Tazama jinsi dhoruba ya mchanga ‘ilivyomeza’ jiji kaskazini magharibi mwa China

Iliyochapishwa

Dhoruba ya mchanga iliyoinuka hadi urefu wa mita 100 (330ft) imeuacha mji mmoja kaskazini magharibi mwa China ukifunikwa na vumbi.

Video za Dunhuang zinaonyesha ukuta wa mchanga unaosakama polepole majengo na barabara katika mji huo .

Jiji hilo liko pembezoni mwa Jangwa la Gobi, ambalo linajulikana kwa hali kali ya hewa.