Matokeo ya uchaguzi Tanzania 2020: Lissu apinga matokeo ya uchaguzi
Iliyochapishwa
Mgombea wa urais kupitia Chama cha upinzani nchini Tanzania, Chadema bwana Tundu Lissu ametangaza kutokubali matokeo ya uchaguzi.
Aidha amesema kuwa uchaguzi huu ulianza kuingia dosari mapema katika kuapisha mawakala ambao ndio waangalizi wa uchaguzi kwa niaba ya chama chao.
Lissu amewataka watanzania kudai haki yao kwa njia ya demokrasia na sio kwa vurugu yoyote .