Uamuzi wa Tanzania kujitoa katika mahakama ya Afrika una athari gani?

Maelezo ya sauti, Tanzania yatuhumiwa 'kutata kiminya haki za binadamu'
Iliyochapishwa

Tanzania inasema imeamua kuitoa itifaki inayowaruhusu wananchi binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali kuishitaki Tanzania katika Mahakama ya Afrika ya Haki za Watu na Binadamu baada ya kujiridhisha kwamba itifaki hiyo inapingana na sheria za ndani za Tanzania.

Mwandishi wa BBC Yusuph Mazimu amezungumza na Mohamed Olotu, ambaye alihukumiwa kwenye mahakama za Tanzania kabla ya kwenda kwenye Mahakama hii na kushinda.

Kwanza alimuuliza amepokeaje uamuzi huu wa Tanzania?