Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
''Tuliongea naye kwenye simu akasema MV Nyerere inakaribia kuondoka”
Salome Lusatu ni miongoni mwa wale walipoteza ndugu na jamaa zao katika mkasa wa kusikitisha wa kuzama kwa kivuko cha Mv Nyerere alasiri ya tarehe 20.09.2018, Mkasa uligrarimu Maisha ya watu 226
Kivuko vha Mv Nyerere kilikuwa kwenye safari zake za kawaida kati ya kisiwa cha Ukerewe na Ukara kilipo pinduka na kuzama dakika chache kabla ya kukita nanga katika ufukwe wa Bwisya kisiwani Ukara
Salome tangu kumpoteza mumwe anasema Maisha yamekuwa ya upweke na anahofu mambo mengi yatabadilika kwani Mumewe walikuwa wakisaidia katika mambo mengi hayupo tena
Mwezi mmoja tangu kutokea kwa mkasa huo bado simanzi na majonzi zimeendelea kutawala katika kisiwa cha ukerewe
Mwandishi wa BBC Eagan Salla alimtembela mjane huyu.
Mtayarishaji: Eagan Salla.