Zanzibar:“Baba aliniambia nilale chini kisha akaniingilia, mama akasema ninyamaze'
Iliyochapishwa
Kesi za udhalilishaji visiwani Zanzibar ni suala linalopigiwa kelele na viongozi wa kada mbalimbali.
Kwa mwaka jana pekee kesi zaidi ya 600 za udhalilishaji ikiwemo kubakwa na kulawitiwa zimefunguliwa katika vituo vya polisi visiwani Zanzibar huku ikiaminika kuna maelfu ya vitendo hivyo vinafanyika na kumalizika nyumbani bila kufika polisi.
Waandishi wa BBC Humphery Mgonja na Munira Hussein wamefuatilia kwa kina matukio ya udhalilishaji hasa kwa watoto visiwani humo na kuandaa ripoti maalum.