Ni vigumu kwa watu kuamini kuwa wanaume wanaweza kubakwa, lakini wameamua kujitokeza

Iliyochapishwa

Ubakaji wa wanaume ni jambo ambalo ni mwiko katika maeneo mengi ya dunia, ikiwa ni pamoja na Afrika ambako kuna unyanyapaa unaohusiana na jambo hilo. Watu wengi hudhani wanaume hawawezi kuwa wahanga wa ubakaji. Lakini waathiriwa wa ubakaji wanajitokeza barani Afrika, kuzungumzia juu ya uzoefu wao, kusaidiana, na kuhakikisha masaibu waliyopitia yanafahamika. BBC imezungumza na wanaume wawili mmoja kutoka Kenya na mwingine kutoka Tanzania. Taarifa hii imeandaliwa na kuhaririwa na Ashley Lime na Anne Okumu.