Albert Nabonibo: Msanii wa muziki wa kiinjili Rwanda aliyekiri kushiriki mapenzi ya jinsia
Iliyochapishwa
Msanii wa muziki wa kiinjili nchini Rwanda amekuwa raia wa kwanza wa nchi hiyo kukiri hadharani kuwa anashiriki mapenzi ya jinsia moja.
Albert Nabonibo mwenye umri wa miaka 35 ameiambia BBC kuwa anatarajia kukosolewa vikali kufuatia hatua huyo lakini yuko tayari kukabiliana na changamoto hizo.
Anasema kuwa utamaduni wa Wanyarwanda unapinga vikali mapenzi ya jinsia moja- na kwamba uamuzi wa kuweka wazi suala hilo umewagutusha mashabiki wake.
Msanii huyo amezungumza na mwandishi wa BBC Anne Ngugi.