Maandamano kupinga ushindi wa Rais Alexander Lukashenko zaidi ya 6000 mbaroni

Maelezo ya video, Maandamano kupinga ushindi wa Rais Alexander Lukashenko
Iliyochapishwa

Mama huyu anamuita binti yake, akitarajia kuitika kwake kutamfariji wakati huu akiwa amekamatwa.

Binti yake ni miongoni mwa watu zaidi ya 6,000 walioripotiwa kukamatwa nchini Belarus wakati wa maandamano ya baada ya matokeo ya uchaguzi.

Alexander Lukashenko anaanza muhula wa sita wa urais nchini humo baada ya kushinda uchaguzi, ambao Umoja wa Ulaya umesema uchaguzi huo haukuwa ''huru na haki''.