CUF 'Hatutashiriki tena Uchaguzi bila Tume huru'

Iliyochapishwa

Mwenyekiti wa chama cha upinzani cha CUF, nchini Tanzania kimesema chama chake hakitashiriki tena uchaguzi nchini humo mpaka Tume huru ya uchaguzi iundwe.

Profesa Ibrahimu Lipumba amesema hakubaliani na matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 28, kwa kuwa umegubikwa na mapungufu.

"Zoezi la kuwaapisha mawakala liliendeshwa kinyume Cha taratibu,Uchaguzi wa Mwaka huu haukuwa na siri. kwa sababu kwenye karatasi za kupiga kura ziko namba za vitambulisho vya wapiga kura."