikuwa asteroid ndogo sawa na ile iliyoangusha miti milioni 80 huko Tunguska, Urusi mnamo 1908. Ingekuwa toleo ndogo zaidi la mwamba mkubwa wa kilomita upana ambao ulifukuza dinosaria. Hadi viumbe hao kutoweka miaka milioni 65 iliyopita.
Tulikuwa na sababu inayowezekana. Sasa tulihitaji uthibitisho wa kile kilichotokea siku hiyo huko Tall el-Hammam.
Kupatikana kwa"almasi" duniani
Uchunguzi wetu ulibaini aina mbalimbali za ushahidi.
Kwenye eneo hilo kuna chembechembe za mchanga zilizopasuka vizuri zinazoitwa quartz iliyoathiriwa ambayo hutengeneza pauni 725,000 kwa kila inchi ya mraba ya shinikizo (gigapascals 5); fikiria vifaru sita vya kijeshi vya tani 68 vya Abrams vilivyorundikwa.

Chanzo cha picha, Allen West, CC BY-ND
Tabaka iliyoharibiwa pia ina almasi ndogo ambazo, kama jina linavyopendekeza, ni ngumu kama almasi. Kila moja ni ndogo kuliko muonekano wa virusi vya mafua.
Inaonekana kwamba mbao na mimea katika eneo hilo viligeuzwa papo hapo kuwa na umbo kama almasi na shinikizo la juu na halijoto ya moto.
Majaribio ya maabara yalionesha kuwa vyungu vya udongo na tofali za matope katika Tall el-Hammam viliyeyushwa kwenye halijoto ya zaidi ya 1,500 ° C. Huo ni moto wa kutosha kuyeyusha gari kwa dakika chache.
Kwa pamoja, uthibitisho huu wote unaonesha kwamba halijoto katika jiji ilipanda zaidi ya ile ya volkano, vita, na moto wa kawaida.
Mchakato huo wa asili uliacha mshtuko mkubwa kwa ulimwengu.
Ushahidi kama huo unapatikana katika tovuti za athari zinazojulikana, kama vile Tunguska na kreta ya Chicxulub, iliyoundwa na asteroidi iliyosababisha dinosaria kutoweka.
Kilichosalia ni kwa nini jiji na makazi zaidi ya 100 katika maeneo mengine yaliachwa kwa karne kadhaa baada ya uharibifu huu.
Huenda viwango vya juu vya chumvi vilivyowekwa wakati wa tukio la athari vilifanya ukulima kutowezekana.
Bado hatuna uhakika, lakini tunaamini kuwa mlipuko huo unaweza kuwa ulitoa mvuke au kumwaga viwango vya sumu vya maji ya chumvi kutoka Bahari ya Chumvi katika bonde lote.
Bila mazao, hakuna mtu ambaye angeweza kuishi huko kwa miaka 600 hivi, hadi mvua kidogo katika hali ya hewa hii ya jangwa ilipopoza chumvi kutoka mashambani.
Je kulikuwa na mashuhuda walionusurika na mlipuko?
Ufafanuzi wa mdomo kuhusu uharibifu wa jiji unaweza kuwa ulipitishwa kwa vizazi hadi kurekodiwa kama hadithi ya Biblia ya Sodoma.
Biblia inaeleza uharibifu wa kituo cha mijini karibu na Bahari ya Chumvi: mawe na moto vilianguka kutoka mbinguni, zaidi ya jiji moja liliharibiwa, moshi mzito ukapanda, na wakazi wa jiji waliangamia.
Je, huu unaweza kuwa ushahidi wa mashahidi wa kale?
Ikiwa ndivyo, uharibifu wa Tall el-Hammam unaweza kuwa uharibifu wa pili wa zamani zaidi wa makazi ya binadamu kwa tukio la athari za ulimwengu, baada ya kijiji cha Abu Hureyra nchini Syria miaka 12,800 iliyopita.
Muhimu zaidi, inaweza kuwa rekodi ya kwanza iliyoandikwa ya tukio hilo la kutisha.
Kinachotisha ni kwamba haitakuwa mara ya mwisho kwa mji wa kibinadamu kukabiliana na hatima hii.

Chanzo cha picha, NASA / JPL-CALTECH
Milipuko ya anga ya ukubwa wa Tunguska, kama vile ule uliotokea Tall el-Hammam, inaweza kuharibu miji na maeneo yote, na kusababisha hatari kubwa leo.
Kufikia Septemba 2021, kuna zaidi ya asteroidi 26,000 zinazojulikana na mamia ya vimondo karibu na Dunia. Kimoja kinaweza kuanguka kwenye sayari bila shaka.
Mamilioni zaidi bado hayajatambuliwa. Isipokuwa darubini za ardhini au zinazozunguka zitambue vitu hivi, ulimwengu unaweza usiwe na onyo lolote, kama ilivyokuwa kwa watu wa Tall el-Hammam.















