Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Msajili wa vyama Tanzania: Miungano ya vyama inapaswa kuwasilishwa kwa msajili wa vyama miezi 3 kabla uchaguzi
Iliyochapishwa
Afisi inayosimamia usajili wa vyama nchini Tanzania imesisitiza kuwa vyama vya kisiasa vinapaswa kuheshimu sheria vinapoingia katika ushirikiano wa aina yoyote ama miungano kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini humo.
Afisi hiyo imesema kwamba vyama hivyo vinapaswa kuwasilisha ushirikiano au muungano huo kwa msajili wa vyama miezi mitatu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.