Fahamu jinsi ndege kwa jina Tai wenye ndevu walivyo katika hatari ya kuangamia Afrika

Iliyochapishwa

Kati ya tai 11 wanaopatikana barani Afrika , saba wapo katika hatari ya kuangamia . Nchini Kenya spishi moja – ya tai wenye ndevu – imesalia na tai watano kulingana na wahifadhi wa wanyama. Sumu imelaumumiwa kuwa mojawapo ya sababu kuu ya kupungua kwa idadi ya ndege hao katika kipindi cha miongo mitatu iliopita kutokana na visa tofauti vya mzozo kati ya binadamu na wanyama.