Wasanii waonywa dhidi ya matumizi mabaya ya lugha katika kazi zao

Iliyochapishwa

Baraza la Kiswahili Tanzania limewataka wasanii nchini Tanzania kuepuka matumizi ya lugha chafu katika utekelezaji wa majukumu yao.

Sigala amesema watakuwa wakifanya kazi hiyo kwa kuandika barua na kuipeleka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) ambalo jukumu lake itakuwa kutoa adhabu ikiwemo kuifungia kazi husika.

Oni Sigalla ni Mhariri Mwandamizi wa Baraza hilo amezungumza na Regina Mziwanda kuhusu hatua hiyo.