Dimpho Mabuya: 'Nanyanyua uzani nikifeli mtihani'
Iliyochapishwa
Soweto, viungani mwa Johannesburg, ni nyumbani kwa wanasoka na wanandondi wengi.
Lakini mtaa huo unatarajia kujipatia umaarufu katika mchezo mwingine - Olimpiki ya unyanyuaji uzani.
BBC Afrika ilitembelea eneo la mazoezi ya mchezo huo kwa kizazi kipya cha mabingwa Afrika Kusini - kufahamu kwanini mchezo huu umekuwa maarufu miongoni mwa wasichana.