Global Newsbeat: Mwanamuziki wa Destiny’s Child Michelle Williams akiri anatatizwa na msongo wa mawazo
Iliyochapishwa
Michelle Williams aliyekuwa katika kundi la Destiny's Child, amejiwasilisha katika kituo cha kuwasaidia watu kukabiliana na matatizo ya afya ya kiakili.
Awali, Williams alizungumza kuhusu kuwa na msongo wa mawazo na kutaka kujiua.
Je, unadhani watu maarufu wakiwa na uwazi kuhusu suala la ugonjwa wa akili basi watasaidia ili swala hili lizungumziwe hadharani? Tupe maoni yako kwenye ukurasa wetu wa Facebook, bbcnewsSwahili.