George Floyd: Mtu aliyewapatia hifadhi waandamanaji 80 waliokuwa wamekwama katika kafyu Marekani

Maelezo ya video, George Floyd: Mtu aliyewapatia hifadhi waandamanaji 80 Marekani
Iliyochapishwa

Ilikuwa imepita muda wa kutotoka nje mjini Washington DC na waandamanaji walikuwa wamekwama baada ya polisi kufunga pande zote za barabara.

Ni wakati huo ambapo mkaazi mmoja alifungua mlango na kuwaruhusu kuingia nyumbani kwake.