Muigizaji maarufu wa filamu Idris Elba atangaza kuambukizwa virusi vya Korona.

Maelezo ya sauti, Muigizaji maarufu wa filamu Idris Elba ametangaza kuambukizwa virusi vya Korona.
Iliyochapishwa

Kupitia mitandao ya kijamii- muigizaji maarufu raia wa Uingereza Idris Elba ametangaza kuwa ameambukizwa virusi vya Korona. Elba amesema kuwa licha ya kutokuwa na dalili zozote za ugonjwa huo- alipatana na mtu aliyeambukizwa na hivyo akaamua kufanyiwa vipimo. Amewasihi mashabiki wake kuchukua tahadhari ya kujilinda kutokana na maambukizi hayo.