Je mitandao ina msukumo gani katika maandalizi ya harusi?
Iliyochapishwa
Utafiti uliofanyika nchini Uingereza unaonyesha namna gani mitandao ya kijamii kama hasa zaidi Instagram na facebook inavyowasukuma wengi kutumia maelfu na hata mamilioni ya pesa kugharimia picha na video zilizo na mvuto. Utafiti huu mpya wa mwaka 2019 unaonesha kuwa gharama ya kuandaa na kupiga picha za harusi imeongezeka kwa wastani wa paundi thelathini na mbili elfu huko Uingereza. Mpangaji wa harusi nchini Gabriel Kudaka na mpigaji picha za harusi Imani Insamila kutoka Tanzania wameieleza BBC ni kwanini msukumo huu umekuwepo...