Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Uyoga watunza msitu wa Nou
Iliyochapishwa
Tanzania ni miongoni mwa nchi kumi zinazopoteza misitu kwa kasi duniani kulingana na takwimu za benki ya dunia (world bank) na wanasema ikiendelea kwa kasi hiyo kwa miaka hamsini ijayo, Tanzania itakuwa haina misitu tena.
Lakini katika msitu wa Nou uliopo Manyara,kaskazini mwa Tanzania,baadhi ya wanakijiji wanaouzunguka msitu huo wameanzisha mbinu ya kutumia uyoga kama njia mbadala ya kujipatia kipato na kuokoa msitu huo.