Virusi vya corona: Wanafunzi Kenya watengeneza vifaa vya kukabiliana na virusi vya corona

Iliyochapishwa

Chuo Kikuu cha Kenya kimejitolea kutengeneza vifaa vya kukabiliana na virus dhidi ya corona. Chuo Kikuu hicho kinatengeneza kila kitu kuanzia barakoa hadi sare za wahudumu wa afya. Na sasa kinafikiria kuanza kutengeneza mashine za kupumua ili kuimarisha uwezo wa kupambana na ugonjwa wa Covid-19.