Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Meya wa Moshi:Nimewapiga marufuku kuvaa barakoa kwasababu wanaleta taharuki
Iliyochapishwa
Meya wa manispaa ya Moshi, Kaskazini mwa Tanzania Bwana Juma Raibu Juma amewataka wajumbe waliovaa barakoa katika kikao cha baraza la madiwani kuzivua kwa madai kuwa manispaa hiyo ipo salama.
Ametoa agizo hilo siku ya Alhamisi ,wakati wa ufunguzi wa kikao cha bajeti cha baraza hilo baada ya kuwataka waliovaa barakoa kusimama na kisha kuwataka wavue.
Aidha amesisitiza kuwa barakoa hizo huenda zikasababisha maambukizi kwasababu zinatoka mataifa ya nje.
Mwandishi wa BBC ,Scolar Kisanga ameongea naye na kumuuliza kwanini amechukua uamuzi huo;