Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ukingo wa magharibi: Matinga tinga yabomoa makaazi ya wapalestina huko Sur Baher
Maafisa wa usalama wameinga katika eneo la Sur Baher, katika eneo la Jerusalem mashariki, kuzibomoa nyumba hizo zinazoarifiwa kuwahifadhi watu 17.
Wakaazi wanasema walipewa vibali vya kuwaruhusu kujenga na mamlaka ya Palestina, na wameishutumu Israel kwa kujaribu kuinyakua ardhihiyo ya ukingo wa magharibi.
Palestina inasema "Huu ni muendelezo wa kuwatoa watu kwa lazima katika makaazi yao na ardhi zao - uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binaadamu,"
Israel inasema makaazi hayo yamejengwa kinyume cha sheria karibu na kizuizi chake kwenye ukingo wa magharibi.