Wauza nyama wadaiwa kutumia dawa za maiti kuhifadhia bidhaa hiyo Uganda
Iliyochapishwa
Serikali ya Uganda imefanya msako mkali kwenye maduka ya nyama nchini humo baada ya kuwepo kwa taarifa kuwa baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakitumia dawa hatari zikiwemo za kuhifadhia maiti na zile za kuulia wadudu.
Wafanyabiashara hao wanadaiwa wamekuwa wakitumia kemikali hizo ili kuhifadhi nyama zisiharibike na waweze kuuziuza kwa muda mrefu.
Kutoka Kampala mwandishi wetu Isaac Mumena na taarifa zaidi.