uchaguzi Uganda 2021: Waandishi habari Uganda waondoka katika mkutano ulioitwa na jeshi

Maelezo ya sauti, uchaguzi Uganda 2021: Waandishi habari Uganda waondoka katika mkutano ulioitwa na jeshi
Iliyochapishwa

Wanahabari nchini uganda wameondoka kutoka mkutano na wanahabari uliyokuwa umeitishwa na jeshi nchini humo , wanahabari hao waliondoka kama ishara ya kuonyesha ghadhabu yao , baada ya wenzao kujikuta kwenye patashika ya vurugu za kisiasa na walinda usalama , juma lililopita.

Jeshi la Uganda UPDF lilikuwa limeitisha mkutano na wanahabari kutangaza shughuli za hisani wakati wa wiki ya wanajeshi nchini humo .

isaac mumena anaripoti kutoka Kampala Uganda