Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu ishirini na watano wauawa huko DR Congo
Iliyochapishwa
Maafisa mashariki mwa Congo wamesema takriban watu ishirini na watano wameuawa katika mashambulizi yanayoshukiwa kufanywa na waasi wa kundi la ADF katika mji wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini mkesha wa mwaka mpya.
Mkuu wa wilaya ya Beni Donat Kibwana amesema raia hao waliuawa katika mashamba yao mkesha wa leo.
Awali Caro Robi amezungumza na mtetezi wa haki za binadamu huko Beni Eli Vahumawa kutaka kujua zaidi hali ikoje mjini humo.