Virusi vya corona: Chanjo ya kwanza ya Covid yaanza kutolewa Marekani

Chanjo

Chanzo cha picha, Getty Images

Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Chanjo ya kwanza ya Covid-19 huko Marekani imefanyika, wakati nchi hiyo ikijiandaa kwa kampeni yake kubwa zaidi ya chanjo.

Muuguzi wa wagonjwa mahututi huko Long Island, New York anaaminika kuwa mtu wa kwanza kupewa chanjo hiyo.

Mamilioni ya chanjo ya Pfizer / BioNTech inasambazwa, na hospitali 150 zinatarajiwa kupokea dozi Jumatatu.

Programu ya chanjo ya inakusudia kufikia watu watu milioni 100 ifikapo mwezi Aprili.

Vifo vilivyotokana na Covid-19 vinakaribia 300,000 nchini Marekani, ambayo ina idadi kubwa zaidi ya vifo ulimwenguni.

Chanjo ya Pfizer ilipokea idhini ya matumizi ya dharura kutoka kwa Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani (FDA) siku ya Ijumaa.

Utoaji wa chanjo hiyo unakuja wakati janga hilo linaendelea kuishambulia nchi. Vifo vimekuwa vikiongezeka sana tangu Novemba na idadi ya watu katika hospitali na ugonjwa pia imeendelea kuongezeka kwa kasi, na zaidi ya watu 109,000 wamelazwa kwa sasa, kulingana na Mradi wa Ufuatiliaji wa Covid.

"Nadhani labda imekuwa Desemba mbaya kabisa kwenye rekodi hapa. Kufikia wiki iliyopita, Covid-19 ndiye inayoongoza kwa kusababisha vifo huko Marekani, hata zaidi ya saratani na ugonjwa wa moyo," Dkt Dora Mills wa MaineHealth, mtandao wa Hospitali 12 huko Portland, Oregon, aliiambia BBC.

"Ni msimu wa giza sana kwetu, lakini pia ni ya ajabu kwamba tuna chanjo chini ya mwaka baada ya virusi hivi kujitokeza. Ikiwa data ya ufanisi na usalama itaendelea kuwepo, hii inaweza kuwa hatua kubwa zaidi ya kisayansi na mafanikio ya maisha yetu. "

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Presentational white space

Chanjo ya Pfizer / BioNTech - Ushirikiano kati ya kampuni kubwa ya dawa ya Marekani na kampuni ya bioteknolojia ya Ujerumani - inatoa hadi 95% ya kinga na ndio chanjo ya kwanza ya Covid-19 kupitishwa na wasimamizi wa Marekani.

Tayari inazinduliwa nchini Uingereza, wakati Canada pia inaanza mpango wake wa chanjo Jumatatu, na dozi 30,000 za awali zikienda kwenye maeneo 14 kote nchini.

Chanjo zinawekwa kwenye baridi wakati wa kusafirisha kwa kutumia barafu

Chanzo cha picha, EPA

Dozi milioni tatu za kwanza huko Marekani zinasambazwa katika maeneo kadhaa katika majimbo yote 50 na ndege ya mizigo na lori.